Karibu Fadhaget Sanitarium Clinic

Tunapenda kukukaribisha katika Kitengo cha Sayansi ya Tiba Asilia.

Kitengo Cha Sayansi Ya Tiba Asilia

Kwa Muda mrefu tumekuwa tukisaidia wengi katika matibabu na kutengeneza dawa bora kabisa kiafya.

Je Unapenda Kufahamu Jinsi Ya Kupata Mapacha?

Tunafundisha jinsi ya kupata jinsia unayotaka, jinsi ya kupata mtoto kama umekosa mtoto kwa muda mrefu. Pia hata jinsi ya kupata watoto mapacha tunaweza kukusaidia.

Tunapatikana Katika Mikoa Zaidi ya 10 Tanzania

Tunazidi kuongeza matawi yetu nchini Tanzania na Nje ya Nchi. Kwa sasa tunapatikana katika mikoa zaidi ya 10 na tunazidi kuongeza matawi yetu. Karibu sana.

Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Wednesday, April 30, 2014

NDEGE IMENISAIDIA KUWAFIKIA WATANZANIA WENYE MAGONJWA SUGU - DR FADHILI EMILY

Tangazo limefanywa na Rumafrica +255 715 851523

Monday, April 28, 2014

JENGO JIPYA LA THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC LAFUNGULIWA RASMI

Tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa kutuwezesha kujenga jengo letu la huduma ya tiba kwa njia ya mimea na matunda hapa Mbezi Afrikana barabara ya Salasala. Jeno hili ni kwaajili tu ya uhudumia Watanzania wenye shida mbalimbali na hasa wenye magonjwa sugu ambayo yamekuwa yakiwatesa na kusababisha watu kukosa kufanya kazi kwaajili ya ujenzi wa Taifa la Tanzania.

Dr. Fadhili Emily wa The Fadhaget Sanitarium Clinic ambaye ndiye mmiliki wa kituo hiki amesema amekuwa akijisikia vibaya sana kuona Watanzania wakitaabika na magonjwa sugu bila ya kufahamu ni wapi wanaweza kujipatia tiba yenye uhakika. Watanzania hawa wamepoteza pesa zao nyingi sana katika maeneo mbalimbali wakitafuta tiba bila ya mafanikio na hii imesababishia hata kukosa chakula nyumbani kutokana na pesa nyingi kupotea kwa manunuzi ya dawa. Hiki kitendo kimemgusa sana Dr. Fadhili Emily na ndio maana akaamua kujenga kituo chake ili watu waweze kufika na kijipatia dawa zeney uhakika katika miili yao.

Tunakukaribisha sana wewe Mtanzania na hata watu wa nchi mbalimbali kufika katika kituo chetu ili kujipatia tiba.

Wasiliana nasi kwa smawasiliano yafuatayo:

P.O.Box 42029,
Mbezi Beach, Afrikana njia ya Salasala, Dar es Salaam, Tanzania
Tunapatikana kwa simu zifuatazo:

+255 712 705 158 | +255 757 931 376 | +255 787 705 158 | +255 757 505 158 | +255 774 505 158 | +255 787 505158

Barua Pepe: fadhaget@gmail.com

Blogu: www.fadhaget.blogspot.com

Pia unaweza kusikiliza Praise Power Radio 99.2FM kila siku ya Jumapili kuanzia saa 11:30 asubuhi mpaka saa 12"30 mchana

THE FADHAGET SANITARIUMCLINIC INAUNGANA NA IMANI ZA WAUMINI WA KANISA LA RABBON CENTER AFRIKA KUSINI YA KWAMBA MIMEA NA MATUNDA NI DAWA YA MAGONJWA SUGU:

The Fadhaget Sanitarium Clinic ni kituo cha Tiba kilichojikita katika kuhudumia afya za watu wenye magonjwa sugu kwa njia ya mimea na matunda na kumekuwa na mafanikio makubwa sana, watu wamepokea uponyaji wao na hii imesababishia hata kufungua matawi yetu katika mikoa 10 hapa Tanzania.

Kwa kutambua hilo, waumini wengi wamekuwa wakitumia mimea hii ambayo imeumbwa na Mungu na imekuwa msaada mkubwa katika uponyaji wao. Tuone watu wa Mungu wakifamia mimea wakiamini watapokea uponyaji wao.

Mdada akila majani ambayo huduma hiyo wanasema ni chakula kutoka mbinguni mwe!

Kuna mengi ambayo yamekuwa yakizungumzwa kuhusu huduma za watumishi mbalimbali, moja wapo ni hii huduma iitwayo Rabboni Centre ministries iliyopo Pretoria nchini Afrika ya kusini, huduma hii iliyochini ya mwanzilishi wake mwalimu ,mchungaji na nabii Daniel Lesego ilianza mwaka 2002. Ni huduma ambayo kwa watu wasioabudu hapo huitilia mashaka kutokana na mwenendo wake.

Kwasasa wapo kwenye mfungo ambao watu hufika kanisani na hatimaye wanaishia kula majani yaliyopo nje ya kanisa hilo akisema kwamba Roho Mtakatifu huongoza mtu kula chochote huku ikidaiwa kuwa manyasi hayo ni chakula kutoka mbinguni.

Inaelezwa kwamba mara baada ya maombi waumini wengi huanza kutapika jambo ambalo kanisani hapo huashiria kwamba mtu amejazwa Roho Mtakatifu.

Lakini kama haitoshi nabii Lesego hufanya maombi huku amewakanyaga watu. Huduma hii imekuwa gumzo nchini humo na nchi jirani kwa jinsi mambo yao yanavyokwenda.

Mnasemaje watumishi kuhusu jambo hili? mwe kula manyasi kweli? mma!


Hapa nabii huyo akikanyaga watu kama njia ya mafundisho yake.

Haa!! angalia jamani, sasa ng'ombe watakula nini jamani???

Mungu tufunulie macho ya rohoni kuyajua mambo haya kama ni wewe au sisi kha!

Hajamaliza bado.

