Karibu Fadhaget Sanitarium Clinic

Tunapenda kukukaribisha katika Kitengo cha Sayansi ya Tiba Asilia.

Kitengo Cha Sayansi Ya Tiba Asilia

Kwa Muda mrefu tumekuwa tukisaidia wengi katika matibabu na kutengeneza dawa bora kabisa kiafya.

Je Unapenda Kufahamu Jinsi Ya Kupata Mapacha?

Tunafundisha jinsi ya kupata jinsia unayotaka, jinsi ya kupata mtoto kama umekosa mtoto kwa muda mrefu. Pia hata jinsi ya kupata watoto mapacha tunaweza kukusaidia.

Tunapatikana Katika Mikoa Zaidi ya 10 Tanzania

Tunazidi kuongeza matawi yetu nchini Tanzania na Nje ya Nchi. Kwa sasa tunapatikana katika mikoa zaidi ya 10 na tunazidi kuongeza matawi yetu. Karibu sana.

Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Saturday, March 29, 2014

DOKTA FADHILI EMILY WA THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC AKIWA OFISI ZAKE MWANZA

Baada ya kusikia kilio cha watu wa Mwanza, Dk. Fadhili Emily aliweza kutemmbelea watu hawa wa Mwanza ambao waliweza kufika katika ofisi za The Fadhaget Sanitarium Clinic Mwanza na kuongea machache. Dk Fadhili Emily aliweza kutoa huduma kwa wagonjwa waliofika mahali hapo na kutoa ushauri kwa wenye magonjwa sugu.


Dk Fadhily Emily

Wafanyakazi waliweza kuongea na mwasisi wa The Fadhaget Sanitariium Clini, Dk Fadhily Emily. Baada ya zoezi kumalizika wafanyakazi walionekana kusikitishwa walipoagana na doctor. Hii inatokana na upendo alionao Dk. Fadhili Emily.

Tuone baadhi ya matukio:








UNAFAHAMU UGONJWA WA KISUKARI NA SABABU ZAKE?

Ugonjwa wa Kisukari ni miongoni mwa magonjwa sugu yanayoendelea kuathiri afya za mamilioni ya watu wa nchi nyingi duniani ikiwamo Tanzania.

Ugonjwa huu hutokea pale ambapo tezi ya kongosho inaposhindwa kutengeneza kichocheo aina ya Insulin au pale mwili unaposhindwa kutumia vizuri kichocheo hicho na kusababisha kuongezeka au kushuka kwa kiwango cha sukari kwenye damu au hyperglycemia.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg2XeKd8RdhS86PIkpkNcmq10YvMMFPSpeVM30ebQABtAKpjEKhq-Y07XyIIYIah8tm4qQeRyoDnp3n36puDMHy_xrmVz7BjuYWKBdfuC_JOW7tvPqKArfQDogyDwkO-NkG-idXTaXlsQJ4/s1600/apples.jpg
Aina za kisukari
Kisukari kimeanishwa katika makundi yafuatayo:

Kisukari Namba Moja
Hii ni aina ya kisukari inayowaathiri zaidi watoto na vijana. Aina hii hutokea iwapo seli maalum zinazotengeneza homoni ya insulin zijulikanazo kama beta cells of Islet of Langerhans.

Iwapo tezi kongosho zitakosekana au zitaharibika kwa sababu yeyote ile, na hivyo kusababisha ukosefu kabisa au upungufu wa kichocheo hicho kwenye damu.

Mambo yanayoweza kusababisha uharibifu wa seli hizi katika tezi kongosho ni pamoja na kushambuliwa kwa tezi hiyo.

Mashambulizi katika kongosho huweza kufanywa na magonjwa yanayosababisha upungufu wa kinga ya mwili.

Uharibifu katika tezi kongosho hupelekea kukosekana kabisa kwa wa tezi ya insulin au huifanya tezi hiyo kuzalishwa kwa kiwango kidogo.

Wagonjwa wa aina hii ya kisukari huhitaji kupewa dawa za insulin kwa njia ya sindano katika maisha yao yoteili waweze kuishi. Ndiyo maana aina hii ya kisukari huitwa pia kisukari kinachotegemea Insulin au Insulin Dependent Diabetes Mellitus (IDDM)

Monday, March 24, 2014

SABABU ZA KUHARISHA KWA WATOTO

Utangulizi

Kuharisha kwa watoto ni tatizo linaloshika nafasi ya pili duniani kwa kusababisha vifo miongoni mwa watoto chini ya miaka mitano. Inakadiriwa kwamba kwa kila watoto 5 wanaofariki , 1 hufa kwa sababu ya kuharisha. Watoto milioni 1.5 kila mwaka hufa kutokana na kuharisha.
Leo hii, inakadiriwa asilimia 39 tu ya watoto wanaoharisha katika nchi zinazoendelea hupata matibabu sahihi.Hata hivyo, mwenendo wa kitakwimu unaonesha kwamba kumekuwa na mafanikio kidogo tangu mwaka 2000.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh22pnX6B55i7JkMI1VAh4Pq56hijCcQG49BiAxmD9YPu8O8WE9WQoRmOj8NH6ccmBwCTp6yCuSTVWQqQZTHh-RV0dwAkH6SzM-vTrSg9ul4rcCIy2wD_Lm09qmohiKKV6xKjfjNM5fdZ20/s400/6.jpg
Kuharisha huelezwa kuwa ni upotevu wa maji na madini muhimu kwa mwili wa binadamu (electrolytes) kupitia kinyesi na kupelekea upungufu wa maji mwilini. Katika hali ya kawaida, watoto wachanga hutoa kiasi cha gramu 5 za kinyesi kwa kila kilo ya mtoto (5g/ kg) kwa siku, wakati mtu mzima hutoa wastani wa gramu 200 kwa siku.

Sababu za Kuharisha kwa watoto

Kuharisha kunaweza kusababishwa na aina mbalimbali za vimelea ingawa pia kunaweza kusitokane na maambukizi ya vimelea (non-infectious causes). Vimelea vinavyosababisha kuharisha ni
Virusi: Virusi vinaongoza katika kusababisha tatizo la kuharisha kwa watoto katika nchi zilizoendelea na zinazoendelea.
Bakteria: Wanasababisha kuharisha kwa asilimia chache 2-10%. Kuharisha kunakosababishwa na bacteria husababisha upotevu mdogo wa maji ukilinganishwa na virusi. Mfano wa bakteria wanaoweza kusababisha tatizo hili ni Campylobacter, Salmonella, Shigella, na Escherichia coli
Parasite pia husababisha kuhara, lakini aina hii ya kuhara huwa ni sugu zaidi (chronic diarrhea) kwa ujumla na mara nyingi haiambatani na homa, kutapika, na upungufu wa maji mwilini. Giardia lamblia na Cryptosporidium parvum ni moja ya aina hii za parasire wanaosababisha kuhara.

Sababu ambazo hazihusiani na maambukizi ya vimelea yaani noninfectious causes ni pamoja na kula chakula kilichochanganywa na sumu au kumeza sumu, matatizo katika sehemu ya utumbo mwembamba na mnene, na matatizo ya usagaji chakula (metabolic abnormalities).

Kwa vile sababu kuu ya kuharisha ni kutokana na virusi, tutazungumzia aina kuu ya virusi wanaosababisha kuhara. Kuna aina takribani 4 wanaojulikana ambavyo ni Rotavirus, Adenovirus, astrovirus na norovirus. Kati ya hivi jamii ya Rotavirusndio wanaongoza duniani kote katika kueneza na kusababisha kuharisha kwa watoto wachanga na wadogo . Katika nchi zinazoendelea, Rotavirus ndiyo chanzo kikuu cha vifo vinavyotokana na kuhara miongoni mwa watoto chini ya umri wa miaka 5. Rotavirus huathiri wavulana na wasichana kwa uwiano sawa. Hatari zaidi ni kwa wale walio na uzito wa kuzaliwa chini ya gramu 1500 vilevile uzito kati ya gramu 1500-2499. Ukali wa ugonjwa ni mkubwa zaidi kwa watoto wenye umri wa miezi 3-24. Watoto wachanga chini ya miezi 3 wanapata sehemu ya kinga (antibodies) kutoka kwa mama anayenyonyesha na vilevile kinga mtoto aipatayo kupitia kondo la nyuma (placenta) kabla ya kuzaliwa. Kwa maana hiyo basi shambulizi la awali baada ya miezi 3 lina uwezekano wa kusababisha ugonjwa mkali zaidi.

