Karibu Fadhaget Sanitarium Clinic

Tunapenda kukukaribisha katika Kitengo cha Sayansi ya Tiba Asilia.

Kitengo Cha Sayansi Ya Tiba Asilia

Kwa Muda mrefu tumekuwa tukisaidia wengi katika matibabu na kutengeneza dawa bora kabisa kiafya.

Je Unapenda Kufahamu Jinsi Ya Kupata Mapacha?

Tunafundisha jinsi ya kupata jinsia unayotaka, jinsi ya kupata mtoto kama umekosa mtoto kwa muda mrefu. Pia hata jinsi ya kupata watoto mapacha tunaweza kukusaidia.

Tunapatikana Katika Mikoa Zaidi ya 10 Tanzania

Tunazidi kuongeza matawi yetu nchini Tanzania na Nje ya Nchi. Kwa sasa tunapatikana katika mikoa zaidi ya 10 na tunazidi kuongeza matawi yetu. Karibu sana.

Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Sunday, September 27, 2015

Dr Fadhily Emily On Interview at Times FM.

View Dr Fadhily Emily's Photos on the interview at Times FM Radio, Dar es Salaam Tanzania.





Monday, September 7, 2015

MTI WA MLONGE NA MATATIZO YA MFUMO WA UZAZI KWA WANAWAKE-2




Tuliwahi kuzungumzia kuhusu wanawake wanaokumbwa na tatizo hili la kuvimba kwa mirija ya uzazi na tukawasihi kwamba wanaweza kutumia mti wa mlonge ili kutatua tatizo hili la kuvimba kwa mirija ya uzazi, lakini kwa ufupi tu wangepata kujua ni jinsi gani wanaweza kukumbwa na tatizo kama hili:

VYANZO
Vyanzo vya tatizo la kuvimba kwa mirija ya uzazi ya mwanamke ni kama vile:
Kukumbwa na bakteria mbalimbali sehemu za siri, lakini hili kwa upande mmoja linaweza kuwakuta watu ambao si waaminifu sana kwenye uhusiano wao au kuwa na wapenzi zaidi ya mmoja.

Pia kuna magonjwa ya zinaa ambayo mara nyingi yanapokaa kwenye mwili kwa muda mrefu pasipo kupata matibabu, pia husababisha tatizo hili la kuvimba kwa mirija ya uzazi.Pia kupata fangasi kwenye shingo ya kizazi cha mwanamke na ikakaa kwa muda bila kupata matibabu basi nayo inaweza kuchangia mtu kupatwa na tatizo hili.

Hivyo basi kama unapatwa na dalili kama hizo za maumivu chini ya kitovu, uchovu wa mwili kupita kiasi, kutopata hamu ya kushiriki tendo la ndoa, maumivu ya kiuno kupita kiasi, hali ya kutokwa na uchafu katika sehemu za siri za mwanamke, endelea kuwa nasi na tutakuelezea nini mlonge unaweza kukufanyia kuondoa tatizo hili japokuwa mimea tiba ipo mingi inayosaidia kuondoa tatizo hili.

Tatizo lingine linaloweza kuondolewa na mmea huu wa mlonge kwa mwanamke ni pamoja na;
ii. Kuna tatizo hili la Pelvic Inflammatory Diseases (PID), hii mara nyingi ni ile hali ya kuvimba kwa kuta za mji wa mimba wa mwanamke lakini pia huambatana na kuvimba kwa mirija ya uzazi ya mwanamke, kama tulivyozungumza katika makala iliyopita kwamba mlonge husaidia sana magonjwa yanayofahamika kama Inflammatory na ile hali ya kuvimbavimba kwenye mwili wa mwanamke sasa tatizo hili la PID ndilo tatizo linalogusia mambo hayo yote.

DALILI ZA PELVIC INFRAMATORY DISEASES (PID)
Mtu ambaye amepima na akakutwa na tatizo hili atakuwa na dalili zifuatazo;
Atakuwa na ile hali ya kupatwa na maumivu makali sana wakati wa hedhi, na hii huweza kumpata mwanamke hata kama anakuwa ameshajifungua na maumivu makali wakati wa hedhi tunaita Dysmenorrheal.