Baada ya manyasi ni mwendo wa kutapika sasa









Picha ya juu na hii huyu ndio nabii Lesego Daniel mwenye maono na huduma hii.

Watu wanajaa kwenye huduma.

Mwe! kama uti wa mgongo shida hii dawa

Maombi yanaendelea.

Waumini wakikaribisha mwaka mpya.

Nabii anafundisha huku skuna yake imekanyaga mtu, sijui



Tembelea TOVUTI YAO Picha zote kwa hisani ya ukurasa wao wa Facebook.


Saturday, April 26, 2014

THE FADHAGET SANITARIUM YAFUNGUA TAWI LAKE KAHAMA

Watu wa Kahama sasa wanaweza kujipatoia huduma zetu za tiba ya matunda na mimea katika eneo lao bila ya tatizo lolote. The Fadhaget Sanitarium imekuwa ikipokea maombi mengi sana kutoka kwa watu wa kahama ambao wamekuwa wakisumbuliwa na magonjwa sugu na kusababishia kukosa hata nuda wa kwenda kufanya kazi za maendeleo. Kwahiyo The Fadhaget Sanitarium Clinic baada ya kuona hayo iliamua kutii kile ambacho wana Kahama wanakihitaji.





THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC YAFUNGUA TAWI MBEYA

Wakazi wa Mbeya na mikoa ya karibu tunapenda kuwajuza ya kwamba ofisi za The Fadhaget Sanitarium Clinic zimefungulia mkoa hapo kwa lengo zima la kutoa huduma ya tiba kwa njia ya matunda na mimea. Baada ya kupokea maombi ya walio wengi wakihitaji huduma yetu nasi tuliona hatuna budi ya kufungua ofisi zetu mkoani hapo. Watu wamekuwa wakisumbuliwa na magonjwa sugu na wengine wamekosa nauli za kufika katika makao yetu makuu Dar es Salaam, baada ya kuona hivyo tukao ni bora kufikisha huduma zetu mkoani hapa

Mbeya tunapatikana mjini karibu na Shule ya Msingi Sisimba au karibu na Mbeya Peak Hotel





Thursday, April 24, 2014

UNHWA YA KOREA KUSINI KUISAIDIA NIMR KATIKA UGUNDUZI WA DAWA KWA KUTUMIA MIMEA



Na Father Kidevu Blog, Dar es Salaam
Taasisi ya taifa ya utafiti wa magonjwa ya binadamu Tanzania (NIMR), imesaini mkataba wa ushirikiano na kampuni ya UNHWA ya Jamhuri ya Korea ambapo kampuni hiyo itaisaidia NIMR teknolojia mpya ya kufanya ugunduzi wa dawa za binadamu kwa kutumia mimea.

Makubaliano hayo yamesainiwa jijini Dar es salaam pembezoni mwa kongamano la 28 la kisayansi la NIMR, ambapo mkurugenzi mkuu wa taasisi hiyo Dk. Mwele Malecela amesema hatua hiyo ni muhimu katika shughuli za utafiti wa afya nchini na maendeleo ya taasisi kwa ujumla.

Dk. Mwele amesema teknolojia hiyo itaongeza uwezo wa kiwanda cha taasisi cha kutengeneza dawa kwa kutumia mimea kilichopo eneo la Mabibo External jijini Dar es salaam na kwamba itawezesha taasisi kujikita zaidi katika utengenezaji wa dawa za saratani mbalimbali pamoja na za kusaidia udhibiti wa virusi vya ukimwi.

Kwa upande wake afisa mtendaji mkuu wa kampuni hiyo ya NHWA bw. YOUNG WOO JIN amesema kampuni yake imefikia hatua hiyo kutokana na mchango wa NIMR katika masuala ya tafiti na ugunduzi wa dawa ambapo ameahidi kuendelea kushirikiana na taasisi hiyo katika kiteknolojia ili kuiongezea uwezo.

MASAI WAKIMBILIA THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC KWA TIBA NA KINGA


Designer:Rumafrica

Monday, April 21, 2014

UNAFAHAMU MATATIZO YA KUKOSA USINGIZI? THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC INAKUPA JIBU

Watu wengi wamekuwa wakisumbuka sana na kupata usingizi. Tatizo la kukosa usingizi ambalo hudumu kwa zaidi ya mwezi mmoja na mara nyingi huhusianishwa na magonjwa mengine makubwa, kama vile kushuka moyo. Tatizo hilo linaweza pia kuwa dalili ya ugonjwa mbaya.


Kushindwa Kupumua Unapolala
Mario alikuwa na tatizo la kusinzia kupita kiasi mchana. Alipokuwa akiendesha gari lao, ilimbidi mke wake amtazame kwa uangalifu kwa kuwa alikuwa na zoea la kusinzia kwa ghafula na hakukumbuka jambo hilo. Alikoroma kwa sauti kubwa mara kwa mara kila usiku na wakati mwingine alishtuka na kuamka, huku akipumua kwa shida.*

Mario alikuwa na dalili za tatizo la kushindwa kupumua anapolala. Mtu anaweza kushindwa kupumua kwa sekunde kumi mpaka dakika mbili au tatu. Mara nyingi mtu mwenye tatizo hilo hupinduka-pinduka akipumua kwa shida kisha hurudi kulala, na tatizo hilo hujirudia mara nyingi sana kila usiku. Kuna aina tatu za tatizo hilo.

Tatizo la kwanza
Hutukia wakati ubongo hautoi ishara inayomwezesha mtu kupumua kikawaida.

Tatizo la pili
Sehemu ya kupitisha hewa iliyo nyuma ya koo huziba kabisa hivyo mtu hushindwa kupumua.

Tatizo la tatu
Linahusisha tatizo la kwanza na la pili na huathiri watu wengi zaidi. Mtu aliye na mojawapo ya matatizo hayo ni kama mtu ambaye halali usiku kucha kila siku!

