Karibu Fadhaget Sanitarium Clinic

Tunapenda kukukaribisha katika Kitengo cha Sayansi ya Tiba Asilia.

Kitengo Cha Sayansi Ya Tiba Asilia

Kwa Muda mrefu tumekuwa tukisaidia wengi katika matibabu na kutengeneza dawa bora kabisa kiafya.

Je Unapenda Kufahamu Jinsi Ya Kupata Mapacha?

Tunafundisha jinsi ya kupata jinsia unayotaka, jinsi ya kupata mtoto kama umekosa mtoto kwa muda mrefu. Pia hata jinsi ya kupata watoto mapacha tunaweza kukusaidia.

Tunapatikana Katika Mikoa Zaidi ya 10 Tanzania

Tunazidi kuongeza matawi yetu nchini Tanzania na Nje ya Nchi. Kwa sasa tunapatikana katika mikoa zaidi ya 10 na tunazidi kuongeza matawi yetu. Karibu sana.

Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Wednesday, June 24, 2015

SPONSOR WA GAZETI LA RUMAFRICA GOSPO Online MAGAZINE DR. FADHILI EMILY AMZAWADIA ZARI BAISKELI


Mpenzi wa Nasibu Abdul ‘Diamond’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’.

Mwandishi wetu
DAKTARI wa Kitengo cha Sayansi na Tiba Asili kilichopo Mbezi-Afrikana, Dokta Fadhili Emily, amemnunulia baiskeli ya kubebea mtoto, mpenzi wa Nasibu Abdul ‘Diamond’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kama zawadi pindi atakapojifungua.


Mfano wa baiskeli aliyitoa Dkt. Fadhili kwa Zari.

Akizungumza na Risasi Mchanganyiko akiwa nchini Sweden alikoenda kwa ziara binafsi, Dokta Fadhili alisema kwa kutambua yeye ni mtu wa Kigoma anakotokea Diamond, ameona amnunulie shemeji yake huyo baiskeli hiyo ambayo kwa mujibu wake, ina thamani ya shilingi milioni 5 za Kitanzania.

Dkt. Fadhili Emily.

“Mimi ni mwenyeji wa Kigoma, Zari ni shemeji yangu hivyo nikiwa huku Sweden nimeona niwawakilishe vijana wote wa kule kwa kumnunulia baiskeli hii ya kisasa shemeji yetu, wanatumia wanawake wengi Ulaya kubebea watoto wao,” alisema.

Zari anatarajiwa kujifungua kati ya Agosti au Septemba, mwaka huu ambapo ujio wa mtoto huyo umekuwa ukitengeneza vichwa vya habari kila kukicha.

Saturday, June 20, 2015

TRICHOMONIASIS

TRICHOMONIASIS


Trichomoniasis, sometimes called "trich" (pronounced "trick"), is a common sexually transmitted infection (STI) that affects both females and males, but symptoms are more common in females.

Trichomoniasis is caused by the single-celled protozoan parasite, Trichomonas vaginalis. The vagina is the most common site of infection in girls and women, and the urethra (urine canal) is the most common site of infection in boys and men. The parasite is sexually transmitted through sex (penis-to-vagina or vulva-to-vulva contact) with an infected partner. Women can get the disease from infected men or women, but men usually contract it only from infected women.




How common is Trichomoniasis?

Trich is the most common, curable STI. Each year, there are about 1 million new cases of Trichomoniasis in the United States. While rich affects both women and men, it is more common in women: the highest numbers of cases are in women between ages 16 and 35.

What are the signs and symptoms of Trichomoniasis?

Only about 30 percent of people that have trich have any symptoms. Most males with trichomoniasis do not have any signs or symptoms. However, some males may have a temporary irritation inside the penis, mild discharge, or notice a slight burning after peeing (urinating) or ejaculating. Some females may have signs or symptoms which include:

  • discharge that is green, yellow or grey,
  • a bad smell,
  • itching in or around the vagina,
  • pain during sex, and
  • pain when peeing (urinating).


How do I know if I have trich?

Trich can’t be diagnosed based on symptoms alone (keep in mind that many people don’t have any symptoms). A healthcare provider must perform a test to diagnose trich. Sometimes healthcare providers will put a sample of vaginal fluid or discharge on a slide so they can see the parasite under a microscope (this is called a “wet prep”). This test is not always reliable.