Kama tunavyojua ipo Primary Dysmenorrheal ambayo ni maumivu makali sana wakati wa hedhi kwa mwanamke ambaye bado hajapata mtoto, lakini Secondary Dysmenorrheal ni ile hali ya kupatwa na maumivu makali sana wakati wa hedhi kwa mwanamke ambaye tayari ameshapata mtoto au watoto.

Tutaendelea wiki ijayo kwa kuwaelezea zaidi dalili za tatizo kama hili la PID na jinsi gani mmea huu wa mlonge unavyoweza kukusaidia kuondoa tatizo hili kwa wanawake.

Kwa ushauri, vipimo na tiba, dokta anapatikana kwenye vituo vyake vya Dar es Salaam, Tanga, Morogoro na Mwanza.Nawatakia afya iliyo njema!

Sunday, September 6, 2015

Mambo Ya Kuzingatia Kabla Ya Kuwa Mjamzito

Ujauzito ni safari ndefu inayomchukua mwanamke miezi tisa au majuma arobaini hadi kujifungua. Ni safari yenye mikikimikiki na hatari nyingi kwa mama na mtoto. Tusichukulie suala la ujauzito kama jambo la kawaida ingawa pia ni wajibu kwa mwanamke.

Ujauzito siyo hali ya hatari au kutisha endapo mambo ya msingi yatazingatiwa kabla ya kuwa mjamzito na kipindi cha ujauzito hadi baada kujifungua. Katika kipindi cha ujauzito kuna mambo mengi ambayo ni mabadiliko humtokea mama na mtoto aliye tumboni.
Katika makala haya tutazungumzia mambo ya kuzingatia kabla ya kuamua kubeba mimba, siyo kila mwanamke anaweza kubeba mimba kwa sababu wengine huwa na matatizo katika mfumo wao wa uzazi, aidha homoni zao hazifanyi kazi vizuri na mayai hayazalishwi au hayapevuki. Huenda pia mirija ya uzazi imeziba au ana matatizo ndani ya kizazi.

NINI CHA KUFANYA?
Ni vyema upange sasa unataka kuwa mjamzito au mwezi fulani unataka kushika mimba, uwe na mpango. Hata hivyo, hakikisha umri wako upo zaidi ya miaka 20 kwa usalama zaidi wa afya yako. Mshirikishe mwenzi wako na mwambie ungependa upate ujauzito, siyo vizuri kushtukiza kwani inaweza kukupa ‘stress’ wewe mwenyewe au mwenzako endapo mmoja wenu hajajiandaa kisaikolojia.

CHEKI AFYA YAKO
Hakikisha una afya njema, huna magonjwa sugu kama kisukari, shinikizo la damu, magonjwa mengine ya moyo, kansa, HIV, kifafa, pumu, siko seli au grupu lako la damu ni RH negative.Endapo una matatizo haya hapo juu, basi haraka wasiliana na daktari wako wa masuala ya uzazi akupe ushauri kwani magonjwa mengine yatakusumbua wakati wa ujauzito, au magonjwa yenyewe yatamwathiri mtoto. Hakikisha huna magonjwa au matatizo katika viungo vya uzazi, mfano kutokwa na uchafu ukeni wenye muwasho na harufu mbaya, vipele au vidonda sehemu za siri, maumivu wakati wa tendo la ndoa, kutokwa na damu au usaha ukeni. Vile vile mfumo wako wa uzazi uwe vizuri, matatizo katika mfumo wa uzazi ni kama vile maumivu ya tumbo chini ya kitovu, kuvurugika kwa mzunguko wa hedhi, kutopevusha mayai na kukosa hamu ya tendo la ndoa.

VILEVI ACHA
Epuka unywaji wa pombe na uvutaji wa sigara, hili hata kwa mwanaume anayetaka mtoto. Mwanamke kabla ya kuwa mjamzito hakikisha unakula sana mboga za majani ili upate kiwango kizuri cha vitamin ya Folic Acid, ni vema ule sana mboga za majani au upate virutubisho vya Folic Acid. Endapo hutakuwa na kiwango kizuri cha Folic Acid, kuna hatari ya kuzaa watoto wenye matatizo.

MAZOEZI
Fanya mazoezi mepesi mara kwa mara ili kuimarisha nyonga na viungo vyako vingine na usipate matatizo wakati wa kujifungua. Pata ushauri wa daktari kipindi muafaka.