Huenda watu wenye matatizo ya kushindwa kupumua wanapolala wakawa hatarini kwa kuwa wanaweza kulala ghafula kazini au wanapoendesha gari. Huenda wakapata shinikizo la damu, moyo wao ukafura, na wakakabili hatari kubwa zaidi ya kupatwa na kiharusi au moyo wao ukaacha kufanya kazi. Dakt. William Dement wa Chuo Kikuu cha Stanford, anakadiria kwamba Wamarekani 38,000 hufa kila mwaka kwa sababu ya madhara ya moyo yanayosababishwa na tatizo la kushindwa kupumua wanapolala.

Ingawa tatizo hilo huwapata sana wanaume wanene kupita kiasi waliozidi umri wa miaka 40, linaweza pia kuwapata watu wenye umri wowote, hata watoto. Kuna matibabu mbalimbali na yote yanapaswa kutolewa na daktari wa matatizo ya usingizi. Njia bora zaidi ya kutibu tatizo la kuziba koo mtu anapolala ambayo haihusishi upasuaji ni kutumia mashine ya kuingiza hewa mapafuni. Mgonjwa huvaa kifaa kinachodhibiti hewa (kilichorekebishwa na daktari ili kifae hali zake) kwenye pua usiku ili apate hewa inayohitajiwa kuzuia tatizo hilo. Ikiwa kifaa hicho hakisuluhishi tatizo hilo, kuna upasuaji mbalimbali unaoweza kufanywa, ambao unatia ndani kutumia miale ya leza au ya redio kuzibua koo.

Kusinzia Mchana
Tatizo lingine linalohitaji kutibiwa ni kusinzia sana mchana na linasababishwa na mfumo wa neva. Kwa mfano, Buck alikuwa akisinzia daima. Alikuwa analala ghafula hata wakati wa mikutano muhimu. Alianza kushikilia funguo mkononi ili zikianguka zimwamshe. Kisha magoti yake yalianza kulegea na alianguka aliposisimuka. Halafu alipokuwa akilala au kuamka mwili wake ulikufa ganzi na alianza kuona maono kabla tu ya kulala.

Tatizo la kusinzia mchana huanza mtu anapokuwa na umri wa miaka 10 mpaka 30. Nyakati nyingine watu wenye tatizo hilo huonekana kuwa timamu lakini hawatambui wakati ukipita. Ubaya wa tatizo hilo ni kwamba mara nyingi halitambuliwi kwa miaka mingi, huku mtu anayeugua akidhaniwa kuwa mvivu, kwamba anafikiri polepole, au anaonekana kuwa mtu asiyeeleweka. Kwa sasa tatizo hilo halina tiba, lakini dalili zake zinaweza kutibiwa kwa kiasi fulani kwa dawa na kufanya mabadiliko maishani.*

Magonjwa Mengine ya Usingizi
Magonjwa mengine mawili ambayo nyakati nyingine humpata mtu wakati mmoja, huathiri miguu na mikono na kumfanya mtu akose usingizi kabisa. Ugonjwa mmoja huifanya miguu ya mtu ishtuke-shtuke anapolala na nyakati nyingine mikono hufanya hivyo pia. Fikiria mfano wa Michael. Uchunguzi ulionyesha kwamba miguu yake iliposhtuka aliamka karibu mara 350 kila usiku!

Ugonjwa mwingine hufanya miguu isitulie,* na mgonjwa huhisi akitaka sana kusogeza miguu na magoti na hivyo hawezi kulala. Ingawa nyakati nyingine hali hiyo husababishwa na kukosa kufanya mazoezi au damu inaposhindwa kuzunguka kikamili, inaonekana wakati mwingine inasababishwa na kula na kunywa vitu vyenye kafeini. Pia kunywa kileo huongeza hali hiyo nyakati nyingine.

Ugonjwa mwingine ni ule wa kusaga au kukaza meno sana wakati mtu anapolala. Ukitokea kwa ukawaida, ugonjwa huo unaweza kuharibu meno na kusababisha maumivu makali ya taya, hivyo mtu hushindwa kulala kabisa. Kuna tiba mbalimbali kama vile upasuaji wa mdomo na kutumia kifaa cha kukinga meno usiku, ikitegemea kiwango cha ugonjwa.

Mazungumzo haya mafupi kuhusu magonjwa kadhaa ya usingizi yanaonyesha kwamba ni hatari kuyapuuza. Huenda matibabu yakawa sahili au tata, lakini mara nyingi ni ya lazima. Ikiwa wewe au mpendwa wako ana ugonjwa mbaya wa kukosa usingizi au dalili zake, inafaa kupata msaada wa kitiba haraka. Hata kama tiba haitaondoa matatizo kabisa, huenda ikapunguza sana hatari zinazohusika na kufanya hali hiyo iwe rahisi kuvumilia. Kisha, wakati ujao, wakati ahadi za Biblia zitakapotimia, “hakuna mkaaji atakayesema: ‘Mimi ni mgonjwa.’” Magonjwa yote yataondolewa kabisa Mungu atakapofanya “vitu vyote kuwa vipya.”—Isaya 33:24; Ufunuo 21:3-5.

THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC TUNASEMA KUOZA KWA MENO (DENTAL CARIES) NI UGONJWA WA KUAMBUKIZWA

Miaka ya nyuma iliaminika kuwa ugonjwa wa kuoza kwa meno si wa kuambukiza; lakini tafiti nyingi zilizofanyika zimedhihirisha ni ugonjwa wa kuambukiza.
Jino lililooza linaweza kuambukiza meno yaliyogusana nalo na pia mgonjwa aliyeoza meno au mwenye wadudu wanaosababisha kuoza kwa meno anaweza kuambukiza mwenzake/wenzake.

Dr. Fadhili Emily

Wadudu wanaosababisha kuoza kwa meno ni sehemu ya wadudu wakazi kinywani (oral flora).

Wadudu hawa hujishikiza kwenye meno na kufanya utando, wana uwezo wa kuchachua vyakula hasa vyenye asili ya sukari na kutoa tindikali.

Ni tindikali hii ambayo huvuta madini kwenye meno na kuweka matobo. Utando huu wa wadudu kwenye jino moja unaweza kuwa na wadudu nusu bilioni, miongoni mwao wakiwemo jamii ya mutans streptococci ambao kimsingi ndiyo wasababishaji wakuu wa kuoza kwa meno. Wadudu wengine ni kama Lactobacillus na Actinomyces.