A culture test is another test for trich, and can be used with males and females. Culture tests use urine, or a swab from the vagina or urethra, and make the trich parasite easier to find by “growing” it in a lab.

Recently, tests that are much more accurate have become available, including DNA tests that are reliable in males and females. These tests can be done with vaginal swabs or urine. One of these tests even allows healthcare providers to check for trichomoniasis, chlamydia, and gonorrhea using the same sample.

What is the treatment for trich?

Trichomoniasis is curable with antibiotics. An antibiotic called Metronidazole (Flagyl) is usually prescribed. If you are prescribed treatment, use all the medicine prescribed, even if your symptoms go away. Your sex partners must also be treated, or you can get trich again. Don't have sex until all partners have finished the medication.

Pregnancy and trichomoniasis

Trichomoniasis can cause babies to be born early or with low birth weight. If you think you may be pregnant be sure to tell your healthcare provider. Women in the first three months of pregnancy should not take medicine for trich because it might hurt the baby. You can take medicine after the first three months. Talk to your healthcare provider about them.

What about other complications?

Having trich can make it easier to become infected with the HIV virus or to pass the HIV virus on to a sex partner.

DO YOU KNOW . . .

your status?
If you are sexually active or have been in the past, do you know your STI status?
Learn more about testing and find a testing center near you.

MWIMBAJI WA GOSPO CHRISTINA MITAMBO AACHI HISTORIA YA MAISHA YAKE


OMBI LA KUPANDA KWA BEI ZA MAJI SAFI NA MAJI TAKA



Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Ewura, Simon Sayore, Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, Mhandisi, Mutaekulwa Mutegeki.

Wadau mbalimbli wakiwa katika mkutano huo.

 Mkutano ukiendelea.

 Mmoja wa wadau wa mkutano huo akichangia hoja.

Wadau wakisiliza hoja za mjumbe aliyekuwa akichangia hayupo pichani pamoja na viongozi wengine waalikwa.

MAMLAKA ya Udhibiti wa Maji Safi na Maji Taka (EWURA), leo imekutana na Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) pamoja na Dawasco juu ya kujadili ombi lililotolewa na Dawasa la pendekezo la kupandisha bei ya maji.

Mkutano huo uliofanyika katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam, Mgeni Rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadick huku ukihusisha wadau mbalimbali kutoka maeneo tofauti.

Akizungumza katika mkutano huo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Mhandisi, Mutoekulwa Mutegeki, alisema kuwa, Ewura ilianzishwa chini ya Sheria ya EWURA sura namba 414 ya sheria ya Tanzania iliyoanzishwa mwaka 2006 kwa madhumuni ya kuhakikisha huduma za maji, umeme, gesi na mafuta zinaimarika kwa kusimamia ubora na bei ya huduma kwa wadau wote na taifa kwa ujumla.
Mutegeki alisema kuwa mkutano huo ni sehemu ya uchunguzi unaofanywa na Ewura kupata maoni ya wadau wa huduma ya maji safi na maji taka kabla ya kutoa maamuzi kuhusu maombi yaliyowasilishwa na DAWASA ya kurekebisha bei za huduma za maji.

Mutegeki aliweza kutoa fursa kwa wadau wote walioweza kufika ukumbini hapo kutoa michango yao ya mawazo juu ya kupandisha ama kupunguza bei kutokana na huduma zinazotolewa na mashirika hayo hivyo mapendekezo hayo yatachukukuliwa kwa ajili ya kufanyiwa kazi.
Aidha kwa upande wa DAWASA, wameiomba EWURA kurekebisha bei za huduma zao kwa makundi yote ya wateja wao na kutaka marekebisho hayo kufanyika kwa kipindi cha robo ya mwisho wa mwaka wa fedha 2014/15  hadi mwaka wa fedha wa 2015/16.
Na Denis Mtima/ GPL

TIGO YATOA DOLA 150,000 KWA HOSPITALI YA CCBRT KUSAIDIA WATOTO WENYE MIGUU ILIYOPINDA



Meneja Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez  (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana wakati wa hafla fupi ya kutiliana saini mkataba wa kusisaidia Hospitali hiyo. Kutoka kulia ni Ofisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa Hospitali ya CCBRT, Erwin Telemans na Daktari Bingwa wa Mifupa wa Hospitali hiyo, Prosper Alute. 

Ofisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa Hospitali ya CCBRT, Erwin Telemans akizungumza katika hafla hiyo.

