Karibu Fadhaget Sanitarium Clinic

Tunapenda kukukaribisha katika Kitengo cha Sayansi ya Tiba Asilia.

Kitengo Cha Sayansi Ya Tiba Asilia

Kwa Muda mrefu tumekuwa tukisaidia wengi katika matibabu na kutengeneza dawa bora kabisa kiafya.

Je Unapenda Kufahamu Jinsi Ya Kupata Mapacha?

Tunafundisha jinsi ya kupata jinsia unayotaka, jinsi ya kupata mtoto kama umekosa mtoto kwa muda mrefu. Pia hata jinsi ya kupata watoto mapacha tunaweza kukusaidia.

Tunapatikana Katika Mikoa Zaidi ya 10 Tanzania

Tunazidi kuongeza matawi yetu nchini Tanzania na Nje ya Nchi. Kwa sasa tunapatikana katika mikoa zaidi ya 10 na tunazidi kuongeza matawi yetu. Karibu sana.

Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Saturday, May 30, 2015

DR. FADHILI EMILY WA THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC AKIWA SAFARI SWEDEN KWAAJILI YA KUNUNUA VIFAA VYA TV YAKE YA TV51

Watanzania mapinduzi yamepamba moto kupindua mazoea tuliyozoea kuona katika TV zetu. Muonekano mpya, watangazaji waliosomea utangazaji kwa kiwango cha juu, waongozaji wa kimataifa vipindi vya TV, nyimbo za dini na za kijamii zenye muonekano tofauti na tulivyozoea kuona katika luninga zetu, vifaa vya kisasa na vyenye ubora wa picha na sauti kutumika katika luninga mpya ya TV51 ndani ya Mbezi Beach Dar es Salaam Tanzania.
Dr Fadhili Emili wa The Fadhaget Sanitariu Clinc Mbezi Beach Dar es Salaama Tanzania akiwa Sweden.

Dr. Fadhili Emily ambaye ni Mkurugenzi wa THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC ambayekwa sasa  yuko nchini  Sweden katika harakati za kununua vifaa vya kisasa vya TV yake ya TV51, amesema anamshukuru Mungu kwa kuweza kumfanikisha kusafiri salama kutoka Tanzania hadi Sweden kwa zoezi zima la kuinua uchumi wa Tanzania kwa kupitia TV yake ambayo itakuwa na vipindi vipya kabisa ambavyo havijawahi kuonekana katika vituo vyetu vya hapa nchini.

Dr. Fadhili Emily aliyevalia Tshirt nyekundu

The Fadhaget Sanitarium Clinic ambayo imethamiria kuondoa tatizo la watu kukosa ajira, na ndio maana ikaona ni vyema kuanzisha TV ambayo itaajiri watu wengi sana na pia watu wataweza kuonyesha taaluma zao, viapaji vyao, biashara zao, huduma zao nk kwa kupitia vipindi mbalimbali vilivyobuniwa kwa ufasaha na ustadi. Kwahiyo Watanzania tutegemee mambo makubwa sana kutoka THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC.
Dr Fadhili Emily
 Dr Fadhili Emily
 Dr. Fadhili Emily
  Dr. Fadhili Emily
  Dr Fadhili Emily

BLATTER ASHINDA TENA URAIS WA FIFA



Sepp Blatter baada ya ushindi.


Blatter akiwa na mpinzani wake Prince Ali bin al-Hussein wa Jordan.

SEPP Blatter ameshinda tena Urais wa FIFA kwa awamu ya tano baada ya kumshinda mpinzani wake Prince Ali bin al-Hussein wa Jordan.

Blatter amepata kura 133 dhidi ya 73 za mpinzani wake huyo katika raundi ya kwanza ya kinyang'anyiro hicho kilichofanyika nchini Uswizi jana licha ya kukumbwa na skendo za ufisadi.

P FUNK AMESHAJIPATIA KADI YA TAMASHA LA FLORA MBASHA



Tamasha hili kubwa ambalo litafanyika Ubungo Plaza limedhaminiwa na THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC. Msikose kufika muone Flora Mbasha anavyomtukuza Mungu kwa njia ya uimbaji na kutambulisha bendi yake ya LIVE


TUZO YAMTIA ‘UCHIZI’ IRENE PAUL!