Jinsi wanavyoambukiza

Ndani ya jamii ya wadudu hawa ziko jamii zingine ndogondogo ambazo zinatofautiana kwa uwezo wa kuchachua vyakula na kutoa tindikali na hata uwezo wa kujishikiza kwenye meno.

Kwa mtu mwenye wadudu wasio wakali anaweza kuambukizwa na mwenzake mwenye wadudu wakali na hivyo kuingia kwenye hatari zaidi ya kuoza meno.

Tafiti zimeonesha wapenzi/wanandoa wanaweza kuambukizana kwa njia ya kubusiana.

Watoto wanaochangia ice cream/ice water mashuleni pia wanaambukizana kwa njia hii.

Tafiti pia zimeonesha wazazi wanaotafunia vyakula watoto wao kama sehemu ya kuvilainisha wanaweza kuwambukiza pia watoto wao.

Njia nyingine ni jino lililooza kuambukiza mengine yanayogusana nayo, tindikali inayozalishwa na wadudu katika jino lililooza inaweza kuathiri jino lililo jirani.

Ndiyo maana inashauriwa ukiona jino limeanza kuoza muone mtaalamu akalitibu au akaling’oe kama halitibiki ili lisiambukize mengine.

Namna ya kujikinga
1. Njia muhimu ni kutembelea cliniki za meno angalau kila baada ya miezi sita
2. Kuzuia watoto kuchangia vyakula mudomoni
3 .Kupima kuangalia kiwango na aina za bakiteria zilizi kwenye mate yake na kupata dawa ikibidi.
4. Kuhusu kubusiana sina la kusema

THE FADHAGET SANITARIUM LEO INAKUPA BAADHI YA SABABU ZA WANAWAKE KUKOSA HEDHI


Wengi wanafahamu kwamba mwanamke akipata mimba hawezi kuziona siku zake za hedhi bila kujua kuwa ziko sababu nyingine zinazoweza kusababisha jambo hilo. Kwa kawaida mwanamke huacha kupata hedhi kitaalam huitwa Menopause anapofikisha umri wa miaka 42 -55 na kuendelea.


Leo tutazieleza sababu nje ya utaratibu huo wa kimaumbile unaoweza kumfanya mwanamke asipate hedhi na moja kubwa ni tabia ya maisha yake ya kila siku, yaani vyakula anavyokula (life
style).

SIGARA
Tatizo moja kubwa ambalo huwakumba wanawake wanaovuta sigara ni kukosa hedhi au kuharakisha kutopata hedhi miaka miwili kabla ya wakati au umri wa miili yao kufanya hivyo. UNENE Wanawake wengine hukumbwa na tatizo hilo kutokana na kuongezeka uzito. Imethibitika kuwa uzito ukiwa mkubwa kwa wanawake unasababisha kuingia katika hatua za kuacha kupata hedhi kwa kuchelewa kwa mwaka mmoja zaidi ikilinganishwa na wanawake ambao hawana uzito mkubwa.Kitaalam hali hiyo inatokana na uingilianaji wa mafuta (kwa watu wanene au walio na uzito uliopitiliza) na homoni za kujamiiana yaani Sex homones.

ULEVI
Wanawake walevi wa pombe yaani wanaokunywa pombe kila siku nao wapo kwenye hatari ya kukumbwa na tatizo hili. Lakini walio katika hatari zaidi ni wale wenye umri kati ya miaka 25 na 49, hawa wanaweza kufunga hedhi kama wataendelea na tabia hiyo ya unywaji wa pombe kila siku.

KUTOKULA NYAMA
Wengine ni wanawake ambao wanafanya mazoezi mazito mara kwa mara na wenye umri kati ya miaka 39 na 49 au wasiokula nyama au vyakula vinavyotokana na nyama (vegetarian) nao wamo katika hatari ya kukosa kuona siku zao za hedhi. Wengi wa wanawake wanaopatwa na tatizo hili hukumbwa pia na tatizo la kuchelewa kuacha kupata hedhi kama inavyotakiwa wakiwa katika umri unaotakiwa na hali hiyo huwahatarisha kwani wanaweza kukumbwa na hatari ya kupata saratani ya matiti. Menopause kama tulivyoeleza hapo juu, ni hatua ya kuacha kupata hedhi ambayo hutokea wakati mwanamke akiwa na umri wa miaka 42-55 na huambatana na usitishwaji wa kutolewa kwa mayai ya uzazi, kupungua kwa kiwango cha homoni za kujamiiana, hivyo kusababisha kupungua kwa hamu ya kujamiiana kwa mwanamke. Hali hiyo husababisha tupu za mwanamke kuwa kavu, nywele kuwa nyembamba, matatizo wakati wa kulala, matiti kusinyaa na kupata hedhi bila mpangilio kabla ya kuacha kupata hedhi kabisa.

USHAURI
Mwanamke yeyote ambaye ataona dalili au kutopata hedhi yake muda muafaka ni vyema akaenda kumuona daktari ili afanyiwe uchunguzi na kama ataonekana ana tatizo la kiafya litapatiwa ufumbuzi. Wale wenye matatizo ya tumbo wamuone mtaalam.

Friday, April 18, 2014

DR. FADHILI EMILY ANAKUTAKIA PASAKA NJEMA NA ULINDE MWILI WAKO NA MAGONJWA NA PIA AJALI KIPINDI CHA PASAKA

Kazi imefanywa na Rumafrica +244 715 851523

MATATIZO YA KUPATA HAJA KUBWA AU KUCHELEWA KUPATA CHOO (CONSTIPATION)


Ni nini tatizo la kupata haja kubwa?
Ni  haja kubwa inayopatikana isiyozidi mara tatu katika wiki na ama haja kubwa inayoleta shida kutoka kwake na utokaji wake ni mithili ya mavi ya mbuzi (uyabisi) hata kama inapatikana kila siku. Hali hii inaposhamiri muathirika hupata choo si zaidi ya mara tatu katika kipindi cha  mwezi mmoja.
Ni moja miongoni mwa matatizo katika mfumo wa kusaga chakula yanayowakumba watu wengi si hapa kwetu Zanzibar tu bali dunia nzima kwa jumla. Shida ya kupata choo ni hali inayowakabili watu mbalimbali.