Jamii hii ya Virusi wana uwezo wa kuenea kwa urahisi sana toka kwa mtoto mmoja kwenda kwa mwingine. Kimsingi wanaenea kwa njia ya kinyesi. Ni rahisi mtoto kupata uambukizi wa rotavirus iwapo atakula chembechembe za kinyesi zenye vimelea hivi. Mtu mwenye vimelea hivi anaweza kuambukiza mtu mwingine hata kabla ya dalili hazijaanza kujionesha kwake au hata siku kadhaa baada ya dalili kujionesha. Mtu aliyeambukizwa anaweza kutoa idadi kubwa ya vimelea hivi kiasi cha virion 1-10 kwa kila mililita ya kinyesi. Ili kuambukizwa kinahitajika kiasi kidogo tu cha hawa vimelea, takribani miligramu 0.000001. Hivyo ni rahisi kuambukizwa kwa kugusana au kwa kushika au kutumia vifaa vyenye maambukizi ya rotavirus. Aidha, rotavirus wamegunduliwa kuwepo katika majimaji ya kwenye kinywa na koo (oropharngeal secretions), ingawa bado haijathibitishwa kama kuna uwezekano wa maambukizi kwa njia ya hewa.

Muonekano wa mgonjwa

Watoto wanaohara kwa sababu ya rotavirusi huwa na dalili kuu tatu ambazo ni homa, kutapika na kuharisha. Kawaida choo kinakuwa cha majimaji sana. Tafiti zinaonesha kuwa asilimia 63 ya watoto wanaolazwa hospitalini kwa tatizo hili wanaonyesha dalili zote 3, asilimia 25 wanakuwa na dalili 2 tu. Wakati mwingine kuharisha kunaweza kujitokeza baadaye baada ya kutapika au homa. Joto la mtoto huwa si kali sana ingawa baadhi ya watoto wanaweza kuwa na joto kali linalozidi nyuzi joto 39 za sentigradi. Kutapika kunaweza kusiwe zaidi ya masaa 24. Vilevile wanaweza kuwa na kuchefuchefu, maumivu ya tumbo (abdominal cramping), kulia pasipo kutulia akibembelezwa (irritability) na uchovu.

Vifo husababishwa na upungufu wa maji mwilini. Upungufu wa maji waweza kuambatana na upungufu na kukosekana uwiano wa madini mwilini (electrolyte imbalance). Aidha kunaweza kusababisha madhara katika figo (ischemic injury to the kidneys) na katika mfumo wa neva (central nervous system) na kusababisha na mtoto kupoteza fahamu (shock).

Inashauriwa kuchunguza kiasi cha maji kilichopotea. Iwapo uzito wa mtoto utakuwa umepungua kwa zaidi ya asilimia 10, mtoto anaweza kuwa na dalili kama
kupoteza fahamu
kuwa na mapigo ya moyo ya kasi
kushindwa kula na kunywa
kuwa na macho yaliyolegea kulegea na kuingia ndani sana (severe sunken eyes)
kushindwa kutoa mkojo kabisa
kutotoa machozi na mdomo kuwa mkavu sana.

Upungufu wa kati ya asilimia 5-10 ya maji mwilini, husababisha
macho ya mtoto huingia ndani (sunken eyes)
ngozi kurudi taratibu pindi inapovutwa (loss of skin turgor)
mapigo ya moyo kuwa kasi
kuwa na ubonyeo katika sehemu ya mbele ya kichwa (depressed anterior frontanele)
uchovu
kiu na kunywa maji kwa haraka
mtoto kutoa machozi kidogo sana pindi anapolia
midomo kuwa mikavu na
kupumua kwa haraka kuliko kawaida

Chini ya asilimia 5 mtoto huwa na
kiu
ngozi inayorudi taratibu pindi ikivutwa
macho yanaweza kuingia ndani na
uchovu.

Unapoona dalili hizi wakati mtoto wako anaharisha unapaswa kumpeleka haraka kituo cha afya ili kupata ushauri wa wataalamu wa afya.

Uchunguzi

Kipimo cha choo: hujumuisha pia uchunguzi wa vimelea.
Kipimo cha antigeni cha Rotavirusi (Rotavirus antigen tests) ingawa asilimia 50 ya majibu yanaweza kuwa si sahihi (false-negative) hasa pale panapokuwa na damu kwenye choo.
Kupima kiwango cha sukari mwilini (blood glucose level)
Chembechembe nyeupe za damu kutambua maambukizi ya bakteria.
Kupimo cha figo (Renal function Test and electrolytes)
Vipimo vingine kutegemea na hali ya mgonjwa.

Matibabu
Ingawa yawezekana mtoto kupona bila hata matibabu lakini ni jambo muhimu kuchunguza madhara yanayoweza kusababishwa na upungufu wa maji mwilini. Ieleweke kuwa watoto wapo katika hatari kubwa zaidi ya ya kupungukiwa na maji mwilini kutokana na kuharisha, hivyo basi msingi wa matibabu ni kurudisha kiasi cha maji kilichopotea.

Hali kadhalika, matumizi ya madini ya zinc yamehusishwa na kupungua kwa makali ya ugonjwa na kupunguza muda wa kuharisha.

ORS ambayo ni mchanganyiko wenye uwiano mzuri wa chumvi na sukari ni aina ya tiba inayopendekezwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa ajili ya matibabu. Uwiano uliopo katika ORS huwezesha utumbo wa mtoto kufyonza vizuri maji na madini mengine.

Matibabu ya kuharisha kwa watoto yanaweza kugawanywa katika awamu kuu mbili:
Kurudisha maji yaliyopotea (rehydration)
Kuendelea kuupa mwili maji kwa ajili ya mahitaji ya kila siku (Maintenance)

Mlezi hushauriwa namna ya kutengeneza mchanganyiko huu ORS kulingana na hali ya mtoto. Kwa mama wanaonyonyesha, wanashauriwa kuendelea kumnyonyesha mtoto mgonjwa huku akimpa mlo wa kawaida wa kila siku. Ikiwezekana, ni vema pia kuendelea kumpa mtoto maji ya ziada. Kama mtoto akitapika, mzazi/mlezi anashauriwa kusubiri kwa angalau dakika 5-10 kabla ya kuendelea tena kumnywesha kidogo kidogo (kwa mfano, kijiko kila baada ya dakika 2-3).

Watoto walio na hali mbaya na wale waliopoteza zaidi ya asilimia 10 hawana budi kupewa maji kwa njia ya mishipa ya damu yaani intravenous fluids.

Kwa vile chanzo kikuu cha kuhara kwa watoto ni maambukizi ya virusi, haishauriwi kutumia antibiotics kama sehemu ya matibabu. Hata hivyo antibiotics zinaweza kutumika tu pale ambapo itathibitika kuwa kuharisha kumesababishwa na bakteria.

Dawa za kuzuia kuharisha kama vile Loperamide hazishauriwi kwavile athari zake ni mbaya zaidi kwa mtoto kuliko faida.

Namna ya kuzuia maambukizi
Kuzingatia usafi wa chakula (kupika na kuhifadhi).
Kunawa mikono kila baada ya kutoka chooni, kabla ya kushika chakula na wakati wa kula
Kuwa makini na watoto wanaoharisha ikiwezekana kuwatenga na wenzao
Matumizi ya Chanjo: Usalama wa chanjo ya Rotavirus bado haujathibitishwa rasmi hasa kwa watoto chini ya wiki 6. Aidha chanjo hii imekuwa ikihusishwa na kutokea kwa matatizo katika utumbo mkubwa na mdogo.

KARIBUNI THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC

Thursday, March 20, 2014

SABABU ZA KUTOKA HARUFU MBAYA UKENI NA NAMNA YA KUJIKINGA

Wanawake na watu wengi huzani kuwa harufu mbaya itokayo ukeni ni matokeo ya uchavu na kutojisafisha vizuri… Matokeo yake huongeza jitihada katika kujisafisha bila mafanikio ya kuondokana na tatizo hili… Kihalisi, badala kusuluhisha, unapojisafisha zaidi ni unaongeza tatizo badala ya kutatua… Japokuwa ni kweli mara nyingine inaweza ikawa ni sababu ya uchafu… Ila mimi naamini walio wengi huwa wanazingatia usafi… Ndo maana nimeona leo tupeane mawazo juu ya tatizo hili, na kujua namna ya kujikinga

http://thegrio.files.wordpress.com/2012/06/bad-smell-16x9.jpg?w=650&h=366

VISABABISHI
i. Bacteria
Tatizo hili husababishwa na Bakteria kwa asilimia kubwa. Kwa asili, ukeni huishi jamii ya bacteria waitwao Lactobacillus ambao jukumu lao kubwa ni kufanya mazingila ya uke kuwa katika hali nzuri. Kutokana na njia mbaya za kusafisha uke, hasa kujisafisha kupindukia, ama kwa kutumia sabuni zenye dawa, husababisha bacteria hawa kufa kwa wingi na mahala pake kuchukuliwa na aina zingine za bacteria ambao huzaana kwa wingi na kusababisha tatizo hili.

