Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Monday, September 7, 2015

MTI WA MLONGE NA MATATIZO YA MFUMO WA UZAZI KWA WANAWAKE-2




Tuliwahi kuzungumzia kuhusu wanawake wanaokumbwa na tatizo hili la kuvimba kwa mirija ya uzazi na tukawasihi kwamba wanaweza kutumia mti wa mlonge ili kutatua tatizo hili la kuvimba kwa mirija ya uzazi, lakini kwa ufupi tu wangepata kujua ni jinsi gani wanaweza kukumbwa na tatizo kama hili:

VYANZO
Vyanzo vya tatizo la kuvimba kwa mirija ya uzazi ya mwanamke ni kama vile:
Kukumbwa na bakteria mbalimbali sehemu za siri, lakini hili kwa upande mmoja linaweza kuwakuta watu ambao si waaminifu sana kwenye uhusiano wao au kuwa na wapenzi zaidi ya mmoja.

Pia kuna magonjwa ya zinaa ambayo mara nyingi yanapokaa kwenye mwili kwa muda mrefu pasipo kupata matibabu, pia husababisha tatizo hili la kuvimba kwa mirija ya uzazi.Pia kupata fangasi kwenye shingo ya kizazi cha mwanamke na ikakaa kwa muda bila kupata matibabu basi nayo inaweza kuchangia mtu kupatwa na tatizo hili.

Hivyo basi kama unapatwa na dalili kama hizo za maumivu chini ya kitovu, uchovu wa mwili kupita kiasi, kutopata hamu ya kushiriki tendo la ndoa, maumivu ya kiuno kupita kiasi, hali ya kutokwa na uchafu katika sehemu za siri za mwanamke, endelea kuwa nasi na tutakuelezea nini mlonge unaweza kukufanyia kuondoa tatizo hili japokuwa mimea tiba ipo mingi inayosaidia kuondoa tatizo hili.

Tatizo lingine linaloweza kuondolewa na mmea huu wa mlonge kwa mwanamke ni pamoja na;
ii. Kuna tatizo hili la Pelvic Inflammatory Diseases (PID), hii mara nyingi ni ile hali ya kuvimba kwa kuta za mji wa mimba wa mwanamke lakini pia huambatana na kuvimba kwa mirija ya uzazi ya mwanamke, kama tulivyozungumza katika makala iliyopita kwamba mlonge husaidia sana magonjwa yanayofahamika kama Inflammatory na ile hali ya kuvimbavimba kwenye mwili wa mwanamke sasa tatizo hili la PID ndilo tatizo linalogusia mambo hayo yote.

DALILI ZA PELVIC INFRAMATORY DISEASES (PID)
Mtu ambaye amepima na akakutwa na tatizo hili atakuwa na dalili zifuatazo;
Atakuwa na ile hali ya kupatwa na maumivu makali sana wakati wa hedhi, na hii huweza kumpata mwanamke hata kama anakuwa ameshajifungua na maumivu makali wakati wa hedhi tunaita Dysmenorrheal.

Kama tunavyojua ipo Primary Dysmenorrheal ambayo ni maumivu makali sana wakati wa hedhi kwa mwanamke ambaye bado hajapata mtoto, lakini Secondary Dysmenorrheal ni ile hali ya kupatwa na maumivu makali sana wakati wa hedhi kwa mwanamke ambaye tayari ameshapata mtoto au watoto.

Tutaendelea wiki ijayo kwa kuwaelezea zaidi dalili za tatizo kama hili la PID na jinsi gani mmea huu wa mlonge unavyoweza kukusaidia kuondoa tatizo hili kwa wanawake.

Kwa ushauri, vipimo na tiba, dokta anapatikana kwenye vituo vyake vya Dar es Salaam, Tanga, Morogoro na Mwanza.Nawatakia afya iliyo njema!

1 comment:

  1. Mimi n inashida sijaona period yapata mwezi wa pili sasa ila tumbo linaniuma chini ya kitovu n.a. kutokwa n.a. uchafu mweupe nilifanya ultrasound nikaambiwa sina shida ni homono imbalance ila maumivuyananizidi sanyingine hadi Kiuno chauma naomba msaada nifanyeje

    ReplyDelete