Dr. Fadhili Emily
Takriban ni wastan wa asilimia kumi na mbili ya watu duniani wanasadikiwa kuwa na tatizo la kuchelewa kupata haja kubwa. Katika hali ya kawaida mwanadamu hupata haja kubwa karibu kila siku au kila baada ya siku moja.
Kwa mtoto mchanga baada kuzaliwa huenda haja mara nne hadi tano kwa siku. Wale wanaonyonya maziwa ya mama (maziwa ya kifua) hupata haja mara nyingi zaidi ukilinganisha na wenzao wanaonyonya maziwa ya kopo yaani fomula (formula). Kwani baadhi yao hupata haja kila baada ya kunyonya wakati wenzao wa maziwa ya kopo hupata haja mara moja tu kwa kila baada siku mbili hadi tatu. Mtoto anaenyonya maziwa ya mama si aghlabu kupata shida ya haja kubwa. Anapotimiza umri wa miaka miwili mtoto hupata choo takriban mara moja hadi mbili kwa siku. Wakati mtoto wa umri wa miaka minne anapata haja kubwa mara moja kwa siku.
Jee hali ikoje hapa kwetu Zanzibar?
Katika kliniki zetu za upasuaji karibu asilimia kubwa ya wagonjwa wanaokuja kwa tatizo la kuumwa na tumbo wengi wao hubainika kuwa na hali isiyoridhisha katika masuala ya kupata haja kubwa. Aidha wagonjwa hao wamekuwa wakilalamika kuchelewa kupata au hupata haja kubwa kwa shida kabisa. Kwa watoto wachanga hali hii pia ipo, na kwa watu wazima kina mama husumbuliwa zaidi ukilinganisha na kina baba. Wazee nao hasa kwasababu ya umri ambapo maradhi mengi hujitokeza na pia kutoweza kujituma kama ilivyo kwa vijana, husumbuliwa na tatizo hili kwa kiasi kikubwa. Watu wengi wamekuwa wakijitibu wenyewe pasipo kujua nini hasa kinawasibu. Hali hiyo hupelekea kwa baadhi yao kupata madhara zaidi wasiyoyatarajia. Mathalan hupata vidonda vya tumbo, maumivu ya tumbo yasiokwisha, kuharisha mara kwa mara, na baadhi yao chango huziba hali inayowapelekea kufanyiwa opresheni ya dharura.
Kuchelewa kupata haja kubwa huwa ni sababu kuu ya kupata maumivu wakati wa kwenda haja. Hali inapokuwa mbaya mtu hukosa kabisa kupata choo na kujamba pia, na uchango wake mkubwa hujaa kinyesi. Kushindwa kupata haja kubwa ni dalili inayotokana na sababu nyingi. Sababu zenyewe zimejigawa namna mbili. Mosi, kuziba choo, na pili ni uchango kuwa na mwendo wa taratibu mno.
SABABU
Zipo sababu kadhaa zinazopelekea kutokea kwa tatizo la kukosa kupata haja kubwa kikawaida, miongoni mwa hizo ni kama hizi zifuatazo:
  • Inaweza ikawa yenyewe tu bila kusababishwa na hali yoyote ile kama vile madhara ya dawa
fulani, au hali ya kiafya, na huwa haiambatani na maumivu ya tumbo. Kwa lugha nyengine ni kwamba sababu hasa huwa haijulikani. Hii ndio sababu maarufu kuliko nyengine zote.
  • Inaweza kusababishwa na mpangilio mbaya wa chakula, kutokula vyakula vyenye fiber (nyuzinyuzi), kunywa maji kidogo kuliko inavyotakiwa.
  • Matumizi ya dawa mbalimbali na baadhi ya athari zake kama vile baadhi ya dawa za kutibu presha (shinikizo la damu), dawa za kupunguza maumivu, dawa za kutibu degedege, dawa za kutibu mamivu ya tumbo ikiwa pamoja na dawa za kutibu mfadhaiko, dawa za kutibu alaji (makole).
  • Mgonjwa wa maradhi ya kisukari, maradhi ya misuli.
  • Maradhi ya uvimbe katika uti wa mgongo, kansa ya utumbo mkubwa, kidonda/kuchanika njia ya haja kubwa mlangoni yaani fisha (anal fissure).
  • Kwa makusudi tu mtu hujizuwia asiende haja kwa sababu labda hakuna choo cha kuridhisha, anaogopa maumivu hasa wale wenye fisha (anal fissure), ama kwa uvivu tu.
  • Watoto nao hupata tatizo la kuzaliwa nalo. Kukosekana mishipa ya fahamu katika sehemu ya utumbo mkubwa huwa ndio sababu inayopelekea utumbo huo kutosukuma kinyesi hivyo kusababisha kuchelewa kupata haja kubwa ambapo mara nyengine hupindukia kipindi cha wiki moja hadi mbili au hata zaidi. Kwa maana hiyo tumbo huvimba na mtoto hudhoofu kiafya. Hili ni tatizo la kipekee.
VIPI TUNACHUNGUZA
Maelezo ama dalili mgonjwa anazozielezea jinsi anavyosumbuka kupata haja kubwa, pekee hutoa taswira kamili ya tatizo linalomkabili. Miongoni mwa dalili hizo ni zile pamoja na kuwa na choo kigumu, hutoka kwa shida, hufanana na mavi ya mbuzi ama sungura yaani uyabisi. Dalili nyengine ni mbweo, kuvimba tumbo, maumivu ya tumbo, kuumwa na kichwa, uchovu, kutojiskia vizuri na pia kuwa na hisia za kutomaliza haja yote. Na anapoulizwa mgonjwa juu ya mpangilio wake wa mlo mara nyingi hubainika kutokutumia vyakula vyenye nyuzinyuzi (hivi ni vyakula vya sehemu ya mimea ambayo haisagwi na mwili wetu na hivyo kusukuma utumbo, huku ikifyonza maji wakati ikitoka na kufanikisha kupata haja kubwa). Wengi wao hawali nafaka, mboga za majani, na matunda kama mlo wa kawaida. Kutokunywa maji ya kutosha, kutofanya mazoezi kikawaida au wakati mwengine husababishwa na matumizi ya baadhi ya dawa ambazo kwa kuzitumia kwa kipindi cha muda mrefu hatimae huleta athari ya kuzuwia au kuchelewa kupata choo.