Brighton Masalu
STAA wa filamu Bongo, Irene Paul ‘Smart Girl’ amezua mshangao baada ya kupiga mayowe huku akirusha mikono kushangilia tuzo aliyopata jambo lililozua miguno kwa waliomshuhudia.


Staa wa filamu Bongo, Irene Paul ‘Smart Girl’ akitahayari wakati wa kuchukua tuzo.

‘Katukio’ hako ‘amazing’ kalishuhudiwa na paparazi wetu mwishoni mwa wiki iliyopita ndani ya Jengo la Mwalimu Nyerere, Posta jijini Dar kulikokuwa na sherehe ya utoaji Tuzo za TAFA na kuwafanya baadhi ya watu kuacha kila kitu kwa muda na kumtumbulia macho.

Msanii huyo alipata tuzo hiyo kwa kipengele cha The Best Actress (Supporting Role) kupitia Filamu ya Never Give Up aliyoshirikiana na msanii kutoka Nigeria, Joseph Van Vicker na kuonekana kuchanganyikiwa namna hiyo.

Baada ya kuchukua tuzo hiyo, ‘kiruka njia’ wetu alimfuata na kumuuliza kulikoni aonekane kupagawa kwa kiwango hicho ambapo alisema kutokana na ugumu wa kipengele hicho kwani alikuwa akichuana na watu anaowaheshimu sana katika tasnia ya filamu, alioamini wana kiwango cha juu kuliko yeye hivyo hakuamini kilichokuwa kinatokea kwa wakati huo.

Wednesday, May 27, 2015

MUONEKANO MPYA WA MWIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI TANZANIA, NEEMA GASPER


LIFAHAMU TATIZO LA UVIMBE KATIKA NJIA YA HAJA KUBWA (BAWASIRI)-2




Wiki iliyopita tulianza kupeana elimu juu ya tatizo la kuota kijinyama katika njia ya haja kubwa (bawasiri). Tuliangalia chanzo cha ugonjwa huu na nikawapa ushauri kwamba ukiona una tatizo hilo ni vema ukawa huru maana ni ugonjwa wa kawaida na unatibika kama magonjwa mengine. Hivyo ni vema ukawahi katika vituo vya tiba ili upate matibabu mapema na kuepukana na adha za ugonjwa husika. Leo tutaangalia dalili za ugonjwa huu wa bawasiri.

Kwa kuwa ugonjwa huu hutokea katika eneo ambalo humfanya mgonjwa ajisikie aibu na dalili zake ni mgonjwa mwenyewe ndiye anaweza kuziona na asijisikie vibaya kuwaeleza wataalamu wa afya ili apewe matibabu mara moja. Dalili za ugonjwa huu ni kama zifuatazo;

Kwanza kabisa ni maumivu wakati wa kujisaidia haja kubwa. Wengi hupata maumivu makali sana wakati wa kutoa haja kubwa. Na wengine mpaka wanatokwa na machozi kwa maumivu lakini wanakaa kimya wanaona kama ni hali ya msimu itakwisha. Napenda kukujulisha kuwa hali hiyo si ya kawaida ni dalili ya ugonjwa huu wa bawasiri ni vema uonapo hali hiyo wahi katika vituo vya tiba.

Kinyesi kuwa na harufu ya damu wakati wa kujisaidia. Niwakumbushe kuwa unapoona damu kwenye kinyesi ni dalili kuwa kuna tatizo katika njia yako ya haja kubwa hivyo unapaswa kuchuka hatua za haraka kujua sababu ya damu hiyo kutoka.

Wakati mwingine kutokana na tatizo hili kushambulia njia ya haja kubwa kuna wakati mgonjwa atashindwa kuzuia haja yake na hivyo haja kuvuja. Hilo si jambo la kawaida ni viashiria vya hatari katika mfumo wa haja kubwa.