Meneja  Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez (wa pili kushoto), akibadilishana hati na Ofisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa Hospitali ya CCBRT baada ya kutiliana saini mkataba wa kusaidi matibabu ya ulemavu wa miguu Dar es Salaam jana. Kushoto ni Daktari Bingwa wa Mifupa wa Hospitali hiyo, Prosper Alute na Meneja Uwajibikaji kwa Jamii, Woinde Shisael.

Meneja wa Mawasiliano wa Tigo, John Wanyanja (kushoto), akizungumza katika hafla hiyo.

Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.

Picha mbalimbali zikionesha miguu iliyopinda.

Wanahabari wakiwa kwenye hafla hiyo.

Joyce Moshi akiwa amembeba mtoto wake Gedion ambaye anatibiwa katika Hospitali hiyo kutokana na miguu yake kupinda ambapo sasa anaendelea vizuri.
 
Na Dotto Mwaibale
HOSPITALI ya CCBRT, imepokea dola 150,000 (zaidi ya sh. mil. 320) kutoka kwa Kampuni ya Mawasiliano ya Tigo kwa ajili ya kugharamia matibabu ya watototo wanaozaliwa na ulemavu wa nyayo zilizopinda kwa miaka mitatu ijayo.
 
Akizungumza Dar es Salaam jana, Meneja Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez alisema hiyo si mara ya kwanza kwa kampuni hiyo kugharamia matibabu ya walewavu kwani miaka mitatu iliyopita pia waligharamia matibabu ya watoto wenye ulemavu wa midomo.
 
"Tuna amini watoto wenye ulemavu wa unyayo uliopinda watapatiwa matibabu mapema, hivyo tunaomba wazazi wenye watoto wao wanaozaliwa na ulemavu huo kujitokeza CCBRT kupatiwa matibabu kwani ni bure na kwa mwaka tunatoa dola 500," alisema Gutierrez.
 
Kwa upande wa Daktari wa Mifupa wa hospitali hiyo, Prosper Alute akizungumzia ugonjwa huo, alisema unasababishwa na kurithi kutoka kwa wazazi au ndugu na kunywa pombe kupindukia au kutumia dawa zenye viambata kali.
 
Alisema asilimia 50 ya watoto wanaozaliwa hupata ugonjwa huo kwa miguu yote ambapo tangu kuingia kwa mwaka huu hadi Aprili, watoto 117 wamegundulika kuwa na ugonjwa huo ambao ni sawa na wastani wa watoto 10 kwa wiki.
 
Alisema ugonjwa huo usipotibiwa kwa haraka unaweza kumsababishia mtoto kutembea kwa shida na wakati mwingine kutotembea kabisa.
 
Kwa upande wa Joyce Mosha, Mkazi wa Mwenge,  ni mmoja wa wazazi ambaye mtoto wake, Gidion ana miezi miwili alikutwa na tatizo hilo na kufanyiwa upasuaji, alisema mara baada ya kujifungua madaktari waligundua mtoto wake kuwa na tatizo hilo, hivyo waliamua aanze kupatiwa matibabu.
 
"Namshukuru Mungu alifanyiwa upasuaji mdogo na hivi sasa anaendelea vizuri, alipogunduliwa ana tatizo hilo kwanza walimfunga plasta ngumu (POP) kwa wiki tano na kisha kumfanyia upasuaji mdogo wa mfupa na kumpa viatu maalumu vya kuvaa na vingine huwa anavaa usiku tu wakati wa kulala," alitoa ushuhuda Joyce.

PETRO MWAMPASHI KUWA MOTO NDANI YA KANISA LA KKKT SALASALA-DAR


ALIYETEKA ALBINO TABORA AFUNGWA JELA MIAKA 10‏


Masanja Mwinamila (44) mara baada ya kufikishwa katika kituo cha Polisi Wilaya ya Nzega Juni 15, 2015.


Mtoto Margreth Hamisi Machiya (6) aliyenusurika kuuzwa akiwa hai na mjomba wake.
 Mtoto Margreth baada ya kufikishwa Kituo cha Polisi Wilaya ya Nzega usiku wa manane.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, ACP Juma Bwire akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na tukio hilo Juni 16, 2015.
 