Pia kwa wale wanaojamiiana kinyume na maumbile, kuna hatari ya kuhamishia bacteria wanaoishi kwenye njia ya haja kubwa na kuwaamishia ukeni ambapo watazaliana na kukuletea madhala haya.

ii. Kuvu(fungus)

Hii mara nyingi huambatana na uchafu mzito utokao ukeni mfano wa maziwa mgando(mtindi)


iii. Magonjwa ya zinaa(STIs)
Kwa asilimia kubwa husababisha na Chlamyidia na kisonono(gonorrhoea). Yote mawili hutibika kirahisi, ila husababisha madhala makubwa zaidi yasipotibiwa kwa wakati. Tukio baya ni kuwa mwanamke anaweza akawa na magonjwa haya na asione dalili yoyote. Ila mara nyingine mwanamke anaweza kujisikia maumivu anapokojoa, na mara nyingine mkojo unakuwa kama una ukungu, vikiambatana na harufu mbaya.


iv. Maambukizi ya via vya uzazi vilivyo ndani ya nyonga[Pelvic Inflammatory Diseases(PID)]
Hii husababishwa na bacteria waambukizwao kwa njia ya ngono wanapofanikiwa kufika kwenye tumbo la uzazi na hata pia mirija ya mimba na hata kokwa(ovaries), hasa chlamydia. Mara nyingi mwanamke anaweza asijisikie chochote hadi pale atakapojisikia maumivu yasiyokwisha ya tumbo(chini ya kitovu), au itakapoingiliana na utungaji wa mimba. Na kama atajisikia, mara nyingi huwa ni maumivu ya nyonga, harufu mbaya, uchafu mzito ukeni, homa, maumivu wakai wa kukojoa na hata maumivu wakati wa kujamiiana.
Tatizo hili lisipotibiwa mapema laweza kusababisha utasa, ama mimba kutunga nje ya mji wa mimba.

v. Kansa ya uke na kansa ya shingo ya kizazi
Asilimia chache sana ya wanawake inaweza ikawa ni kutokana na kansa ya shingo ya kizazi ama ya uke. Hapa ndipo inapoonyesha kuwa tatizo hili siyo la kufumbia macho, na umuhimu wa kuwahi kwa wataalam wa tiba kwa uchunguzi wa mapema na kabla tatizo halijawa kubwa.

vi. Uchafu
Usipokuwa msafi kwa kiwango kikubwa utakuwa unakaribisha wadudu kuzaliana na kukuletea madhala. Pia unatakiwa kuwa makini wakati wa hedhi, na pia uchaguzi wa pedi, kwani kuna pedi ambazo zina kemikali za kukata harufu zinaweza kukudhulu.


JINSI YA KUJIKINGA
• Usiwe unaosha ukeni kupita kiasi kwani husababisha kuondoa bacteria wa asili wa ukeni(Lactobacilli) na kukaribisha bacteria wenye madhala.

• Pia epuka sabuni zenye dawa(antibacterial soap) usafishapo ukeni, kwani hii pia huua bacteria wa asili wa ukeni.

• Hii haimaanishi usiwe unasafisha ukeni. Usafi ni muhimu, kwani uchafu pia hukaribisha vimelea vya magonjwa.

• Kama tatizo limeshajitokeza, wahi haraka kwa wataalam wa tiba wakufanyie uchunguzi na kujua ni kipi kati ya vilivyotajwa hapo juu kilichosababisha. Daktari atakuchunguza na kujua kama ni bacteria, fungus ama ni dalili za awali za kansa na kuchukua hatua mapema kuepusha madhala zaidi.

• Kumbuka kujisafisha kupindukia si suluhisho kama tatizo limeshajitokea, kwani kunaweza kuzidisha tatizo badala ya kusuluhisha.

SABABU ZA KUTOKUSHIKA MIMBA

Tatizo la baadhi ya wanandoa kutokushika mimba limekuwa likiongezeka mwaka hadi mwaka na wengine hukata tamaa mapema kwani huweka fikra za kupata mimba kuanzia mwezi wa kwanza wa ndoa yao.
Mtu ambaye ana tatizo la kutoshika mimba kitaalamu tunasema Infertility na kushindwa kupata mimba kwao huitwa Conceive. Kwa kawaida kwa mujibu wa tafiti mbalimbali, wanandoa asilimia 50 wanapata mimba ikiwa watajamiiana bila kutumia kinga wakifanya tendo hilo ndani ya miezi mitatu na asilimia 75 baada ya miezi sita na asilimia 95 baada ya mwaka mmoja.
http://www.visualphotos.com/photo/2x4591395/profile_of_pregnant_african_woman_with_bare_belly_BLD024020.jpg
Sababu za tatizo la kutopata mimba ni nyingi sana na baadhi yake ni hizi zifuatazo.
Matatizo ya mbegu za kiume (Sperm disorders). Asilimia 35 ya wanaume wana tatizo hili na lingine ni kutopevuka kwa mayai kwa wanawake yaani kitaalamu huitwa Ovalatory dysfunction, asilimia 20.
Matatizo mengine ni yale yasiyo ya kawaida ya ute wa shingo ya uzazi ambapo ni asilimia 5 tu, wengine huwa na matatizo ya homoni na wapo ambao hawapati mimba na sababu zao hazijulikani ni asilimia 10, wengine ni kutokana na kuwa na msongo wa mawazo na wasiwasi.

Tatizo lingine la kutoshika mimba husababishwa na hitilafu katika mirija ya uzazi (tubal dysfunction), hawa huwa asilimia 30. Sababu zote hizi nitaeleza moja moja kwa kirefu katika matoleo yetu yajayo lakini wote wenye tatizo hili wanashauriwa kuhudhuria kliniki za akina mama ili waonane na madaktari.
Lakini pia wanashauriwa kufuatilia siku zao za mzunguko wa hedhi na tendo la ndoa mara kwa mara hasa baada ya siku 10 kutoka siku anamaliza hedhi na aanzie siku ya kwanza ya kupata hedhi. Ushauri Wanawake wanashauriwa wawe wanapima joto la mwili asubuhi na jioni kipindi cha kushika mimba na kama litaongezeka kwa nyuzi joto 0.5 wanashauriwa kipindi hicho kufanya tendo la ndoa.
Kwa nchi za Ulaya na Marekani wana kipimo cha kuonesha siku ambayo yai litapevuka, hivyo mtu kuwa na uhakika na siku ya kupata mimba akiamua.

Kipimo hicho kinaitwa Luteinizing hormone prediction test kits. Wanawake wanaotaka kupata mimba wanashauriwa kuepuka ulevi na uvutaji wa sigara wa kupindukia. Lakini hata wale wenye mimba wanashauriwa kuepuka vitu hivyo.

Itaendelea siku nyingine.

DK. FADHILI EMILY WA THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC AKIFANYA MAHOJIANO REDIONI

Hivi karibuni niliweza kufanya mahojiano katika moja ya radio hapa jijini Dar es Salaam kuhusiana na huduma bora zinazotolewa na The Fadhaget Sanitarium Clinic zilizopo Mbezi ya Tegeta eneo la  Afrikanasana barabara ya Salasala.


Dk. Fadhili Emily wa The Fadhaget Sanitarium Clinic

Saturday, March 15, 2014

TAWI JIPYA LA THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC LAFUNGULIWA MKOA WA DODOMA

The Fadhaget Sanitarim Clinic chini ya mkurugenzi Dk. Fadhili Emily inapenda kukujulisha ya kuwa sasa huduma yetu inapatikana katika mkoa wa Dodoma. Hii ni kutokana na wananchi wa mkoa wa Dodoma kuhitaji huduma yetu ambayo imefanyika msaada mkubwa kwa maelfu ya wagonjwa walipona kwa kupitia dawa zinazosambazwa na clinic yetu.