Tunachunguza kwa kuliangalia na kugusa tumbo, ikibidi huangalia njia ya haja kubwa, wakati mwengine hata kwa kutumia darubini maalum tunaweza kubaini tatizo hilo. Xray ya tumbo ingawa si lazima, nayo pia huweza kutumika kubainisha uwepo wa tatizo.
KINGA
JE, VIPI TUNAWEZA KUJIKINGA?
Ni rahisi zaidi kukinga usipate hali hii kuliko kutibu. Mara au pindi ukipata nafuu jambo la msingi ni kujitahidi kuendeleza mazoezi kwa maana ya matembezi, kuogelea, au kushiriki michezo ya aina yoyote ile ilimradi tu utoke jasho. Kunywa maji kiasi cha kutosha ambacho kwa wastani mtu mzima anatakiwa kwa siku anywe lita mbili hadi mbili na nusu kulingana na hali ya hewa. Kula mboga za majani kama vile mchicha, kisambu, mtoriro, kabichi, karoti na nyenginezo; nafaka kwa mfano karanga, mahindi, ngano, fiwi, mbaazi, kunde, maharage, njugu mawe na kadhalika; pendelea kula matunda hususan ndizi mbivu, embe, chenza na machungwa (kula hadi maganda ya ndani), papai, balungi, pea(parachichi), fenesi, epul (usilimenye), shelisheli na mengine mengi tu ambayo kwa kweli katika mazingira yetu Mola ametujaalia tunayo mengi sihaba. Yote haya hutengeneza mazingira mazuri ya kupata haja kubwa kikawaida na bila shida yoyote.
Na kwa watoto ni kuwapangia muda wa kwenda kujisaidia mapema asubuhi na kipindi cha takriban dakika thelathini baada kupata mlo.
NINI HASA KAZI YA VYAKULA VYENYE NYUZINYUZI?
Vyakula vya namna hii kwa kawaida havisagwi na mwili kwahiyo hupita katika utumbo na kutoka mwilini.Iwapo tutakula nafaka na matunda na mboga za majani tutakuwa na nafasi kubwa kujikinga kupata maradhi kama vile, maradhi ya moyo, unene wa maradhi (obesity), kuepuka kupata bawasili, na hata kusaidia mwili kudhibiti kiwango cha sukari katika damu kwa kuchelewesha uyeyukaji wake mwilini. Inadhibiti na kupunguza kiwango cha mafuta  mwilini kwa kuambatana nayo. Na kubwa zaidi huwa ni kinga tosha dhidi ya kansa ya utumbo mkubwa kwani hubeba sumu za kwenye utumbo na kutoka nazo. Kwa lugha isiyo ya kitaalamu labda tunaweza kusema na kumithilisha vyakula vya nyuzinyuzi vinafanyakazi kama brashi. Vinasafisha njia yote ya mfumo wa usagaji chakula.
TIBA
  • Ni pamoja na kunywa maji ya kutosha.
  • Kula vyakula vyenye nyuzinyuzi (fiber), hivi vingi vinapatikana katika mboga za majani, nafaka na matunda.
  • Matumizi ya haluli kama ni tiba inabidi kutumiwa kwa hadhari sana, kwa vile kuzoeleka kwake kunaweza kupelekea uchango ushindwe kufanyakazi wenyewe.
  • Nayo upigaji wa bomba hutumiwa zaidi kama kisisimuzi. Hatahivyo bomba huleta manufaa ama matokeo chanya zaidi pale tu kinyesi kinapokuwa kimejikusanya karibu na mlango wa haja kubwa.
ATHARI ZA MATATIZO YA HAJA KUBWA
Kukosa kupata haja kubwa au ama kupata haja kubwa kwa shida ikiwemo kupata choo kigumu kunaweza kusababisha miongoni mwa maradhi mengine ni pamoja na kupata bawasili, kidonda ama mpasuko katika mlango wa haja kubwa (fisha), kutoka futuru (mwijiko), mrundikano wa kinyesi katika uchango. Hali hii ikiachwa kuendelea tumbo litajaa na kuvimba, litakuwa gumu  na lenye maumivu. Mgonjwa anaweza akawa na dalili za kuziba utumbo yaani kutapika na kadhalika.
HADHARI
Siku zote yapaswa  tuwe makini na tuchukuwe hadhari pale inapotokezea kutopata haja kubwa kwa ghafla na ikadumu kwa siku kadhaa. Hali hii hutokea aghlabu sana kwa wazee na ni moja ya dalili ya kuwepo kwa uvimbe katika uchango mkubwa ambao mara nyingi huwa ni kansa ya utumbo. Bilashaka huambatana na dalili nyengine kama vile kutokwa damu njia ya haja kubwa wakati wa kujisaidia, kuharisha baadhi ya wakati na kupungua uzito wa mwili au kukonda na kadhalika.
USHAURI
Hapanashaka ili kupunguza tatizo hili ambalo linawakabili watu wengi katika jamii yetu, elimu ya chakula bora na mlo ulopangika ndio jibu sahihi ama muarubaini wa kutilia mkazo. Tuanzie skuli na majumbani mwetu kuwaelimisha hasa wanetu. Ni kweli kabisa tumejaaliwa rasilimali nyingi sana  kwa maana ya matunda ya msimu yanayofika kuzagaa kama uchafu na kuharibika, nafaka hadi kuoza ovyo, mboga za majani za kila aina, lakini la ajabu ni kuona watu wetu wengi hawajui thamani ya neema hiyo na kutokuitumia kwake ndio chanzo kikubwa cha maradhi mengi yanayotukabili. Hivyo basi tuwazoweshe watoto wetu kupenda kula matunda, nafaka na mboga za majani tangu wako wadogo, kwani si tu hupelekea kupata haja kubwa kikawaida bali pia vyakula hivi vimejaa vitamini mbalimbali muhimu kwa siha ya mwanadamu.
Muone daktari wako atakuskiliza, atakuchunguza na hatimae atakupa maelezo yenye tija kwako. Tukumbuke samaki mkunje angali mbichi, udongo upate ulimaji.