Na Daniel Mbega, Nzega
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi ya Wilaya ya Nzega leo hii imemhukumu Masanja Mwinamila (44), mkazi wa Kitongoji cha Kona Nne, Kijiji cha Ugembe II, Kata ya Mwakashanhala, Tarafa ya Puge wilayani Nzega katika Mkoa wa Tabora kwenda jela miaka 10 kwa kosa la kuteka mtoto mwenye albinism, Margreth Hamisi (6).

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Saraphine Nsana, alitoa hukumu hiyo baada ya mshtakiwa kusomewa shtaka na kukiri kutenda kosa hilo.
Ilielezwa mahakamani hapo kwamba, mnamo Juni 15, 2015 majira ya saa 3:00 usiku katika Kijiji cha Ugembe II, Kata ya Mwakashanhala wilayani Nzega, mtuhumiwa alimteka binti huyo kwa lengo la kwenda ‘kumuuza’ ili ajipatie fedha (kiasi kimehifadhiwa).
Hii ni mara ya kwanza kwa kesi inayohusisha utekaji nyara, kujeruhi na mauaji dhidi ya watu wenye albinism kuchukua muda mfupi zaidi, kwani ndiyo kwanza kesi hiyo ya Jinai Namba 116/2015 imefikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza na kutolewa hukumu.
Jitihada za Polisi
Mafanikio ya kukamatwa kwa Masanja Mwinamila akiwa katika harakati za kutaka kumuuza mtoto Margreth Hamisi, ambaye ni mpwa wake, yametokana na umakini wa Jeshi la Polisi nchini ambapo maofisa wake wa Kikosi Kazi cha Taifa waliweka mtego na kufanikiwa kumnasa mtuhumiwa kabla hajamdhuru mateka wake.
Tukio hilo limefanikisha kuubomoa mtandao hatari wa mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) kwani ni takriban wiki tatu tu tangu maofisa usalama walipofanikiwa kuwanasa watu wengine sita wakiwa katika harakati za kuuza mifupa inayodhaniwa kuwa ya binadamu (albino) mjini Kahama Mei 22, 2015 ambapo tayari wamekwishafikishwa mahakamani pamoja na wengine watatu waliokamatwa baadaye.
Matukio hayo mawili makubwa yaliyotokea katika kipindi hicho yamedhihirisha namna serikali kupitia jeshi hilo na vyombo vingine vya usalama inavyoshughulikia mitandao hiyo hatari usiku na mchana ili kuhakikisha Watanzania wote wanaishi kwa amani na usalama.
Kukamatwa na hatimaye kuhukimiwa kwa Masanja Mwinamila kumedhihirisha kwamba matukio mengi ya kuuawa au kujeruhiwa kwa watu wenye albinism yanapangwa na kufanikishwa na wanandugu wenyewe kwa sababu ya mawazo potofu ya kutafuta utajiri kwa njia za mkato.
Kama alivyoeleza Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, ACP. Juma Bwire, Juni 16, 2015, Masanja alithubutu kwenda kumnyakua mtoto huyo Margret Hamisi (6) majira ya saa 3 usiku na kukimbia naye gizani akiwa na lengo la kumuuza ajipatie utajiri.
Lakini habari kutoka eneo la tukio zinaeleza kwamba, haikuwa kazi rahisi kwa wanausalama kumwokoa binti huyo akiwa hai na kumtia mbaroni mtuhumiwa, kwani walilazimika kujifanya ‘wanunuzi’ ili kuweka mtego wa kumkamata mtuhumiwa na kumwokoa mateka.
Taarifa za uchunguzi zinaeleza kwamba, mtuhumiwa huyo alianza mchakato wa kutafuta ‘soko’ la kumuuza mtoto wa dada yake mapema mwezi Juni 2015, lakini wasamaria wema wakawaarifu wanausalama kuhusu kinachotaka kutokea katika eneo hilo.
Ilibidi maofisa wawili wa usalama wapangiwe kazi ambapo mmoja alijifanya mnunuzi na mwingine mganga wa jadi anayeambatana na ‘tajiri’ huyo feki ambao walikutanishwa na mtuhumiwa huyo aliyewaeleza kwamba ‘dili la albino lipo’.
“Alisema kuna dada yake mwenye albinism ambaye ana watoto wawili – wa kiume na wa kike – ambaonao wana albinism, huyo dada ni mtoto wa baba yake mdogo ambaye alifariki mwaka jana (2014), hivyo nyumbani hakuna mtu wa kiume wa kuleta upinzani.
“Akasema kwamba biashara hiyo ingefanyika sana, kwani alipanga kuanza kumuuza mtoto wa kike, halafu angemuuza yule wa kiume na hatimaye kummalizia dada yake!” kilisema chanzo cha ndani kutoka eneo la tukio.
Kwa kawaida asilimia kubwa ya wakazi wa Kanda ya Ziwa ni wapagani na wanawaamini waganga wa jadi kuliko mtu yeyote, hiyo alipokutanishwa na watu hao wawili, mtuhumiwa Masanja Mwinamila aliamini kila alichoambiwa na ‘mganga’.