TIKETI ZA TAMASHA LA FLORA MBASHA ZINAPATIKANA SASA


DAKTARI: MBONI MASIMBA ILIKUWA AFE




Imelda mtema
Mtangazaji mahiri wa Kipindi cha The Mboni Show kinachorushwa kupitia Televisheni ya Taifa ya TBC1, Mboni Masimba, amejikuta akiangua kilio kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar, alipotembelea wodi ya wazazi na kusimulia jinsi ambavyo daktari alimweleza kuwa ilikuwa kiduchu tu afe wakati wa kujifungua hivi karibuni.


Mtangazaji mahiri wa Kipindi cha The Mboni Show, Mboni Masimba akihojiwa katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Akiwa wodini hapo juzikati, Mboni ambaye pamoja na timu yake walikwenda kwa ajili ya kukabidhi vifaa mbalimbali vya msaada kwa akina mama ambao wapo kwenye wodi hiyo, alisema kuwa hospitali ambayo ni ya uhakika ni Muhimbili pekee kwani ndiyo walionusuru uhai wake.

“Daktari alinieleza kuwa mimi nilikuwa ni wa kufa jamani hapa ndipo niliporejeshewa uhai wangu tena japokuwa nilijifungulia hospitali nyingine lakini huko kote walishindwa, hapa ndipo walinitibu pekee na niliweka ahadi kuwa nitarudi kwa ajili ya kutoa kwa wengine,” alisema Mboni.

Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Uzazi, Dk. Mathew Kalianga alisema kuwa ugonjwa uliompata Mboni kitaalam unaitwa Pulmonary Embolism ambapo mara nyingi watu wanaopata ugonjwa huo ni asilimia tano tu kati ya mia ndiyo wanapona hivyo Mboni ni mmoja aliyebahatika.

Pulmonary Embolism ni ugonjwa wa Kuganda kwa damu ambao husababisha mshipa mkubwa unaosafirisha damu na hewa kwenda kwenye mapafu kuziba. Hali hiyo huweza kusababisha mtu kufariki dunia ghafla. Ndiyo uliomuua mwanamuziki wa Nigeria marehemu Goldie.

Mboni aliyesindikizwa na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda alitoa msaada wa mashuka, viti vya matairi na vingine vingi vinavyohitajika wodini hapo.

SOURCE: Global Publisher

MKALI WA MOVIE ZA MAPIGANO TANZANIA


Tuesday, May 26, 2015

MKALI WA CAMERA - DAVID NGAYOMA AFARIKI DUNIA JANA USIKU

R.I.P David Ngayoma
Akiwa alikuwa  ni mmoja wa wataalamu wa Camera Operaror katika kampuni ya Sahara Media group(Star tv) Bw.David Ngayoma amefariki dunia jana katika Hosptal ya Rufaa ya Bugando baada ya kusumbuliwa na maralia na Plesha kwa muda mfupi iliyopelekea mauti yake. 
Tutamkumbuka kwa mengi aliyoweza kuyafanya hasa akiwa na kampuni ya Sahara Media pia nimeshikwa na simamnzi kubwa kwani ni mmoja ya watu wakionikaribisha vyema sahara media na tukishirikiana kwa masuala ya kijamii na kifamilia kama rafiki na kaka yangu wa hiari,amekuwa mwalimu wangu wa mabo mengi hasa camera na utengenezaji wa makala katika workshop mbalimbali zikiwemo zile za DW. sisi tulimpenda lakini mungu ampenda zaidi jina la Bwana lihimidiwe R.I.P Brother, na msiba wake unataraji kufanyika nyumbani kwa kaka yake mabibo jijini dar es salaam hivyo endelea kusoma blog hii kwa uptodates za msiba huu.
NaLonely L.Nzali

Marehemu David Ngayoma enzi za Uhai wake

Monday, May 25, 2015

FADHAGET MUSIC STUDIO KUTOA OFFER YA KUREKODI

Katika kuhakikisha kuongeza ajira kwa vijana hapa nchini fadhaget Media Ltd
ambao pia ni wamiliki wa studio za kisasa za Fadhaget Music record zilizopo
mbezi Beach Africana.
Wanakuletea offer ya kurecord Muziki kwa kiwango cha gharama za kitanzania Tsh 50,000/= tu kwa single moja.
wahi sasa uweze jipatia nafasi hii na kumubuka offer hii ni ya wiki mbili na usajiri unafanyika katika ofisi za Fadhaget Media Ltd jijini Dar es salaam maeneo ya Mbezi Beach Africana.
kwa mawasiliano waweza wasiliana nao kwa namba 0766 982982.