DR FADHILI EMILY AKIWA KATIKA ZIARA YAKE ZANZIBAR

Jamani kuna watu wanataabika hapa duniani na magonjwa sugu. Magonjwa haya wyamesababisha hata uchumi wa nchi kushuka chini, watu wamekuwa hawafanyi kazi kutokana na kuumwa, wamekuwa watu wa kukaa nyumbani na kuwa tegemezi. Dr. Fadhili Emily alitambua hilo na kuamua kutafuta suluhu ya magonjwa haya akishirikiana na vyuo vya kimataifa katika kutafuta  dawa za mimea na matunda ambazo zitatibu magonjwa haya sugu.

Zoezi la kuzipata dawa lilifanikiwa na ikabaki sasa kutafuta njia za kuwafikia wagonjwa mikoani kwao, na hii ni kutokana na Watanzania wengi kutokuwa na kipato cha kufika Dar es Salaam kwa matibabu. Dr Fadhili Emily aliamua kufunga safari na kuelekea Zanzibar na huko aliweza kufungua ofisi nyingine ya tiba kwa njia ya mimea na matunda. Wazanzibar waliobahatika kufika mahali hapo walifurahi sana kwa kufikishiwa huduma mlangoni, Kwahiyo Wazanzibar mtapata huduma hii eneo la Zanzibar Unguja. Nikutakie siku njema.



Ofisi mpya ya The Fadhaget Sanitarium Clinic ikiwa katika ukarabati Zanzibar Unguja

JE UNAFAHAMU DALILI NA ISHARA ZA UJAUZITO? THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC INAKUPA JIBU

Doctor Fadhili Emily wa The Fadhaget Sanitarium Clinic ninependa kukusalimu kwanza na pole kwa majukumu yanayokusibu. Leo hii nilitaka ujue ya kwamba dalili za ujauzito hutofautiana kati ya mwanamke na mwanamke, ingawa kuchelewa au kukosa hedhi ni dalili moja muhimu sana

Ni muhimu kuzitambua na kuzifahamu dalili hizi kwa sababu zinaweza kusaidia kuelezea au kutofautisha matatizo mengine mbali ya ujauzito.

Dr. Fadhili Emily

Dalili na ishara za Ujauzito:


1. Kutokwa damu kidogo ukeni wakati kiumbe kikipandikizwa kwenye mfuko wa uzazi, ingawa siyo wanawake wote hupatwa na dalili hii

2. Kukosa hedhi, hii ni moja ya dalili kubwa za ujauzito
3. Maumivu ya matiti na kuvimba matiti (huweza kutokea kati ya wiki ya 1 hadi ya 2)
4. Uchovu, wanawake wengi hujihisi uchovu na hali ya kutopenda kufanya lolote.
5. Kupoteza ladha au kuhisi ladha ya chuma mdomoni
6. Kuongezeka kwa hisia ya harufu, kipindi cha ujauzito wanawake wengi huongezeka hisia ya harufu
7. Kichefuchefu na kutapika
8. Maumivu ya kichwa
9. Kizunguzungu
10. Kukojoa mara kwa mara (hasa kati ya wiki 6-8)
11. Kubadilika rangi kwa ngozi inayozunguka chuchu kuwa nyeusi
12. Kutamani baadhi ya vyakula na kuchukia vingine
13. Kupanuka kwa mfuko wa uzazi
14. Tumbo kujaa au kuvimbiwa
15. Kununa na kukasirika haraka
16. Kiungulila au kupata choo kigumu
17. Kolostramu kuanza kutoka kwenye matiti
18. Kuongezeka uzito
19. Kuweza kupapasa mtoto (palpation of the baby)
20. Kulainika na kuvimba kwa shingo ya uzazi (Hegars sign) - kuanzia wiki ya 6
21. Shingo ya uzazi kubadilika rangi kuwa ya samawati kutokana na msongamano wa damu katika mishipa ya vena. Ishara hii huitwa pia Chadwick's sign

Dalili nyingine ni pamoja na


1. Mstari wima mweusi hutokea tumboni kuanzia chini ya kitovu (linea nigra)
2. Mama kuhisi mtoto akicheza (kuanzia wiki ya 20)
3. Maumivu ya mgongo hasa mimba ikishakuwa kubwa.
4. Kipimo cha mimba kuwa chanya (positive).
5. Kusikia mapigo ya moyo ya mtoto
6. Mtoto kuonekana kwenye kipimo cha ultrasound

Thursday, April 17, 2014

TUMAINI KWA WALIOKATA TAMAA NA MAGONJWA SUGU LIKO THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC






H BABA NAYE AKIRI KUWA DAWA ZA THE FADHAGE SANITARIUM CLINIC NI BORA


PICHA ZA DR. FADHILI EMILY WA THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC KATIKA ZIARA YAKE MKOA MWANZA

Dr. Fadhili Emily ambay amefanyika zawadi kwa walio wengi na hasa waliotumia dawa zake za mimea na tiba watakubaliana nami na kusema hakika dawa zake kiboko. Hivi karubuni alifanya ziara mkoani Mwanza kwa lengo la kutoa huduma kwa walio na magonjwa sugu na magonjwa ya kawaida ambao wameshindwa kufika katika kituo chake hapa Dar es Salaama kutokana na hali ya kiuchumi. Watu wa Mwanza waliweza kuhudumiwa katika kituo kilichoko Mwanza cha The Fadhaget Sanitarium Clinic.

