Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Friday, March 13, 2015

OSEPHAT KATABARUKI ALIVYOAGWA NA WAKAZI WA DAR


UMATI wa wakazi wa jijini Dar es Salaam jana ulifurika katika Kanisa ka KKT Mtoni-Mtongani kumuaga marehemu Josephat Katabaruki aliyefariki dunia ghafla Machi 9 mwaka huu nyumbani kwake Mtoni-Mtongani, Wilaya ya Temeke, Dar es Salaam.

Akizungumza na mtandao huu, mpwa wa marehemu ambaye ni ofisa mwandamizi katika kampuni ya Global Publishers Ltd, Laurence Kabende, aliomboleza na kusema ‘jembe’ la familia limeondoka ghafla na kuiacha familia yake katika wakati mgumu.

Mchungaji akihubiri

Marehemu Katabaruki anatarajiwa kuzikwa kijijini kwao Ruvinga, mkoani Kagera. Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi. Amen!

Laurence Kabende (wa pili kulia) akiwa na ndugu wa karibu katika viwanja vya Kanisa la KKT Mtoni-Mtongani.


Ndugu wa marehemu wakisubiri kuaga.


Gari lililobeba mwili wa marehemu likiwa jirani na mlango wa kanisa.

Jamaa wa karibu wakijadili jambo.


Marehemu Katabaruki enzi za uhai wake.


Mke wa marehemu (katikati) akiwa kanisani.

Laurence Kabende akielezea historia ya marehemu.


Ndugu na watoto wa marehemu wakimsikiliza Kabende.

Mtoto wa kike ambaye jina lake halikufahamika, akilia kwa uchungu baada ya kuuaga mwili wa baba yake.


Mke wa marehemu (katikati) akisaidiwa kwenda kuuaga mwili wa mmewe.
Kabenda akiwa na Meneja Mkuu wa Global Publishers, Abdallah Mrisho.

Akibadilishana mawazo na wahariri wa magazeti ya Championi (kushoto) na Mrisho (wa pili kulia).


Jeneza lenye mwili wa Katabaruki likiingizwa kwenye gari.

0 comments:

Post a Comment