Kwa hiyo mkazi wa Dodoma na mikoa ya jirani huna sababu ya kupoteza nauli yako na muda wako wa kufika Dar es Salaama kwa matibabu. Huduma hii imekufikia mlangoni ili uweze kupona, sio kipindi cha kupoteza muda wa kufunga safari kufika katika makao yetu makuu hapa jijini Dar es Salaam. Huduma zinazopatikana hapo ndizo zinazotolewa Dar es Salaama.
Dodoma tunapatikana Dodoma mjini karibu na soko kuu Majengo ni ghorofa ya kwanza kulia kwako kama unaelekea stand ya Mshikamano.
Tupigie kwa ushauri
+255 712 705 158 | +255 757 931 376 | +255 787 705 158
+255 757 505 158 | +255 774 505 158 | +255 787 505158
DR. Fadhili Emily

THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC TUNGEPENDA KUKUJULISHA KUHUSIANA NA VIDONDA VYA TUMBO

The fadhaget Sanitarium Clinic tungependa kukujulisha machache kuhusiana na vidonda vya tumbo. Kwa maelezo zaidi fika katika ofisi zetu hapa Dar es Salaam maeneo ya Afrikana barabara ya Salasala na mikoani utasaidiwa


Dr. Fadhili Emily



Ugonjwa wa vidonda vya tumbo hutokea iwapo kidonda cha ukubwa wa angalau wa nusu sentimita kitatokea kwenye sehemu yeyote ya ukuta wa tumbo au utumbo wa binadamu. Kwa kawaida tatizo hili huleta maumivu makali sana ya tumbo ingawa si lazima kila maumivu ayapatayo mgonjwa husababishwa na vidonda vya tumbo.

Tafiti zimeonesha kwamba karibu asilimia 70 mpaka 90 ya vidonda vya tumbo husababishwa na aina ya vimelea vya bakteria wajulikanao kama Helicobacter pylori. Aidha matumizi ya baadhi ya dawa za kutuliza maumivu za jamii ya Non Steroid Anti-inflamatory Drugs kama Aspirin au Diclofenac huweza kusababisha au kuongeza uwezekano wa kupata ugonjwa huu.

Kuna dhana iliyozoeleka kuwa vidonda vya tumbo huathiri zaidi mfuko wa kuhifadhia chakula yaani tumbo (stomach). Dhana hii si kweli kwani sehemu inayoadhiriwa zaidi na tatizo hili ni sehemu ya kwanza ya utumbo mdogo ijulikanayo kama duodenum.

Makundi ya PUD

Kuna makundi makuu yafuatayo ya ugonjwa huu

1. Vidonda vinavyotokea kwenye mfuko wa kuhifadhia chakula yaani tumbo (Gastric ulcers)
2. Vidonda vinavyotokea kwenye sehemu ya kwanza ya utumbo mdogo (Duodenal Ulcers)
3. Vidonda vinavyotokea kwenye koo (Oesophageal ulcers)
4. Vidonda vijulikanavyo kama Merckel’s Diverticulum ulcers.


Visababishi vya PUD

Vidonda vya tumbo husababishwa na

Maambukizi ya bakteria aina ya Helicobacter pylori: Imeonekana kuwa zaidi ya asilimia 50 ya watu duniani wana vimelea hivi katika utumbo. Aidha, miongoni mwao, karibu asilimia 80 huwa hawaoneshi dalili yeyote ya kuugua ugonjwa wa vidonda vya tumbo.

Aina hii ya vimelea vya bacteria husababisha karibu asilimia 60 ya vidonda vinavyotokea kwenye tumbo (gastric ulcers) na zaidi ya asilimia 90 ya duodenal ulcers.

Hali hii husababishwa zaidi na kushindwa kwa mfumo wa kinga mwilini kuwaua na kuwaondoa kabisa vimelea hawa ndani ya mwili. Matokeo ya kushindwa huku husababisha kuwepo kwa uambukizi wa kudumu katika kuta za tumbo (chronic active gastritis), uambukizi ambao huharibu mfumo na uwezo wa kuta za tumbo kutunza homoni ya Gastrin, ambayo ni muhimu katika kuhakikisha mazingira ya tumbo yanakuwa na kiwango salama cha tindikali.

Kwa kawaida, kazi ya gastrin ni kuchochea utolewaji wa tindikali (gastric acid) kutoka kwenye seli za ukuta wa tumbo zijulikanazo kama Parietal cells. Iwapo bacteria hawa watashambulia na kuharibu ukuta wa tumbo, mfumo wa gastrin pia uharibika, na hivyo kusababisha gastrin kuzalishwa kwa wingi hali ambayo pia huchochea uzalishaji wa gastric acid kwa wingi. Matokeo ya kuzalishwa kwa wingi kwa tindikali hii hupelekea kuchubuka kwa ukuta wa tumbo na hivyo kusababisha vidonda vya tumbo.

Matumizi ya muda mrefu ya dawa za kuondoa maumivu za kundi la NSAIDs: Ukuta wa utumbo hujilinda na madhara yatokanayo na tindikali ya utumbo (gastric acid) kwa kuwa na utando laini (mucus) ambao hutolewa na vichocheo vijulikavyo kama Prostaglandins. Dawa hizi za kundi la NSAIDs huharibu mfumo wa kutengeza vichocheo hivi yaani prostaglandins na hivyo kufanya kuta za tumbo kukosa utando wa kuzilinda na mashambulizi ya tindikali hali ambayo hupelekea kutokea kwa vidonda vya tumbo.

Uvutaji wa sigara: Uvutaji sigara sambamba na maambukizi ya bakteria aina ya Helicobacter pylori huongeza madhara ya ugonjwa wa vidonda vya tumbo. Ifahamike tu kuwa uvutaji sigara pekee hausababishi vidonda vya tumbo.

Vyakula au viungo vya chakula vyenye uchachu: Kinyume na dhana iliyozoeleka miongoni mwa watu wengi, baadhi ya vyakula vyenye uchachu na upilipili kama vile pilipili, ndimu, limao na masala havina uhusiano na uwezekano wa kupata vidonda vya tumbo.

Watu walio katika kundi la damu la O: Imeonekana pia kwamba kundi la damu lijulikanalo kama blood group O, halina uhusiano wa kusababisha vidonda vya tumbo.

Unywaji wa pombe: Unywaji wa pombe pekee hausababishi vidonda vya tumbo. Hata hivyo, unywaji wa pombe sambamba na maambukizi ya vimelea vya Helicobacter pylori huongeza madhara ya ugonjwa wa vidonda vya tumbo.

Vitu vingine: Vitu vinavyohusishwa na uongezaji wa madhara ya vidonda vya tumbo ni pamoja na upasuaji wa tumbo (major abdominal surgeries), kuungua kwa moto (burns), ugonjwa wa figo; na kubadilishwa kwa viungo vya mwili kama figo au ini.

Dalili au viashiria vya PUD

Maumivu makali au kiungulia maeneo ya chembe moyo (epigastic pains): Maumivu juu kidogo ya tumbo mara nyingi huendana na muda wa kula chakula. Mtu mwenye vidonda kwenye tumbo (gastric ulcers) hupata maumivu makali sana kipindi anapokula au mara tu baada ya kumaliza kula wakati aliye na vidonda kwenye sehemu ya kwanza ya utumbo mdogo (duodenal ulcers) hupata maumivu makali anapokuwa na njaa na hupata nafuu pindi anapokula.


Kuvimbiwa au tumbo kujaa gesi. Hali hii pia yaweza kuendana na kubeua au kujamba mara kwa mara.
Kucheua na kuongezeka kwa mate yanayoshuka tumboni baada ya kucheua.
Kichefuchefu na kutapika
Kupoteza hamu ya kula na kupungua uzito
Kutapika damu
Kupata haja kubwa cha rangi nyeusi au kahawia chenye harufu mbaya sana. Hii humaanisha mgonjwa anapata haja kubwa au choo kilichochanganyika na damu kwa mbali Uwepo wa dalili kama kiungulia cha muda mrefu, kucheua na kutapika baada ya kula na historia ya kutumia dawa za kupunguza maumivu (NSAIDs) kwa muda muda mrefu bila kufuata ushauri wa daktari ni ishara tosha ya kumfanya mgonjwa kumuona daktari kumpima na kumfanyia uchunguzi ili kujiridhisha kuwa hana tatizo la vidonda vya tumbo.

