Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Sunday, May 24, 2015

UBONGO WA KAJALA WAPATA TATIZO

Imelda mtemMaskini Kajala! Ndivyo unavyoweza kusema ukisikia mkasa wa staa wa kiwango cha juu kwenye tasnia ya filamu za Kibongo, Kajala Masanja ‘Kay’, ambaye anadaiwa kwa hivi sasa hayuko sawa kiafya baada ya kupigwa chupa kichwani akiwa katika shoo ya kumchangia mke wa msanii Mabeste iliyofanyika New Maisha Club, Masaki jijini Dar.

Kajala Masanja akionekana na jeraha usoni kipindi ambacho alikua amepigwa chupa.

TUJIUNGE NA CHANZO
Chanzo makini ambacho ni mtu wa karibu wa Kajala kimeliambia Ijumaa Wikienda kwamba, tangu staa huyo akumbwe na sekeseke hilo amekuwa katika kipindi kigumu kwani amekuwa akipata maumivu makali sehemu ya kichwani huku akianguka mara kwa mara.


Kajala Masanja.


Kilidai kwamba, pia Kajala amekuwa akipata kizunguzungu kikali hivyo kujiona yupo kwenye hatari kubwa hasa ikitokea akaanguka vibaya kwani anaweza kupoteza maisha.

ASHINDWA KUENDESHA GARI
Mpashaji wetu huyo aliweka wazi kuwa tangu Kajala akumbane na mkasa huo mzito uliomsababishia kushonwa nyuzi mbili juu ya jicho, amekuwa hayuko vizuri na kuna wakati hawezi hata kuendesha gari hivyo kukwamisha shughuli zake za kila siku.

“Kiukweli Kajala hayupo vizuri kabisa, amekuwa kwenye kipindi kigumu mno tangu alipopigwa chupa klabu.

“Amekuwa akianguka mara kwa mara kutokana na kizunguzungu kikali anachopata akisimama au kutembea,” kilisema chanzo hicho.


CT-SCAN;mfano wa mashine ambayo Kajala amefanyiwa vipimo.


ATINGA HOSPITALINI
Habari zilizidi kumiminika kuwa, baada ya kuona hivyo Kajala alikwenda kwenye Hospitali ya Regency iliyopo Upanga jijini Dar kwa ajili ya kufanya vipimo.

AFANYIWA CT-SCAN
Kilisema kuwa alipofika hospitalini hapo alifanyiwa kipimo cha CT-SCAN kichwani ambapo majibu yalipotoka aliambiwa kuwa kinachomsumbua ni damu iliyoganda sehemu aliyopigwa chupa.

MAJIBU YA DAKTARI
“Daktari alimpa majibu ya kushangaza maana alimwambia kama angezembea, tatizo lingekuwa kubwa sana kwenye ubongo na lingeleta shida zaidi,” kilisema chanzo hicho.

HUYU HAPA KAJALA
Baada ya kunyetishiwa mkasa huo wa kusikitisha, Ijumaa Wikienda lilimtafuta Kajala ili kuthibitisha tatizo hilo alilokuwa nalo ambapo alikiri kuwa alikuwa akihisi kizunguzungu kikali cha mara kwa mara lakini hakuwa amegundua kama alikuwa na tatizo la kuvilia damu kichwani.

“Lakini kwa sasa namshukuru Mungu niko sawa kidogo. Ukweli nilikuwa napata shida sana kila nikiinuka, napata shida ya kizunguzungu kikali sana,” alisema Kajala.

TUJIKUMBUSHE TUKIO
Wakati Kajala akitoka Klabu ya New Maisha hivi karibuni, akiwa anashuka kwenye ngazi, ghafla alishangaa kurushiwa chupa kichwani iliyosababisha kuanguka kutoka kwenye ngazi hadi chini na kusaidiwa na wasamaria wema waliompeleka katika Hospitali ya Mwananyamala jijini Dar ambapo alishonwa jeraha alilolipata.

Katika sakata hilo, Kajala alisema kuwa mtu aliyempiga chupa ni mwanaume na tayari yupo mikononi mwa polisi japo kabla ya tukio hilo alikuwa hamjui na wala alikuwa hajawahi kumuona.

0 comments:

Post a Comment