Sunday, May 24, 2015

UBONGO WA KAJALA WAPATA TATIZO

Imelda mtemMaskini Kajala! Ndivyo unavyoweza kusema ukisikia mkasa wa staa wa kiwango cha juu kwenye tasnia ya filamu za Kibongo, Kajala Masanja ‘Kay’, ambaye anadaiwa kwa hivi sasa hayuko sawa kiafya baada ya kupigwa chupa kichwani akiwa katika shoo ya kumchangia mke wa msanii Mabeste iliyofanyika New Maisha Club, Masaki jijini Dar.

Kajala Masanja akionekana na jeraha usoni kipindi ambacho alikua amepigwa chupa.

TUJIUNGE NA CHANZO
Chanzo makini ambacho ni mtu wa karibu wa Kajala kimeliambia Ijumaa Wikienda kwamba, tangu staa huyo akumbwe na sekeseke hilo amekuwa katika kipindi kigumu kwani amekuwa akipata maumivu makali sehemu ya kichwani huku akianguka mara kwa mara.


Kajala Masanja.


Kilidai kwamba, pia Kajala amekuwa akipata kizunguzungu kikali hivyo kujiona yupo kwenye hatari kubwa hasa ikitokea akaanguka vibaya kwani anaweza kupoteza maisha.

ASHINDWA KUENDESHA GARI
Mpashaji wetu huyo aliweka wazi kuwa tangu Kajala akumbane na mkasa huo mzito uliomsababishia kushonwa nyuzi mbili juu ya jicho, amekuwa hayuko vizuri na kuna wakati hawezi hata kuendesha gari hivyo kukwamisha shughuli zake za kila siku.

“Kiukweli Kajala hayupo vizuri kabisa, amekuwa kwenye kipindi kigumu mno tangu alipopigwa chupa klabu.

“Amekuwa akianguka mara kwa mara kutokana na kizunguzungu kikali anachopata akisimama au kutembea,” kilisema chanzo hicho.


CT-SCAN;mfano wa mashine ambayo Kajala amefanyiwa vipimo.


ATINGA HOSPITALINI
Habari zilizidi kumiminika kuwa, baada ya kuona hivyo Kajala alikwenda kwenye Hospitali ya Regency iliyopo Upanga jijini Dar kwa ajili ya kufanya vipimo.

AFANYIWA CT-SCAN
Kilisema kuwa alipofika hospitalini hapo alifanyiwa kipimo cha CT-SCAN kichwani ambapo majibu yalipotoka aliambiwa kuwa kinachomsumbua ni damu iliyoganda sehemu aliyopigwa chupa.

MAJIBU YA DAKTARI
“Daktari alimpa majibu ya kushangaza maana alimwambia kama angezembea, tatizo lingekuwa kubwa sana kwenye ubongo na lingeleta shida zaidi,” kilisema chanzo hicho.

HUYU HAPA KAJALA
Baada ya kunyetishiwa mkasa huo wa kusikitisha, Ijumaa Wikienda lilimtafuta Kajala ili kuthibitisha tatizo hilo alilokuwa nalo ambapo alikiri kuwa alikuwa akihisi kizunguzungu kikali cha mara kwa mara lakini hakuwa amegundua kama alikuwa na tatizo la kuvilia damu kichwani.

“Lakini kwa sasa namshukuru Mungu niko sawa kidogo. Ukweli nilikuwa napata shida sana kila nikiinuka, napata shida ya kizunguzungu kikali sana,” alisema Kajala.

TUJIKUMBUSHE TUKIO
Wakati Kajala akitoka Klabu ya New Maisha hivi karibuni, akiwa anashuka kwenye ngazi, ghafla alishangaa kurushiwa chupa kichwani iliyosababisha kuanguka kutoka kwenye ngazi hadi chini na kusaidiwa na wasamaria wema waliompeleka katika Hospitali ya Mwananyamala jijini Dar ambapo alishonwa jeraha alilolipata.