Dr. Fadhili Emily akiwa katika ofisi yake Mwanza

Katika ziara hii aliweza kuongea na wasanii wa Bongo Flava kama vile H Baba ambaye naye alikiri kuwa dawa The Fadhaget Sanitarium Clinic na vipimo vya tiba ya mimea na matunda ni bora na hakuna kipingamizi. Umefika wakati wa kuwatumia hawa madaktari waliopewa karama ya kutumia mimea na matunda kuokoa afya za watu.

Dr. Fadhili Emily (kushoto) akiwa na H Baba wa Bongo Flava

Baadhi ya mimea inayotumika kama tiba

Dr. Fadhili Emily akiwa amejipumzisha baada ya kazi nzito ya kuhudumia Watanzania

TUONE ZIARA YAKE KATIKA PICHA





DALILI NA SABABU ZA MIGUU/MIKONO KUFA GANZI. NI KITU GANI CHA KUFANYA


Monday, April 14, 2014

KWANINI HUSHIKI MIMBA? THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC INAKUPA SABABU ZA KUTOSHIKA MIMBA KWA MAWANAMKE

SEHEMU YA KWANZA
Mtu ambaye ana tatizo la kutoshika mimba kitaalamu tunasema Infertility na kushindwa kupata mimba kwao huitwa Conceive. Kwa kawaida kwa mujibu wa tafiti mbalimbali, wanandoa asilimia 50 wanapata mimba ikiwa watajamiiana bila kutumia kinga wakifanya tendo hilo ndani ya miezi mitatu na asilimia 75 baada ya miezi sita na asilimia 95 baada ya mwaka mmoja.
Sababu za tatizo la kutopata mimba ni nyingi sana na baadhi yake ni hizi zifuatazo. Matatizo ya mbegu za kiume (Sperm disorders). Asilimia 35 ya wanaume wana tatizo hili na lingine ni kutopevuka kwa mayai kwa wanawake yaani kitaalamu huitwa Ovalatory dysfunction, asilimia 20.
Matatizo mengine ni yale yasiyo ya kawaida ya ute wa shingo ya uzazi ambapo ni asilimia 5 tu, wengine huwa na matatizo ya homoni na wapo ambao hawapati mimba na sababu zao hazijulikani ni asilimia 10, wengine ni kutokana na kuwa na msongo wa mawazo na wasiwasi.
Tatizo lingine la kutoshika mimba husababishwa na hitilafu katika mirija ya uzazi (tubal dysfunction), hawa huwa asilimia 30. Sababu zote hizi nitaeleza moja moja kwa kirefu katika matoleo yetu yajayo lakini wote wenye tatizo hili wanashauriwa kuhudhuria kliniki za akina mama ili waonane na madaktari.
Lakini pia wanashauriwa kufuatilia siku zao za mzunguko wa hedhi na tendo la ndoa mara kwa mara hasa baada ya siku 10 kutoka siku anamaliza hedhi na aanzie siku ya kwanza ya kupata hedhi. Ushauri Wanawake wanashauriwa wawe wanapima joto la mwili asubuhi na jioni kipindi cha kushika mimba na kama litaongezeka kwa nyuzi joto 0.5 wanashauriwa kipindi hicho kufanya tendo la ndoa.
Kwa nchi za Ulaya na Marekani wana kipimo cha kuonesha siku ambayo yai litapevuka, hivyo mtu kuwa na uhakika na siku ya kupata mimba akiamua.
Kipimo hicho kinaitwa Luteinizing hormone prediction test kits. Wanawake wanaotaka kupata mimba wanashauriwa kuepuka ulevi na uvutaji wa sigara wa kupindukia. Lakini hata wale wenye mimba wanashauriwa kuepuka vitu hivyo.

SEHEMU YA PILI
Tatizo la mwanamke kutoshika mimba limegawanyika katika makundi mawili, la kwanza huitwa kitaalamu ‘primary Infertility’.
Kundi hili ni lile ambao mwanamke huwa hajawahi kushika mimba hata siku moja na kundi la pili huitwa ‘Secondary Infertility’, hili ni lile la wanawake ambao wamewahi kushika mimba wakajifungua au mimba zikaharibika.
Zipo sababu nyingi sana zinazofanya mwanamke asiweze kushika mimba kama vile kupata maambukizi katika viungo vya uzazi, hali duni ya lishe na kukumbwa na magonjwa sugu.
Wanawake wengine wanakuwa na matatizo yanayohusu upevushaji wa mayai ambayo kitaalamu huitwa ‘Ovulatory’. Tatizo hili huathiri wanawake kwa kiasi kikubwa ambapo mwanamke anapata siku zake kama kawaida lakini hapevushi mayai.

Hali hiyo husababishwa na matatizo katika mfumo wa homoni mwilini, tatizo linaweza kutokea lenyewe kutokana na mabadiliko ya mwilini.
Lakini pia tatizo hilo linaweza kujitokeza kutokana na matumizi yanayohusiana na dawa za homoni kutumika kiholela bila kupata ushauri wa daktari na ndiyo maana tunasisitiza kuwa si vema kunywa dawa bila kushauriwa na daktari.
Wanawake wengine wanaweza kushindwa kupata mimba kutokana na matumizi ya baadhi ya vyakula au vipodozi vyenye kemikali.

Ieleweke kwamba wanawake wanaotaka kupata mimba wanakuwa na dalili za upevushaji wa mayai na kubwa ni kupata ute wa uzazi.

Daktari anaweza kuona upevushaji huo kwa kutumia vifaa maalumu ambavyo siku hizi hata mwanamke akiwa nyumbani anaweza kupima mkojo siku unazohisi unaweza kupata mimba.
Matatizo mengine yanayosababisha mwanake asipate mimba ni kuwa na matatizo kwenye mirija kwani inaweza kuziba, kutanuka au kuweka usaha au maji. Maambukizi katika mirija au upasuaji wa mimba nje ya kizazi au kufunga kizazi kunaweza kumfanya mwanamke asipate mimba.
Itaendelea wiki ijayo.