Mganga huyo feki, mbali ya kumpigia ramli na kumwogesha dawa kwenye njiapanda, alimtaka mtuhumiwa kuleta mtoto huyo akiwa hai kwa maelezo kwamba inabidi ‘afanye tambiko ili dawa zifanye kazi’, lakini lengo likiwa kumzuia mtuhumiwa asimdhuru mtoto na hivyo kupata nafasi ya kumwokoa.
Akiwa na shauku kubwa ya kupata mamilioni ya fedha, baada ya kukubali masharti ya mganga, Masanja alimuomba ‘tajiri’ atafute bunduki ili wakati yeye atakapomnyakua mtoto, wafyatue risasi hewani kuwatisha watu watakaokimbilia eneo la tukio mara yowe litakapopigwa.
Taarifa zinasema, wanausalama waliposikia kauli hiyo wakahisi mtuhumiwa angeweza kwenda hata na panga na kuwajeruhi watu atakaowakuta eneo la tukio ili amchukue mtoto, hivyo mganga huyo akatoa masharti kwamba hata kama bunduki itapatikana, lakini asingependa kuona damu inamwagika kwa yeyote huku akimwaminisha kwamba dawa atakazoogeshwa zitamfanya awe ‘kiza’ asionekane na mtu yeyote.
Takriban mara tatu zoezi hilo liliahirishwa kwa kuangalia mazingira ya kiusalama, lakini baada ya wanausalama kujipanga vyema, ndipo Juni 15, 2015 wakafanikisha mtego huo na kumkamata mtuhumiwa akiwa amembeba mtoto ambaye alinyakuliwa akiwa usingizini.
“Ilikuwa ni kazi ngumu, lakini kama siyo imani kwa mganga, ingekuwa hatari sana hata kwa wanausalama wenyewe. Jamaa alipewa masharti kwamba, mtoto huyo anayeuzwa anatakiwa afikishwe kwa mganga akiwa hai bila kujeruhiwa mahali popote; Familia itakayovamiwa pia isimwage damu; Fedha za manunuzi kabla ya kukabidhiwa mlengwa lazima zifanyiwe tambiko na masharti ya matumizi; hakutakiwa kufanya zianaa siku nne kabla ya tukio; na lazima kuogeshwa dawa wale wote watakaokwenda kwenye tukio,” kilifafanua chanzo kingine.
Bi. Joyce Mwandu Nkimbui (33), ambaye ni mama wa Margret, anasema siku tatu mfululizo kabla ya tukio, mtuhumiwa huyo ambaye ni kaka yake anayeishi jirani na hapo alikuwa akija asubuhi na jioni akijifanya kuja kusalimia na wakati mwingine hata kupikiwa chakula.
Hata hivyo, alishangaa kukuta kwamba ndiye aliyevamia nyumbani kwao usiku wa Juni 15, 2015 na kumwamuru asikimbie kabla yeye hajaingia ndani na kumkwapua mtoto.
“Walikuja usiku, sijui walikuwa wangapi, lakini wakanilazimisha ‘wewe mama tulia’, nikaogopa na kukimbilia kwenye majani, nikaanguka kwa sababu sioni vizuri usiku, nikakutana na mwenyekiti wa kitongoji, ambaye tulikwenda naye nyumbani na kukuta tayari mtoto hayupo,” Joyce alisema kwa masikitiko.
Matukio mbalimbali.
Tangu mwaka 2006 serikali imekuwa ikipambana na matukio ya kuuawa na kujeruhiwa kwa watu wenye albinism nchini, ambapo tayari watu zaidi ya 10 wamehukumiwa kunyongwa, wengine kesi zao ziko mahakamani na watuhumiwa wengine wanaendelea kusakwa kwa kuhusika na matukio hayo ya kutisha.
Wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya wenye albinism duniani jijini Arusha Juni 13, 2015, Rais Jakaya Kikwete alisisitiza kuwa kati ya watu 13 waliohukumiwa kunyongwa wawili kesi zao zipo katika hatua ya mwisho kufikishwa kwake na kuahidi zitakapofika mezani kwake atazitendea haki stahiki.
"Lakini mwaka 2014 hadi 2015 serikali tumepambana na watu wakatili dhidi ya walemavu kwa kuwakamata watu 25 kati yao sita kesi zao zipo mahakamani, huku watano upelelezi unaendelea na 11 wameachiwa huru kwa kutopatikana na hatia," alisema.
Rais Kikwete pia aliwahakikishia wenye albinism kupatiwa vifaa vya kupambana na kansa ya ngozi bure kwenye hospitali za serikali.
Mwaka 2009, Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliangua kilio bungeni kuonyesha uchungu alionao dhidi ya vitendo vya mauaji ya kikatili ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino), na machozi yake yakayeyusha hoja ya wabunge wa upinzani waliokuwa wamepania kumbana, ili ajiuzulu kwa madai kwamba, alitoa amri ya kuua wauaji ambayo ni kinyume na katiba ya nchi.