Vipimo vya kutambua Ugonjwa wa vidonda vya tumbo

Vipimo vinavyotumika katika kutambua tatizo la vidonda vya tumbo ni pamoja na

1. Vipimo vya kuangalia ndani ya utumbo ambavyo ni pamoja na


Kipimo cha oesophagogastroduodenoscopy (EGD) au Upper GI endoscopy au gastroscopy. Kwa kutumia kipimo hiki, daktari huangalia moja kwa moja ndani ya utumbo wa mgonjwa kuona sehemu iliyo na vidonda pamoja na ukubwa wa tatizo lake. Aidha vipimo hivi humuwezesha daktari kuchukua sehemu ya utumbo iliyoathiriwa kwa ajili ya kuchunguza zaidi maabara ili kutambua uwepo wa vidonda au tatizo jingine linalomsumbua mgonjwa tofauti na vidonda vya tumbo.
Kipimo kingine kijulikanacho kama Barium meal kina uwezo pia wa kuthibitisha uwepo wa ugonjwa wa vidonda vya tumbo. 2. Vipimo vya kutambua uwepo wa uambukizi wa bakteria aina ya Helicobacter pylori kama


Kipimo kiitwacho Urea breath test
Kipimo cha kuotesha kinyama kilichochukuliwa kutoka katika kipimo cha OGD (culture from an OGD biopsy specimen).
Kipimo kinachoitwa Rapid Urease Test ambacho hufanywa kwa kutumia kinyama kilichochukuliwa kutoka kwenye utumbo wakati wa kufanya OGD. Kipimo hiki huangalia tabia ya vimelea hawa wa H. pylori.
Kipimo cha damu kwa ajili ya kutambua kiwango cha maambukizi ya vimelea wa H. pylori (antibody levels).
Kipimo cha haja kubwa kwa ajili ya kutambua kama bacteria wapo hai au wamekufa (stool antigen test). Kipimo hiki ni cha uhakika zaidi na nafuu kuliko kipimo cha Urea Breath Test.
Kipimo cha kimaabara cha kuchunguza kinyama kilichochukuliwa wakati wa kipimo cha OGD. 3. Vipimo vingine maalum vya kitaalamu zaidi kama


Kiwango cha homoni ya gastrin katika damu
Kipimo cha kuangalia uzalishaji wa homoni ya secretin ambayo uhusika katika uchocheaji wa homoni ya gastrin
Kupima kiwango cha tindikali inayozalishwa katika tumbo. Hata hivyo vipimo hivi ni vya gharama zaidi na ni aghalabu hutumika mara kwa mara.

Matibabu ya Ugonjwa wa vidonda vya tumbo

Habari nzuri ni kuwa ugonjwa huu wa vidonda vya tumbo unatibika. Hata hivyo tabia ya baadhi ya wagonjwa wengi kuacha kumalizia dawa au kutumia dawa chini ya kiwango tofauti na walivyoshauriwa na madaktari husababisha kujirudia kwa tatizo au kufanya tatizo kuwa sugu zaidi.

Iwapo itagundulika uwepo wa H. pylori tiba inayotumika ni kuchanganya dawa za antibayotic (antibiotic) za aina tofauti kama Amoxicillin, Tetracycline, Clarithromycin au Metronidazole na dawa zenye uwezo wa kupunguza uzalishaji wa tindikali kwa wingi au kwa kitaalamu Proton Pump Inhibitors (PPI). Wakati mwingine daktari anaweza pia kuongeza dawa ya Bismuth Compound.

1. Kwa wagonjwa sugu, dawa za antibioc za aina tatu tofauti zinaweza kutumika. Dawa hizi ni pamoja na Amoxicillin + Clarithromycin + Metronidazole ambazo hutumika sambamba na dawa yeyote moja kutoka kundi la PPI kama vile Omeprazole au Pantoprazole pamoja na Bismuth Compound.

2. Kwa mgonjwa wa kawaida ambaye si sugu tiba bora inayoshauriwa ni kuchanganya dawa za antibiotic za aina mbili kama Amoxycillin + Metronidazole sambamba na dawa yeyote moja ya jamii ya PPI kama Pantoprazole.

3. Iwapo hakuna ushahidi wa kuwepo kwa uambukizi wa bacteria, dawa yeyote moja ya jamii ya PPI yaweza kutumika kwa muda mrefu zaidi bila kuchanganya na antibiotic yeyote.

Kwa kawaida kitendo cha kutibu na kuwaondoa Helicobacter Pylori humaliza na kuponyesha kabisa vidonda vya tumbo.

Hata hivyo, inawezekana kabisa ugonjwa huu kujirudia tena, hali ambayo hulazimisha kurudiwa tena kwa matibabu kwa kutumia aina nyingine ya antibiotics.

Aidha msomaji, inashauriwa si vyema kwa mgonjwa kujitibu mwenyewe bila kufuata ushauri wa daktari ili kuepuka madhara yanayoweza kutokea iwapo dawa hazitatumiwa inavyopaswa.

Ni kweli Maziwa ya ng’ombe yanaponyesha vidonda vya tumbo?

Kinyume na dhana iliyozoeleka ndani ya jamii, maziwa ya ng'ombe hayaponyeshi vidonda vya tumbo, bali huongeza madhara yatokanayo na ugonjwa huu. Hii ni kwa sababu, maziwa huwa na tabia ya kutengeneza aina fulani ya kinga au ukuta (protective coat) kwa vimelea vya Helicobacter Pylori ambayo huvikinga vimelea hivi dhidi ya mashambulizi ya dawa na hivyo kufanya dawa kushindwa kuwaua na kuwaondoa kabisa vimelea hivi.

Kinachotokea ni kuwa, maziwa huondoa tu kwa muda maumivu ya tumbo kwa kupunguza makali ya tindikali iliyopo tumboni. Pindi maziwa haya yanapoisha, maumivu hurejea tena na kuwa makali kama hapo awali.

Matibabu ya vidonda vya tumbo kwa njia ya upasuaji

Zipo aina nyingi ya upasuaji unaofanywa ili kutibu ugonjwa huu. Kuvuja damu ndani ya mwili kupitia vidonda vya tumbo ni sababu mojawapo ya kufanyiwa upasuaji kwa vile ni hatari sana hata kupelekea kifo iwapo mgonjwa hatapata tiba haraka.


Endoscopy: ni njia inayotumika kutibu uvujaji wa damu unaotokana na vidonda vya tumbo. Aina hii ya tiba hutegemea sana aina na sehemu vilipo vidonda vya tumbo. Tiba hii yaweza kufanyika kwa kuchoma sehemu inayovuja damu ndani ya tumbo au utumbo kwa lengo la kusitisha uvujaji wa damu (cautery) au kwa kuvifunga vidonda kwa kutumia vifaa maalum (clippings). Aidha tiba hii ni nzuri na haina madhara yeyote yale.
Madaktari wengi hupendelea upasuaji ujulikanao kitaalamu kama simple oversewing sambamba na tiba ya kuondoa bakteria. Aidha, mgonjwa pia hushauriwa kuacha matumizi ya dawa za NSAIDs kwa ajili ya kuondoa uwezekano wa damu kuendelea kutoka kwa vile kama ilivyoonekana hapo awali, matumizi ya dawa hizi huweza kusababisha uvujaji wa ndani kwa ndani ya mwili.
Wagonjwa sugu, hufanyiwa baadhi ya upasuaji ambao huitaji utaalamu wa hali ya juu katika kuondoa neva na mishipa ya fahamu yenye kuhusika na uzalishaji wa tindikali katika tumbo. Madhara ya ugonjwa wa vidonda vya tumbo

Uvujaji wa damu ndani ya utumbo: Hali hii yaweza kusababishwa na vidonda kuenea hadi kwenye mishipa ya damu na hivyo kufanya damu kuanza kuvuja. Hali hii ni hatari sana na inahitaji tiba ya dharura.
Vidonda vya tumbo huweza kusababisha tundu (kutoboka kwa ukuta wa tumbo) na kufanya vitu vilivyo ndani ya utumbo kutapakaa katika tumbo (abdomen) Hali hii huitwa peritonitis na ni hatari sana na inahitaji matibabu ya dharura. Aidha, kuenea huko kunaweza pia kuathiri tezi kongosho na kusababisha madhara katika tezi hiyo, ugonjwa unaojulikana kama pancreatitis.
Vidonda vya tumbo vinaweza pia kuenea na kuathiri pia viungo vya jirani kama vile ini au kongosho (pancrease)
Kuvimba kwa kuta za tumbo pamoja na makovu yasababishwayo na vidonda hivi huweza kusababisha kuziba kwa njia ya kupitishia chakula kutoka kwenye tumbo (stomach) kwenda sehemu ya kwanza ya utumbo mdogo (duodenum) hali ambayo kitaalamu huitwa gastric outlet obstruction.
Iwapo vidonda vya tumbo vimesababishwa na H. pylori, kuna uwezekano wa kati ya mara tatu hadi ya sita ya mgonjwa kupata kansa ya tumbo (stomach cancer).

PEPTIC ULCERS

Ulcers of the stomach (gastric ulcers) and the duodenum (the first part of the intestines after the stomach) are together known as peptic ulcers.
Symptoms
Although most peptic ulcers are quite small, they can be incredibly painful. This pain tends to be:

A constant gnawing or burning pain.
Located in the upper, central abdomen (but may penetrate into the back).
Worse at night or in the early morning.
Worse if you miss a meal.
Relieved by food or 'white medicine' such as antacids or milk.
Other symptoms include:

Tiredness.
Nausea and vomiting.
Indigestion or heartburn, vomiting blood or passing blood in the stools (this may be the only sign of an ulcer).
Anaemia, caused by blood loss, resulting in paleness and shortness of breath.
However, some people have no symptoms at all.

If left untreated, peptic ulcers may cause rapid internal bleeding, which can be very dangerous, or a perforation or obstruction in the intestines.