Katika sakata hilo, Kajala alisema kuwa mtu aliyempiga chupa ni mwanaume na tayari yupo mikononi mwa polisi japo kabla ya tukio hilo alikuwa hamjui na wala alikuwa hajawahi kumuona.

NJEMBA ASHIKISHWA ADABU!

Gabriel Ng’osha
Shika adabu yako! Njemba mmoja ambaye jina halikufahamika ameshikishwa adabu na wananchi wenye hasira kali baada ya kutembezewa kichapo ‘hevi’ alipokwapua simu ya abiria mwenzake.


Kijana huyo aliyedaiwa kuwa kibaka akiwa chini ya ulinzi.

Ishu hiyo ilijiri wikiendi iliyopita maeneo ya Mtaa wa Kongo-Kariakoo jijini Darndani ya basi la UDA ambapo kijana huyo alidaiwa kukwapua simu hiyo.


Akiwa chini ya ulinzi baada ya kukwapua simu.

Akizungumza na Ijumaa Wikienda, shuhuda wa tukio hilo alisema: “Kiukweli jamaa alipigwa sana, kama siyo polisi kunusuru uhai wake angeuawa na wananchi waliokuwa na hasira,’’ alisema shuhuda na kuongeza kuwa polisi waliokuwa doria waliondoka naye kwenda kituo cha polisi ili sheria ichukue mkondo wake.

AJALI YA BASI LA SUPER FEO YAUA 3, YAJERUHI 28 MKOANI MBEYA



WATU watatu wamekufa papo hapo huku wengine 28 wakijeruhiwa baada ya basi la Kampuni ya Super Feo walilokuwa wakisafiria kutoka jijini Mbeya kwenda Songea mkoani Ruvuma kupinduka na kutumbukia mtoni leo asubuhi.

Ajali hiyo imetokea katika Kijiji cha Shamwenga, Kata ya Inyara mkoani Mbeya.

MBUNGE WA SOMALIA, YUSUF DIRIR AUAWA KATIKA SHAMBULIO MOGADISHU




Gari alilokuwemo Yusuf Dirir.

MBUNGE wa Somalia, Yusuf Dirir ameuawa kwa kupigwa risasi katika Mji wa Mogadishu jana.
Wanausalama wameeleza kuwa Yusuf Dirir aliuawa baada ya gari lake kushambuliwa na wanamgambo wanaodhaniwa kuwa wa Kundi la Al Shabaab.

Wapiganaji wa Al Shabaab.

Wafanyakazi wengine watatu wa Wizara ya Usafirishaji nao pia waliuawa katika shambulio lingine lililotokea jana.
Takribani wabunge watano waliuawa na Kundi la Al Shabaab mwaka jana huku kundi hilo likidai kuendeleza mauaji dhidi ya wabunge.

Kundi hilo jana Jumamosi lilipambana na vikosi vya majeshi ya serikali katika Wilaya ya Awdigle na Kijiji cha Mubarak kusini mwa Mji wa Mogadishu.

Katika mapigano hayo, takribani watu 17 wameripotiwa kupoteza maisha.

KIONGOZI WA CHAMA CHA UPINZANI BURUNDI AUAWA



Baadhi wananchi wakiwa eneo alipouawa Zedi Feruzi.

KIONGOZI wa chama kidogo cha upinzani nchini Burundi ameuawa kwa kupigwa risasi katika Mji mkuu wa nchi hiyo Bujumbura.


Mwili wa Zedi Feruzi amabye alikuwa kiongozi wa Chama cha Union for Peace and Development ulipatikana nje ya nyumba yake kwenye mji wa Bujumbura.


Juzi Ijumaa watu wawili waliuawa katika maandamano hayo yaliyochukua wiki kadhaa huku watu zaidi ya 100,000 wakiwa wameihama nchi hiyo kutokana na vurugu hizo za kupinga uamuzi wa Rais Pierre Nkurunziza kuwania urais kwa muhula wa tatu.