MARY MGOGO ANAKUALIKA KATIKA TAMASHA LA UZINDUZI WA DVD YAKE NDANI YA UBUNGO PLAZA-DAR


JENGO LA EKAMASUITES LODGE YA KIJITONYAMA DAR LATEKETEA KWA MOTO




Jengo la nyumba ya wageni ijulikanayo kama Ekamasuites Lodge iliyopo kijitonyama jijini Dar, linavyoteketea kwa moto.

Jengo lilivyoteketea kwa moto.

kikosi cha zimamoto kikikiwasili eneo la tukio.

Jengo moja la Nyumba ya wageni ijulikanayo kama Ekamasuites Lodge iliyopo eneo la Kijitonyama karibu na Kituo cha Polisi cha Mabatini jijini Dar es Salaam, imeteketea vibaya kwa moto muda mfupi uliopita, Kikosi cha Zima Moto kimechelewa kufika eneo la tukio na taarifa zinasema, kikosi hicho ndipo kinawasili eneo hilo tayari kuuzima moto huo.

JENNIFER MGENDI KUFANYA TAMASHA KUBWA TABATA -DAR


Friday, June 19, 2015

KUMUONA MTOTO WA ZARI, MIL.20

AMA kweli Mbongo-Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Mama Kijacho, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, sasa ni wa kimataifa zaidi ambapo wakati mwanamama huyo akijiandaa kujifungua, tayari mtoto ajaye ameandaliwa chumba maalum cha kulala na gharama za kumuona kwa atakayehitaji picha hasa za kwenye vyombo vya habari, itakuwa si chini ya Sh. milioni 20.
Mbongo-Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Mama Kijacho, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’.
CHANZO KUTOKA WCB
Kwa mujibu wa chanzo makini ambacho kipo ndani ya Wasafi Classic Baby (WBC), Diamond na Zari wameamua kutenga chumba maalum cha mtoto wao atakapozaliwa.
Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ akiwa katika pozi na lafiki yake.
MASHARTI YA KUMWAGA
Ilidaiwa kwamba, chumba hicho kitakuwa mahususi kwa mtoto tu na wala hakuna mtu mwingine atakaye ruhusiwa kuingia kumuona bila malipo zaidi ya mama, baba na familia yao ambao nao wataingia kwa sharti la kutopiga picha.
“Naona Zari anampeleka Diamond kimataifa kila kukicha maana nimeshuhudia chumba kina ‘full’ mazagazaga ya mtoto na nilipouliza nikaambiwa hicho ni chumba cha mtoto wa Zari mara tu atakapozaliwa.
“Wanasema mtoto atakuwa na chumba chake maalum na hataruhusiwa mtu mwingine kulala wala kumuona.
“Kwa watu wa media (vyombo vya habari) lazima watoe si chini ya milioni 20 kwa picha na interview (mahojiano) na Zari.
KAMA KANYE NA KIM
“Wameamua kufanya hivyo ili kuendana na wasanii wengine wa Marekani kama Kanye West na Kim Kardashian au Jay Z na Beyonce ambao wamekuwa wakifanya hivyo.
ULINZI USIPIME
“Nimeshuhudia hadi vitu vya mtoto na kitanda chake tayari vimeshaandaliwa mara tu mtoto atakapokuja atakuwa katika chumba hicho ambacho kipo ndani ya mjengo wao, Madale (Tegeta, Dar). Unaambiwa ulinzi utakuwa mkali usipime.
“Wamejipanga mtu yeyote asimuone mtoto huyo kuanzia siku anajifungua kwani wanategemea kuweka ulinzi wa hali ya juu kuanzia hospitalini hivyo hata wanahabari wakihitaji lolote juu ya mtoto huyo watatakiwa kulipa kiasi hicho cha fedha,” kilitiririka chanzo hicho.