Causes and risk factors
Peptic ulcers occur when the membrane lining the digestive system breaks down or erodes. This membrane normally stands up to some fairly tough challenges, containing and churning up food particles while resisting the effects of the stomach's powerful digestive juices.

The discovery that the bacteria Helicobacter pylori (H.pylori) is the main cause of these ulcers has been one of the great success stories of modern medicine.

Several mechanisms protect the digestive membrane, but under certain conditions these fail, allowing acid and digestive enzymes to cause damage. These conditions include:

Infection with H. pylori - many people carry this bacteria, and while not everyone with H. pylori develops an ulcer, almost everyone with an ulcer has H. pylori.
Non-steroidal anti-inflammatory drugs (NSAIDs) - these include aspirin, ibuprofen and many painkillers used for conditions such as arthritis. Ulcers and haemorrhage are a common problem with these drugs.
Smoking.
Excessive amounts of alcohol.
Other factors that increase the risk of an ulcer include a family history of ulcers and being blood group O.

It used to be thought that high levels of stress could cause ulcers, but many doctors now think emotional stress simply accentuates the pain of an existing ulcer and may interfere with healing.

Events that put mmense physical stress on the body, such as severe burns, major surgery or a major trauma, do seem to be linked to peptic ulcers.

Tests to confirm the diagnosis of an ulcer include:

Gastroscopy - a thin tube or endoscope is passed into the stomach to look at the digestive membrane.
Barium studies - a substance called barium is swallowed and then highlights ulcers on an x-ray.
Tests will also look for the presence of H. pylori. These may involve a blood test, breath test or biopsy of the digestive membrane.

Treatment and recovery If H. pylori is detected,
The main treatment is eradication therapy. This usually means taking a combination of two antibiotics and a drug that suppresses stomach acid production for a week. It's commonly known as 'triple therapy'.

It's also important to cut down on factors that can aggravate an ulcer, such as smoking, and stop taking any NSAIDs.

Although medical treatments usually cure the ulcer, an operation is still required in some cases. This may involve cutting the main nerve that controls acid production in the stomach (the vagus nerve) or removing part of the stomach itself.

THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC YAFUNGUA OFISI MKOA WA TANGA

The Fadhaget Sanitarium Clinic inapenda kukujulisha wewe mkazi wa Tanga na mikoa ya jirani ya kwamba sasa tumefungua ofisi yetu mpya mkoa Tanga. Hii ni kutoka na wananchi wa mkoa wa Tanga kuhitaji huduma yetu iwafikie, watu wamekuwa wakusumbuliwa na magonjwa mbalimbali na kuwasababishia hata kushindwa kufanya kazi, na hii imechangia sana hata uchumi wa nchi kushuka kwani watu hawafanyi kazi kutokana ma magonjwa yanayowasumbua. The Fadhaget Sanitarium clinic kwa kuona hilo ikishirikiana na wananchi wa mkoa huo ikaamua kufungua tawi linginge la tiba.

Ofisi yetu ipo Tanga mjini  barabara ya 16 kama unaelekea Makolola ni kituo cha mzimuni, nyumba ya 7 kushoto  kama  unaelekea jele ya watoto.

Dk. Fadhili Emily wa The Fadhaget Sanitaium Clinic

Ofisi ya The Fadhaget Sanitarium Clinic Tanga

Makao makuu ya huduma hii ya The Fadhaget Sanitarium Clinic yako  jini Dar es Salaam eneo la Mbezi Afrikana barabara ya Salasala.

Jengo jipya la The Fadhaget Sanitarium Clinic (Makao Makuu) hapa Bongo

FAIDA 5 ZA MAJI AMBAZO HAZIZUNGUMZIWI SANA

The Fadhaget Sanitarium Clinic tunakushauri kunywa maji ya kutosha ili kuwa na afya njema. Sehemu kubwa ya mwili wako ni maji. Kila seli kwenye mwili wako unahitaji maji ili kuchukua chakula na kutoa uchafu. Pia maji yanahitajika kwa usafirishaji mwilini, sehemu kubwa ya damu ni maji. Faida hizo zimezungumzwa sana na hivyo umesisitizwa kunywa maji walau lita moja na nusu kwa siku ili kuwa na afya njema. Kuna faida nyingine za maji ambazo huwa hazizungumziwi sana, na hizi hapa ni baadhi tu ya faida hizo
Drinking Water Testing

1. Kunywa maji kwa wingi kunakufanya uonekane kijana. Mwili wako ukiwa na maji ya kutosha inazuia ngozi kukunjamana na hivyo mtu kuonekana na ngozi nyororo hata kama umri umekwenda.

2. Kupunguza uzito/unene. Kama hupendezwi na uzito ama unene wa mwili wako ukinywa maji mengi utapunguza uzito wako. Unywaji wa maji mengi unapunguza uzito wa mwili kwa sababu;
Ukinywa maji mengi unapunguza hamu ya kula hivyo hutoweza kula chakula kingi kinachosababisha uzito kuwa mkubwa. Pia maji yanasaidia uunguzwaji wa mafuta mwilini na kusidia kuondoa sumu mwilini.

3. Kujenga misuli. Mwili unapokuwa na maji ya kutosha unaweza kusambaza hewa ya oksijeni vizuri zaidi na hivyo misuli ya mwili inaweza kufanya kazi kwa muda mrefu bila kuchoka. Hii inasaidia kujenga misuli ya mwili.

4. Kuongeza akili, ndio unywaji wa maji unaongeza uwezo wa kufikiri na kuweka kumbukumbu. Hii ni kwa sababu maji yanasambaza chumvi zinazohitajika na seli za fahamu kwa ajili ya kusafirisha taarifa mbalimbali. Tafiti zinaonyesha kwamba ukinywa glasi 10 za maji unaongeza uwezo wa kufikiri kwa asilimia 30. Jaribu kama huamini.

5. Unywaji wa maji mengi unasaidia viungo kufanya kazi vizuri. Kunakuwa na majimaji ya kutosha kwenye viungo yanayozuia maumivu ya viungo.
Kwa kifupi hizo ni baadhi tu ya faida za kunywa maji ya kutosha. Kiwang cha kunywa inabidi kisiwe chini ya glasi nane kwa siku. Kunywa maji utunze afya yako

Wednesday, March 12, 2014

HABARI KUTOKA MITANDAONI: JE WAJUA SIMU YAKO YA MKONONI YAWEZA SABABISHA UKAZAA MTOTO MTUKUTU? SOMA HAPA



MIONZI ya simu za mkononi inaweza kuathiri maendeleo ya ubongo wa watoto walioko tumboni mwa mama zao, utafiti umeeleza.Utafiti huo umetaja madhara mengine ya mionzi ya simu za mkononi kuwa ni uharibifu wa manii, mimba, kupungua kwa nguvu za kiume, kupoteza kumbukumbu na kuzaa watoto watukutu.

Pia umeeleza kuwa matumizi kupita kiasi ya simu hizo, husababisha mtindio wa ubongo na upungufu wa udadisi kwa watoto tangu udogo wao.

Hata hivyo, utafiti huo uliofanywa na Shule ya Tiba na Dawa ya Chuo Kikuu cha Yale, Marekani na kuripotiwa na Gazeti la The Telegraph la Uingereza, umepingwa na watafiti wengine, wakisema haujakidhi baadhi ya vigezo ili kuuthibitisha.
Kiongozi wa jopo la utafiti huo, Profesa Hugh Taylor alisema utafiti huo ulioanzia kwa panya, baadaye ulithibitika kwa binadamu.

Profesa Taylor ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya Uzazi, Magonjwa ya Wanawake na Sayansi ya Uzazi, alisema: “Tulikuwa na panya wenye mimba katika maboksi na tuliwawekea simu juu ya vichwa vyao. Panya tuliokuwa tumewaweka katika bwawa lile, nusu yao walikuwa wazima na nusu yao walikufa. Panya waliokuwa hai tuliwaacha wajifungue na baada ya kujifungua, tukaanza kutafiti watoto wao.”
“Panya ambao hawakuwa karibu na simu za mikononi walionekana kuwa werevu. Kumbukumbu zao hazikupungua ikilinganishwa na panya walioathiriwa na mionzi ya simu za mikononi ambao katika vipimo vya awali wakiwa tumboni, walionekana kuhangaika.”

“Panya hao wenye mimba waliowekwa kwa siku 17 katika boksi hilo na simu kupigwa mfululizo juu ya vichwa vyao, walizaa watoto watukutu na waliokosa kumbukumbu.”
Aliongeza: “Matokeo hayo yanaweza kutokea kwa binadamu pia. Mjamzito anayetumia simu ya mkononi muda mwingi, anaweza pia kuzaa taahira.”

