Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Tuesday, June 2, 2015

BABA WA KAMBO WA KIM KADARSHIAN ABADILISHA JINSIA YAKE


Moja ya familia zisizoishiwa vituko na kila mara kuingia kwenye headlines ni pamoja na familia ya Kriss Jenner ambaye ni mama mzazi wa staa maarufu duniani Kim Kardashian.

Baada ya kusambaa kwa muda mrefu habari kuhusu kujibadilisha jinsia kwa baba wa kambo wa Kim Kardashian, aitwaye Bruce Jenner, sasa ni rasmi kuwa baba huyo amejibadilisha jinsia yake na sasa anajulikana kama Caitlyn Jenner.


Uamuzi huo umevuta hisia za watu wengi kwenye mitandao ya kijamii, lakini pia umeonekana kupokelewa tofauti na familia ya akina Kardashian.. mkewe wa zamani ambaye ni Kriss Jenner na familia yake wameonekana kutopendezwa na uamuzi huo japo yeye mwenyewe hana tatizo kabisa na ishu hiyo kama ambavyo wengine wanamchukulia.


Katika Ukurasa wake mpya wa Twitter alioufungua muda mfupi baada ya kujitangaza na kupata followers wengi, Bruce Jenner ameonesha kufurahishwa na hatua aliyofikia hivi sasa.

0 comments:

Post a Comment