BABA KIJACHO ANASEMAJE?
Baada ya kunyetishiwa mchongo huo, gazeti hili lilimtafuta Baba Kijacho, Diamond ili kuthibitisha ishu hiyo ambapo alisema ni kweli wameshaandaa chumba maalum kwa ajili yake, mara tu atakapozaliwa na kwamba haitaonekana sura yake kwani kutakuwa na bei maalum kwa yoyote atakayehitaji kumuona.
“Yeah! Ni kweli kuna chumba chake maalum na pia haitaonekana sura yake maana kutakuwa na bei maalum kwa magazine au televisheni itakayohitaji kuwa na ‘exclusive’ ya kuonesha sura yake kwa mara ya kwanza.
“Bei ya mtu kumuona au kwa vyombo vya habari, hiyo itategemea na ukaribu wetu na chombo husika kitakachokuwa kikihitaji kurusha habari ya mtoto wetu,” alisema Diamond anayesumbua na kibao chake kipya cha Nana.
DIAMOND PRESHA TUPU
Diamond kwa sasa yupo kwenye presha kubwa ya kuomba mashabiki wake wampigie kura kwa wingi katika Tuzo za MTV (Mama’s) baada ya kuteuliwa kuwania Vipengele vya Msanii Bora wa Kiume Afrika, Mtumbuizaji Bora wa Kiume Afrika na Nyimbo Bora ya Kushirikiana Afrika.
ZARI ATAJIFUNGUA LINI?
Kwa upande wake, Zari anatarajiwa kujifungua mtoto wa kike kuanzia Agosti, mwaka huu na kuendelea.

Tuesday, June 16, 2015

SEHEMU YA KWANZA: MATUKIO YA TAMASHA LA FLORA MBASHA LILILODHAMINIWA NA THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC ILIYOPO MBEZI BEACH

Jina la Flora Mbasha sio geni masikio mwa watu wengi duniani. Flora Mbasha amejulikana kutokana na uimbaji wake wa nyimbo za Injili nchini na nje ya Tanzania. Huduma yake hii imewagusa watu wengi sana na na kusabaisha watu kuweza kuokoka.

Rumafrica ilibahatika kuhudhuria tamasha la Flora Mbasha siku ya Jumapili 14/06/2015 katika ukumbi wa Ubungo Plaza na kuweza kujifunza mengi sana kutoka kwa mkongwe wa nyimbo za Injili Tanzania Flora Mbasha.
Kwanza, kitu nilichojifunza ni KUJIAMINI, Flora Mbasha ikiwa ni mara yake ya kwanza kufanya tamasha katika jiji la Dar es Salaam, aliweza kuthubutu kufanya tamasha lake la LIVE akiwa na bendi yake ambayo ilitambulishwa siku hiyo kwa mara ya kwanza kabisa.

Pili, ni UWEZO wa kutawala jukwaa, Flora alionekana kulimudu jukwaa kama vile ameshawahi kufanya tamasha la LIVE,

Tatu, HISIA, Flora Mbasha aliweza kuimba nyimbo zake za kuabudu kwa hisia sana mpaka ikasababisha watu wote kukaa kimia huku wengine wakitoa machozi, ilifika kipindi hata mgeni Rasmi Mh. Freeman Mbowe kubaki akishangaa jinsi Flora Mbashaalivyokuwa  akiimba kwa hisia, Flora Mbasha aliweza kutoa machozi baada ya kumaliza kuimba wimbo wake wa kuabudu, na hii inaonyesha ni jinsi gani hata yeye  mwenyewe anavyoweza kuguswa na kile anachokiimba.

Nne, KUPENDWA, nasema hivi ni kutokana na jinsi nilivyoshudia watu kutoka Mwanza, Kigoma na Morogoro waliokuja kumuona Flora Mbasha akiimba baada ya kukaa kimia sana kwa muda mrefu. Mwimbaji mmoja anayeitwa Ency Mwalukasa alishudia kuwa yeye binafsi anampenda sana Flora Mbasha, na nyimbo zake huwa zinamgusa sana na kuinua imani yake na Mungu wake.