Utafiti huo umebaini kuwa kati ya asilimia tatu na saba ya watoto wenye umri wa kwenda shule, wana tatizo la utukutu linaloweza pia kuathiri maendeleo yao kitaaluma. Alisema kiwango hicho kimekuwa kikiongezeka kwa asilimia tatu kila mwaka tangu mwaka 1997.

Profesa Taylor alisema anaamini kuwa simu za mikononi pia ni sababu ya baadhi ya watoto kukosa adabu na pengine kutokuwa makini katika mambo mbalimbali wanapokuwa watu wazima.

“‘Huu ni utafiti wa kwanza unaoonyesha ushahidi wa madhara ya mionzi ya simu za mkononi. Tumeonyesha kuwa matatizo ya tabia katika panya yalitokana na mionzi ya simu za mkononi waliyoipata wakiwa tumboni,” alisema Profesa Taylor na kuongeza:

“Kuongezeka kwa utovu wa nidhamu kwa watoto kunaweza kuwa sehemu ya madhara ya mionzi ya simu, ambazo mama zao walikuwa wakizitumia wakati wao wakiwa bado tumboni.”

Profesa Taylor alifanya utafiti huo kwa kuwachukua panya 33 wenye mimba na kuwaweka kwenye boksi lenye nyavu kisha kuweka simu juu yake. Simu hiyo ilikuwa ikiita mfululizo kwa siku 17.
Pia aliwaweka panya wengine 33 katika mazingira ya aina hiyo lakini hakuweka simu juu ya boksi hilo.
“Zaidi ya watu 160 waliofanyiwa utafiti wa aina hiyo pia walionekana kuwa na tofauti za kitabia ambayo inaweza kuhusishwa na utafiti huo.

Hata hivyo, Profesa Taylor alisema kuna haja ya kuendelea kufanya utafiti zaidi ili kubaini sababu ya mionzi hiyo ya simu kuathiri watoto walio tumboni mwa mama zao na namna bora ya matumizi ya simu kwa wanawake wajawazito.

Mtaalamu huyo anatarajia kuungana na wenzake akiwamo Dk Devra Davis, anayeongoza Shirika lisilo la Kiserikali la Mazingira na Afya la “Environmental Health Trust” kwa ajili ya utafiti zaidi kuhusu madhara ya simu.

Mwaka 2011, Shirika la Kimataifa la Afya Duniani linalojihusisha na uchunguzi wa kansa, lilidai kuwa mionzi ya simu inaweza kusababisha kansa na hivyo jopo hilo la madaktari linaendelea na utafiti zaidi.

Nchi nyingine duniani ikiwamo Ufaransa, ilipiga marufuku kwa kampuni za matangazo ya simu kwa watoto kutokana na hatari mbalimbali zinazoweza kuwatokea.

Utafiti huo uliochapishwa katika Jarida la ‘Scientific Reports’ wiki iliyopita
Lengo la utafiti
Ongezeko la matatizo ya magonjwa wa mishipa ya fahamu, matatizo mbalimbali ya ubongo pamoja na magonjwa ya akili, ni mojawapo ya mambo yaliyochagiza kufanyika kwa utafiti huo.
Dk Hugh alisema simu za mkononi hazina madhara kwa watu wazima kama inavyodaiwa na wengi, lakini ni vifaa vyenye kuleta athari kubwa kwa watoto walio tumboni.

“Matatizo yanayowapata watoto wa binadamu walio wengi hivi sasa ikiwa ni pamoja na magonjwa ya mtindio wa ubongo, mishipa ya fahamu inasababishwa na matumizi ya simu za mkononi kwa mama wajawazito pamoja na kukaa nazo jirani kwa muda mrefu.”

“Haijalishi mama anaongea na simu au la! Mionzi inapenya na kuleta madhara pia kusababisha kazi ya ukuaji wa mtoto katika ubongo kulegalega, wapo ambao wanalala na simu kitandani zikiwa zimewashwa... hii ni hatari zaidi labda iwe imezimwa,” anasema Dk Hugh.

Watalaamu Dar
Akizungumzia utafiti huo jana, Mkurugenzi wa Teknolojia ya Nyuklia wa Taasisi ya Mionzi Tanzania (Taec), alisema ni vigumu kuukosoa utafiti huo kwa sasa hadi hapo Shirika la Afya Duniani (WHO), litakapotoa tamko sahihi ingawa alisema mionzi ina athari kubwa kwa binadamu.

“Nilipata kusoma utafiti huo katika mitandao siku mbili zilizopita, ni utafiti ambao umewekwa wazi, kwa kweli hata mimi ulinishtua, lakini ni mapema kuzungumzia hilo kwa sasa. Kwani utafiti huo bado unakinzana kwa mambo mengi, licha ya kupingwa pia na baadhi ya wanasayansi.

“Nadhani ni muda mwafaka sasa kufanya uchunguzi kwa binadamu na si kutumia panya kama walivyofanya Chuo Kikuu cha Yale. Hata hivyo, jopo la madaktari pia wanatarajia kufanya kikao chao mapema wiki hii, labda tutapata maoni mapya.”

Alisema kwa kawaida mionzi ina madhara kwa binadamu, lakini bado kuna maswali mengi kwa wanasayansi duniani ambayo bado hayajapatiwa ufumbuzi, hivyo inawawia vigumu Taec kutoa ufafanuzi wowote kuhusu athari hizo.

Meneja wa Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Innocent Mungy alisema utafiti huo unaweza kuwa msaada mkubwa kwa nchi kama Tanzania ambayo hivi sasa ndiyo imechipukia katika matumizi ya simu za mkononi.

Source: Vituko Vya Mtaa

Tuesday, March 11, 2014

MATUNDA NI MUHIMU SANA KATIKA MWILI WAKO

The Fadhaget Sanitarium Clinic tunakushauri uanze sasa kutumia matunda kwaani ya umuhimu sana katika mwili wako. Kuna mambo mengi unaweza kufaidika katika utumiaji wa matunda katika mwili wako. Pia unashauriwa kupenda sana kutumia mbogamboga mara kwa mara kwa afya yako.


Dr. Fadhili Emily

LEO TUTAANGALIA FAIDA ZA MACHUNGWA MWILINI MWAKO

Faida ya jamii ya machungwa watu wengi kujua. Ni muhimu sana ladha na matunda. Labda kwa sababu hii kwamba wanawake na kuja na chakula kulingana na matunda chungwa. Ingawa chakula machungwa sio mpya. Bibi Royal katika Ufaransa, pia, akaketi juu ya chakula kama hiyo.

Pamoja na hayo, si tu kupoteza uzito lakini pia kudumisha freshness wa ngozi, urembo, nywele, kutakasa mwili na kukuza afya kwa ujumla. Hivyo, kutaja kwanza ya chakula machungwa unaweza kuhusishwa na karne ya 15. Kisha hadithi juu yake, kuja na. Favorite Ukurasa wa Mfalme Louis 14 Ninon de Laclos ni walipanga kila siku kwa ajili ya machungwa kumi.

Pamoja na kwamba ni gharama kubwa sana kwa mfalme, lakini matokeo yalikuwa na thamani yake: uzuri wake na ngozi walikuwa ili kamili, bila kujali umri. Tangu wakati huo, kama vile matunda jamii ya machungwa machungwa akawa maarufu. Orange ni mwakilishi mkuu wa familia ya matunda jamii ya machungwa.
image001

Ana ladha brightest, vitamini C, ambalo kuzuia au kuepuka SARS na baridi ya kawaida. Aidha, machungwa ina ladha wengi, ni rahisi kuharibu microbes. Na muhimu mafuta imefikia katikaOrange, kufanya harufu na ladha ya matunda zaidi expressive. Matumizi ya mara kwa mara ya machungwa husaidia kuondoa sumu mwilini.

Kwa hivyo wengi sifa muhimu, machungwa, na kuvutia ya tahadhari ya wanawake. Naye, kwa upande wake, alikuja na chakula na msingi juu yake. Kukubali machungwa juu ya ratiba maalum kwa kiasi haki inaweza kuzuia njaa kwa muda. Kalori mwili si kufanya hivyo maalum, lakini faida kwamba nitakupa sana.

Basi nini uhakika machungwa mlo? Kuna wawili variants kuu yake: mlo kwa siku 14 na siku 21. - Chakula cha mchana katika machungwa na yai kuchemsha, unaweza kunywa lita 0.3 ya mtindi na kuongeza michache crackers; - Kwa chakula cha jioni nyanya mbili, ya wanandoa wa mayai kuchemshwa na majani ya saladi. Katika mlo machungwa kwa muda wa siku 14 kwa kutumia mayai tu siku ya kwanza. Kisha kuchukua nafasi yao nyama kuchemsha katika siku ya pili na ya tatu.