JOHARI AJIFUNGUA KWA SIRI

Brighton Masalu
Mshtuko! Baada ya kujulikana kwa wengi kuwa hana mtoto na madai ya kutokuwa na uwezo wa kuzaa, mwigizaji wa kitambo Bongo, Blandina William Chagula ‘Johari’ ameshangaza baada ya siri kuvuja kuwa amejifungua kwa siri ambapo mtoto ana umri wa miezi 7 sasa, jambo lililozua mkanganyiko na mjadala mzito, Risasi Jumamosi linakupa ‘exclusive story’.


Mwigizaji wa kitambo Bongo, Blandina William Chagula ‘Johari’

UBUYU WAMWAGWA
Mwandishi wetu akiwa katika majukumu yake ya kila siku, ghafla alipigiwa simu na chanzo chake cha kuaminika ambacho ni mtu wa karibu wa Johari na kuanika kila kitu huku kikiomba hifadhi ya jina.


Mtoto wa Johari.

Sosi: Wewe (kikitaja jina la mwandishi) una habari?
Mwandishi: Zimejaa tele lakini hiyo yako inaweza kuwa ya muhimu zaidi.
Sosi: Tena ni muhimu kweli, unajua kuwa Johari ana mtoto na sasa anatimiza miezi saba?
Mwandishi: Unasema? Kajifungua lini na wapi?
Sosi: Kitambo tu, mbona hata kwenye ukurasa wake wa Instagram kaweka hizo picha, kwani hamjaingia huko?
Mwandishi: Ok, ok, nashukuru kwa taarifa.

Chanzo hicho kilisema kuwa, Johari alinasa mimba mwezi Machi, mwaka jana na kufanya siri kwa kutoonekana mara kwa mara na ilipofikisha muda wa kujifungua yaani mwezi Desemba alikwenda kujifungulia nyumbani kwao, Kijiji cha Ngokolo mkoani Shinyanga.

Huko alikaa kwa muda wa miezi minne na kurudi Dar kwa siri ambapo mtoto alitafutiwa mlezi maalum akishirikiana na mama mzazi wa Johari (jina linahifadhiwa).
Wakati hayo yakiendelea, ilisemekana kwamba Johari alikuwa akipigana usiku na mchana kutunza siri hiyo ikiwemo kutoruhusu watu wengi wakiwemo jamaa na marafiki kufika nyumbani kwao, Ubungo, Dar.


Mwigizaji wa kitambo Bongo, Blandina William Chagula ‘Johari’ akiwa na mwanaye.

JOHARI ASAKWA KILA KONA
Baada ya mwanahabari wetu kupata ubuyu huo, alianza harakati za kumsaka Johari kwa njia ya simu ya kiganjani lakini hakupatikana na kuamua kwenda hadi ofisini kwake, Sinza-Mori jijini Dar.
Alipokutwa ofisini kwake, RJ, Johari alibanwa juu ya madai hayo ambapo awali, alikataa kwa kutikisa kichwa huku akisindikiza na maneno ya kutaka kuheshimiwa.

“Hakuna kitu kama hicho na kama huna kingine cha kuuliza, naomba uniache nina majukumu mengi mezani kwangu,” alisema Johari huku akimtazama mwandishi wetu kwa jicho la ‘niondolee umbeya wako hapa’ licha ya mwandishi wetu kubaini mabadiliko mwilini mwake ikiwemo kunawiri kulikopitiliza.

UCHUNGUZI ZAIDI
Mwandishi wetu hakuridhika na majibu ya msanii huyo ndipo akaamua kuingia kwa undani na kina zaidi kutafuta data za kutosha ili kujua lipi ni tui na yapi ni maziwa juu ya utata wa habari hiyo.

Mwanahabari wetu alianza kwa kuwapeleleza watu wa karibu wakiwemo wafanyakazi wenzake na kubahatika kupata maelezo ya kina zaidi kutoka kwa mmoja wa rafiki mwingine wa Johari na kuyalinganisha na yale ya sosi wa kwanza na kubaini ukweli halisi.
“Huyo (Johari) asiwadanganye kabisa, ukweli ni kwamba alijifungua mwezi Desemba, mwaka jana kuelekea Krismasi na alikwenda kujifungulia kwao Shinyanga.