Sasa tuone matukio haya, na tutazidi kuwaletea matukio mengine, zidi kutembelea blogu yetu hii. Picha zimepigwa na Rumafrica +255 715 851 523
KIPINDI CHA RED CARPET
 Mwimbaji wa nyimbo za Injili Glory Mainah
 Dancers wa mwimbaji wa nyimbo za Injili Neema Gasper
 MC na mwimbaji wa nyimbo za Injili Sarah Mvungi
  MC na mwimbaji wa nyimbo za Injili Sarah Mvungi
 Mwimbaji wa nyimbo za Injili Neema Gasper
  Mwimbaji wa nyimbo za Injili Neema Gasper
  Mwimbaji wa nyimbo za Injili Neema Gasper na MC Sarah Mvungi
  Mwimbaji wa nyimbo za Injili Neema Gasper na MC Saraha Mvungi
  Mwimbaji wa nyimbo za Injili Neema Gasper, mtoto wa MC Saraha Mvungi na MC Saraha Mvungi
 Neema Gasper na dancers wake
 Mdau wa Flora Mbasha

KIPINDI CHA WAIMBAJI WAALIKWA KUMTUKUZA MUNGU KWA UIMBAJI
 Furaha Isaya
  Furaha Isaya akifuatia MC Joyce Omben, Christina Mbilinyi
 Kustoho ni mwimbaji wa nyimbo za Injili Christina Matai

 Glory Mainah




Meneja wa The Fadhaget Sanitarium Clinic, Lonely

 Waimbaji wa nyimbo za Injili Jesca Sanga (kulia) na Judy Sanga watoto  Mch. Burton Sanga
 Neema Gasper
  Neema Gasper
 MC Bony Magupa



 MC na mwimbaji wa nyimbo za Injili Saraha Mvungi

 Mkurugenzi wa Grace Products LTD (kushoto) ambaye ni mfadhili wa tamasha hili
 Mtoto wa MC Saraha Mvungi akiimba
 MC Joyce Ombeni
 Christina Matai
 Lilian Kimola (kushoto) na Furaha Isaya
 Christina Mbilinyi mwimabji wa nyimbo za Injili Tanzania
 Kutoka kulia ni Glory Mainah, Neema Gasper, Saraha Mvungi na mwanae Sarah Mvungi

 Kulia ni Elizabeth Ngaiza
 Mwimbaji wa Nyimbo Za Injili Elizabeth Ngaiza


 Mwimbaji wa nyimbo za Injili Celline Theophil (kulia) akiwa na rafiki yake

 Mtangazaji wa Praise Power Redio, Mwimbaji wa nyimbo za Injili, MC na mtangazji wa Channel Ten Bony Magupa akiimba


 Ambwene Masongwe akiimba huku wadau wake wakimpongeza kwa fedha
 Dada alitesoma Risala akimtunza Ambwene Mwasongwe


 Elizabeth Ngaiza
  Elizabeth Ngaiza
  Elizabeth Ngaiza
Kutoka kulia ni Christina Mbilinyi, Christopher Mwahangilam (hajajulikana), Furaha Isanya, MC Joyce Ombeni, MC Bony Magupa
 Mwimbaji wa nyimbo za Injili Glory Mainah
 Christina Mbilinyi na Christopher Mwahangila
 Mwimbaji wa nyimbo za Injili Neema Gasper


 Enct Mwalukasa (kulia)
 Rafiki yake Flora Mbasha kutoka USA
 Kutoka kulia ni Glory Mainah, Elizabeth Ngaiza na Sarah Mvungi

 Dancers wa Mch, Maximillian Majeshi Majeshi

 Jesca Sanga (kushoto) na Judith Sanga

 Christopher Mwahangila
 Mama mzazi wa Flora Mbasha
  Christopher Mwahangila
 Mwimbaji wa nyimbo za Injili Neema Gasper akimpongeza Christopher Mwahangila
 Glory Mainah na Elizabeth Ngaiza (kulia)
MC Bony Magupa akimhoji Christopher Mwahangiala

ENDELEA KUTEMBELEA BLOGU HII KWA MATUKIO MENGINE YA FLORA MBASHA