Next siku mbili, mabadiliko ya nyama ya curd. siku ya sita ya samaki kila siku mvuke (kuchemsha au Motoni inawezekana). Wiki ijayo ni sawa na ya kwanza kuanza na mayai na kuishia katika samaki. wiki mbili machungwa chakula husaidia kupoteza fedha juu ya 7 na kusafisha mwili vizuri.

Chaguo pili machungwa mlochakula kwa muda wa siku 21 (wiki tatu). Ni atawaokoa kutoka uzito kupita kiasi na 15kg. Chakula Hii ni zaidi rigid na muda mrefu kuliko mtangulizi wake.

Kulingana na haja yake kwa kuzingatia madhubuti na mahitaji yafuatayo: no sigara, pombe, na kuondoa kabisa kutoa juu ya kahawa na vinywaji aina hiyo. Mazoezi ya viungo katika kipindi hiki lazima dhaifu. Hivyo, chakula machungwa kwa muda wa siku 21 kama ifuatavyo: - Wakati wa wiki ya kwanza ya mlo wako wa kila siku lazima na wajumbe tu wa bidhaa hizo hadi pauni machungwa, kuchemsha mayai mawili yanaweza kuoshwa chini na maji ya madini, lakini si zaidi ya lita 2 kwa siku.

- Katika wiki ya pili kuendelea kula vizuri, lakini kuongeza oatmeal, kuchemshwa katika maji, unsalted na bila mafuta. - Wiki ya tatu hupunguza kiasi cha maji ya kunywa kwa siku hadi lita moja; uji mabadiliko ya matunda au mboga ambazo zinaweza kuliwa wakati wowote katika siku kwa wingi yoyote. Kuna wengi tafsiri ya machungwa mlo. Wao hutofautiana idadi ya siku ya chakula chakula, na kunywa inaruhusiwa.

Lakini jambo inabakia ile ile: kiwango cha thamani, kusafisha mwili wa kuendeleza na kurejesha uzuri na softness, kukata rufaa kwa ujumla, na, hivyo, hali nzuri.

TUMIA MATUNDA MENGINE KAMA HAYA HAPA CHINI KWA AFYA YAKO


Dr. Fadhili Emily

















Thursday, March 6, 2014

THE FADHAGET SANITARIUM CLINICM - KITENGO CHA SAYANSI YA TIBA ASILIA TUMEFUNGUA MATAWI SABA MIKOANI



Dk. Fadhili Emily wa The Fadhaget Sanitarium Ckinic
Tunahusika na kutibu magonjwa karibia yote, hasa yaliyo sugu kama vile vidonda vya tumbo, figo kufa ganzi, miguu kuwaka moto, kuvimba miguu na unapobonyeza linabaki shimo, kisukari, pumu, moyo, mapafu, sickle cell (upungufu wa damu), kuziba kwa mirija ya uzazi, uvimbe wa kizazi, matokeo ya dalili za hatari katika via vya uzazi kama vile kuwashwa, vipele kutokea pembeni mwa mlango wa uzazi, kutoka kwa uchafu kama maziwa ya mgando katika eneo la uzazi, kutokuwa na hamu ya tendo la ndoa, mimba kutoka, kuzaa mtoto jinsia unayotaka, matatizo ya chango la uzazi, upungufu au ongezeko la siku za kike yaani hedhi, upungufu wa kinga mwilini (CD4 na CD8), na dalili nyingine za hatari kiafya.


The Fadhaget Sanitarium Clinic tunapatikana

1. DAR ES SALAAM
Mbezi Beach Afrikana njia ya Salasala


2. MWANZA

Tunapatika Mwanza mjini Kilimahewa kituo cha Mnazi mmoja barabara mpya ya lami

3. ARUSHA
Arusha tunapatikana round about ya Florida nyuma ya Galax

4. MBEYA
Mbeya tunapatikana mjini karibu na Shule ya Msingi Sisimba au karibu na Mbeya Peak Hotel

5. ZANZIBAR
Zanznibar tunapatikana Unguja barabara kuu ya Amani, kituo cha Gongo Store

6. TANGA
Tanga tunapatikana Tanga mjini barabara ya 16 kituo cha Mzimuni ni nyumba ya 7 kushoto kama unaelekea jela ya watoto.

7. DODOMA
Dodoma tunapatikana Dodoma mjini karibu na soko kuu Majengo ni ghorofa ya kwanza kulia kwako kama unaelekea stand ya Mshikamano.

Logo au nembo ya The Fadhaget Sanitarium Clinic

Tupigie kwa ushauri
+255 712 705 158
+255 757 931 376
+255 787 705 158
+255 757 505 158
+255 774 505 158
+255 787 505158

DR. Fadhili Emily

Fuatilia vipindi vyetu kupitia
1. Star TV: saa 3:30 usiku Jumatatu usiku (kila siku) baada ya idhaa ya BBC London .
2. Radio Free Africa: Kila siku za Jumamosi saa 3:30 baada ya taarifa ya michezo
3. Channel 10: Kila siku za Jumatano saa 11:00 jioni
4. Praise Power Radio: Kila siku za Jumanne na Alhamis saa 2:00 usiku hadi 3:00 usiku.


Mara nyingi watu tumekuwa tukiishi bila kujali afya zetu, pengine kutokuona umuhimu wa afya au kutokuwa na elimu ya kutosha kuhusu afya kwa kutambua hilo The Fdhaget Sanitarium Clinic kitengo cha Sayansi ya Tiba Asilia, tumeamua kuungana na jamii katika kutoa elimu ya afya. Katika vyombo vya habari kama vile TV, vituo vya redio, vipeperushi, CD, DVD, na vitabu vinavyoelimisha kuhusu afya. Hili litatufanikisha kuweza kufahamu umuhimu wa afya zetu.

CD zenye mafundisho juu matumizi ya simu na madhara yake, zinapatikana ofisini kwetu

Tunashauri ndugu zetu jamaa na marafiki umuhimu ya kutibiwa au kujitibu kwa kutumia dawa zitokanazo na mimea na matunda asilia, kwani hazina kemikali yoyote ambazo zaweza kusababisha usumbufu mwingi katika miili yetu. Bali dawa hizi zinatusaidia virutubisho, madini, na vitamin muhimu katika mwili.

Maasai nao baada ya kuhangaika sana kutafuta njia ya kutatua matatizo yao ya magonjwa waliweza kufika The Fadhaget Sanitarium Clinic na kukutana na Dk.  Fadhili Emily kwa vipimo na tiba.

Tunawatakia afya njema na Mungu awabariki
Kutana na DR. Fadhili Emily wa The Fadhaget Sanitarium Clinic kwa ushauri na tiba ya afya, waweza kupiga kwa ushauri
+255 712 705 158
+255 757 931 376
+255 787 705 158
+255 757 505 158
+255 774 505 158
+255 787 505158

DR. Fadhili Emily

THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC KWA VIPIMO NA TIBA
UMUHIMU WA KUTIBIWA NA DAWA ZITOKANAZO NA MIMEA NA MATUNDA ASILIA

Kutokana na uumbaji wa Mungu ilipendekezwa na Mungu mwenyewe, mwanadamu ajitibu au atibiwe kwa kutumia uasili alioupata katika bustani ya Eden, ambao kwa hakika ni miti, majani na matunda mbalimbali ya porini, ushahidi soma Ezekiel 47:7-12, fungu hili linazungumzia jinsi na namna ya matunda na majani yalivyobarikiwa kwa njia ya uponyaji.

Utumiaji wa dawa zitumikazo na mimea na matunda asilia, humuwezesha mgonjwa apate kujitibu salama pasipo ongezeko la kemikali au sumu yoyote katika mwili, ziwezazo kutokana na dawa za kemikali ambazo kwa hakika tumekuja kupata baada ya mapinduzi ya viwanda, ambapo kwa hakika zimeanza karne ya 19 mpaka karne hii tuliyonayo hivi leo.

Kutana na wahudumu mbalimbali kutoka kona mbalimbali za dunia kuweza kusaidiwa na tiba itokanayo na mimea asilia.

Kwa maoni na ushauri tupigie kwa namba zifuatazo
+255 712 705 158
+255 757 931 376
+255 787 705 158
+255 757 505 158
+255 774 505 158
+255 787 505158
DR. Fadhili Emily wa Fadhaget Sanitarium Clinic

Tunamshukuru Mungu kwa kuisaidia The Fadhaget Sanitarium Clinic kupata huu usafiri ambao umekuwa msaada mkubwa sana katika utafutaji madawa maporini na kusaidia wagonjwa wanapokuwa wamezidiwa majumbani mwao au mahali popote pale.

TEMBELEA BLOGU YETU
www.fadhaget.blogspot,com