RISASI LAMRUDIA JOHARI
Kama mjumbe wa nyumba kumi, mwandishi wetu hakuchoka hivyo aliamua kumtafuta tena Johari huku safari hii akitumia mbinu za ndani za taaluma yake (uandishi) ambapo alimtega Johari kuwa anamhitaji kwa shida nyingine na kuomba miadi (appointment) ya kukutana naye.


Johari akiwa na mwanaye katika picha tofauti.

AINGIA, ATOKA!
Katika kupanga mahali na wakati wa kuonana, huku mwandishi wetu akiwa na ushahidi wa picha zikimuonesha Johari akiwa na mtoto wake na nyingine zikimuonesha mama yake Johari akiwa na mjukuu wake.

Hata hivyo, msanii huyo alileta upinzani mkali wa kukutana na mwandishi wetu na wakati mwingine kukubali kwa masharti mazito ikiwemo kutokuwa na kamera wala kifaa chochote cha kurekodia sauti, kitendo ambacho huitwa na vijana wa mjini kuingia na kutoka.

AWEKWA CHINI YA ULINZI
Baada ya vuta nikuvute ya muda mrefu, hatimaye walikubaliana kukutana Sinza-Mori na kuanza mazungumzo huku mwandishi akimuanzia mbali kabisa kwa kutumia saikolojia ya kiuandishi na bila kujishtukia, ghafla Johari alijikuta akiingia mwenyewe kwenye mtego na kujikuta akikiri kuwa amezaa na mtoto ana umri wa miezi saba sasa!

AWA MDOGO KAMA PIRITONI
Kwa kubanwa na maswali mazito na muhimu, Johari alijikuta akiwa mpole na mdogo mithili ya kidonge cha piritoni na kuamua kuweka wazi kila kitu licha ya kutumia mbinu za ‘mfamaji’.
“Lakini jamani, mimi si mwanamke? Sasa kama ni hivyo kuzaa ni jambo la ajabu au mlitaka niutangazie ulimwengu wote kuwa nimebeba mimba na sasa nimezaa?” alihoji Johari.

JINA LA MTOTO LAFANANA NA LA MAMA RAY!
Huku akimkazia macho usoni, ‘karani’ wetu alimuuliza Johari jina la ‘anko’ wake ambapo kwa uso uliochoka, msanii huyo alilitaja kuwa anaitwa Maria na ndipo mwandishi wetu akaibua swali jipya!

NI MTOTO WA RAY?
Mwandishi alishtuka kusikia jina la anko wake kwani hata mama mzazi wa aliyewahi kudaiwa kuwa mwandani wake ambaye ni mkurugenzi mwenzake Johari, Vincent Kigosi ‘Ray’ anaitwa Maria Kigosi.
Mwandishi: Kwani ni mtoto wa Ray?
Johari: (akikunja ndita) achana na mimi, nina kazi nyingine siko tayari kuendelea na mazungumzo.

HUKO NYUMA
Kabla ya ishu hii kuwa wazi, siku za nyuma Magazeti ya Global yaliwahi kunyetishiwa juu ya Johari kuwa mjamzito lakini alipoulizwa alikataa katakata. Hata alipofuatwa nyumbani kwao alijificha ili asionekane na wanahabari wetu. Ili kujua baba wa mtoto, usicheze mbali na Magazeti ya Global.

KIPINDI CHA MBONI SHOW CHAAZIMISHA MIAKA MITATU KWA KUTOA MSAADA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI, DAR‏ NA THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC WADHAMINI ZOEZI ZIMA


Tangazo limetengezwa na Rumafrica +255 715 851 523


Mkurugenzi wa Mboni Show, Mboni Masimba akipongezwa meneja wa Jengo la Wazazi, Sister Amina Mwakuluzo kwa moyo aliyouonyesha. Kila mwaka Kipindi cha Mboni huwa kinaadhimisha kwa kutoa msaada sehemu mbali mbali ikiwa ni mpango wake wa kurudisha fadhira kwa jamii ambapo mwaka huu aliungwa mkono na PSPF, Nakiete Pharmacy, Fadhaget Sanitarium Clinic pamoja Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda.

Mkurugenzi wa Mboni Show, Mboni Masimba akimkabidhi Mkuu wa Idara ya Uzazi na Magonjwa ya Akina mama wa hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dokta Mathew Kallaga (aliyepokea kwa niaba ya uongozi) vifaa mbali mbali vyenye thamani ya Tshs. Milioni saba alivyotoa kwa hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam ikiwa ni maadhimisho ya miaka mitatu ya kipindi hicho. Kila mwaka Kipindi cha Mboni huwa kinaadhimisha kwa kutoa msaada sehemu mbali mbali ikiwa ni mpango wake wa kurudisha fadhira kwa jamii ambapo mwaka huu aliungwa mkono na PSPF, Nakiete Pharmacy, Fadhaget Sanitarium Clinic pamoja Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda.

Mkurugenzi wa Mboni Show, Mboni Masimba akitoa shukrani zake kwa uongozi wa hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa kuweza kumpokea na kukubali vifaa alivyotoa ili viweze kuendelea kusaidia jamii. Mboni alitoa vifaa mbali mbali vyenye thamani ya Tshs. Milioni saba alivyotoa kwa hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam ikiwa ni maadhimisho ya miaka mitatu ya kipindi hicho. Kila mwaka Kipindi cha Mboni huwa kinaadhimisha kwa kutoa msaada sehemu mbali mbali ikiwa ni mpango wake wa kurudisha fadhira kwa jamii ambapo mwaka huu aliungwa mkono na PSPF, Nakiete Pharmacy, Fadhaget Sanitarium Clinic pamoja Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda.

Mkurugenzi wa Mboni Show, Mboni Masimba akimkabidhi kikombe Mkuu wa Idara ya Uzazi na Magonjwa ya Akina mama wa hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dokta Mathew Kallaga.

Mkurugenzi wa Mboni Show, Mboni Masimba akitoa zawadi mbali mbali kwa akinamama aliyowakuta katika wodi ya wazazi. Kipindi cha Mboni huwa kinaadhimisha kwa kutoa msaada sehemu mbali mbali ikiwa ni mpango wake wa kurudisha fadhira kwa jamii ambapo mwaka huu aliungwa mkono na PSPF, Nakiete Pharmacy, Fadhaget Sanitarium Clinic pamoja Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda.

Mkurugenzi wa Mboni Show, Mboni Masimba akimkabidhi nguo kwa mama aliyejifungua mtoto wa kike. Pembeni anayeshikilia nguo ni Mkurugenzi wa Fadhaget Sanitarium Clinic, Dokta Fadhili Emily.



... Mkurugenzi wa Mboni Show, Mboni Masimba akiwa amebeba mtoto kwa furaha.


Mkurugenzi wa Mboni Show, Mboni Masimba akitoa zawadi ya Nakiete Baby Diaper ambazo hutengenezwa na Kuuzwa na Nakiete Pharmacy ambao nao waliungana nae kutoa msaada huo.


Mkurugenzi wa Mboni Show, Mboni Masimba (katikati) akiongea machache mara baada ya kukabidhi vifaa vyenye thamani ya Tshs. Milioni saba alivyotoa kwa hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam ikiwa ni maadhimisho ya miaka mitatu ya kipindi hicho. Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Fadhaget Sanitarium Clinic, Dokta Fadhili Emily, Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Nakiete Pharmacy, Dorine Mzava na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda. Wengine ni Mkuu wa Idara ya Uzazi na Magonjwa ya Akina mama wa hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dokta Mathew Kallaga na Dokta Vicent Tarimo.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda akiongea wakati alipounga mkono Kipindi cha Mboni Show katika utoaji wa Misaada katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam. Pembeni kulia ni Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Nakiete Pharmacy, Dorine Mzava na Mkurugenzi wa Mboni Show, Mboni Masimba.

Mkurugenzi wa Mboni Show, Mboni Masimba akitia shukrani kwa wauguzi wa hospitali hiyo.


Picha ya Pamoja...

Mkurugenzi wa Mboni Show, Mboni Masimba akihojiwa na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza kutoa msaada katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Mboni Show, Mboni Masimba akishow ndugu zake na Emma Kahere na Mariam Masimba.


Timu ya Mboni Show ikifurahia pamoja madokta.
(Picha zote na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.)