YANAYOKWAMISHA UJAUZITO
Matatizo yanayoweza kukusababishia usipate mimba ni kutofahamu siku za kupata mimba, kuziba mirija ya uzazi.Pia uwepo wa uvimbe ndani ya kizazi na kwenye vifuko vya mayai. Uvimbe wa aina hii unaweza kutibika kwa dawa na ukaisha au kwa njia ya upasuaji, inategemea na daktari wako atakavyoona na kuamua. Kwa upande wa wanaume wanaojiandaa kuwa wazazi, ni vema umjulishe mpenzi wako sasa unataka mtoto au lini unataka mtoto. Tibu magonjwa yanayoathiri mfumo wa uzazi, mfano maumivu ya korodani, maumivu ya njia ya mkojo, upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume. Kutoa manii mepesi sana kiasi kwamba baada ya tendo la ndoa manii zote zinatoka ukeni.
Ni vema ukapime mbegu zako za kiume kuona kama zina ubora wa kutosha, usiwe na maumivu yoyote ya mwili kwani yataweza kukusababishia kupunguza nguvu za kiume na kushindwa kufanya tendo la ndoa.

Friday, September 4, 2015

Faida za Tikiti Maji Kiafya.

Baadhi ya vyakula vimekuwa vikifurahisha pale vinapoliwa, tikiti maji ni miongoni mwa vyakula hivyo. Kwanza ule mchanganyiko wa rangi zake hulifanya sio tu kuvutia bali kuwa kama ua lililochanua juu ya meza ya mlaji husika. Kama vile haitoshi tunda hili limejaaliwa virutubisho kadha wa kadha vyenye faida kubwa katika afya ya mwanadamu. Licha ya 92% ya tikiti maji kuwa ni maji, bado zile 8% zilizobaki zina faida kubwa sana kiafya jambo linaloonekana kutofahamika kwa wengi. Zifuatazo ni baadhi tu ya faida chache kati ya nyingi za tunda hili la tikiti maji:


Tikiti maji ni chanzo kizuri cha vitamini.
 Katika tunda hilo kuna 
 
  • Vitamin A, inayosaidia kuboresha afya ya macho na pia kuondosha sumu mwilini; 
  • Vitamin C, inayosaidia kuboresha kinga, kuponya majeraha, kukinga uharifu wa seli, kuboresha afya meno na fizi;  na 
  • Vitamini B6, inayosaidia ubongo kufanya kazi na pia kuibadilisha protini kuwa nishati.


    Tunda la tikiti maji lina kiwango kikubwa cha  lycopene kuliko tunda lolote au mboga za majani. Ikiwa familia yako inaishi kwenye eneo lisilo na vyanzo vya madini ya potasium, unaweza kuwapa tikiti badala yake. Lina uwezo mkubwa wa kusaidia misuli na mfumo wa fahamu kwa ujumla kufanya kazi zake vizuri.

Halikadhalika tunda hili huweza kukuondoa katika hatari ya kupata shinikizo la damu. Tikiti pia lina  Amino Acid na virutubisho vingine vinavyosaidia kurahisisha mtiririko wa damu kwenye mishipa yake.

Sifa ya kipekee iliyopo katika tunda hili, ni ule uwezo wake wa kusaidia kupunguza ama kuondoa tatizo la upungufu wa nguvu za kiume. Kwa kunywa juisi yake iliyokamuliwa bila kumenywa kwa maganda yake, kutaisadia kabisa kuondoa tatizo hilo.

Kwa kawaida tunda hili huliwa  pejke yake au kwa kuchanganya na matunda mengine. Kwa mujibu wa wataalamu wa mambo ya afya ya vyakula kila kitu kwenye tikiti maji kina faida kiafya ukianzia kwenye majani tunda na hata nyama yake.

Wednesday, September 2, 2015

Fahamu Vyakula Vya Kuondoa Gesi Tumboni au Kusaidia Tumbo Kujaa.

Watu wengi wamekuwa wakihangaika sana na matumbo yao kujaa gesi na pengine kuvimba. Leo hii The Fadhaget Sanitarium Clinic imekuletea baadhi ya vyakula vya kula kuondo hili tatizo linakusumbua kwa muda mrefu. Pia kuna dawa maalumu zinapatikana katoika kituo chetu cha tiba kwa njia ya mimea na matunda. Sasa soma hivi vyakula kwa faida yako. 



KWA njia moja au nyingine, unajikuta tumbo limechafuka kwa kujaa gesi, kuuma na hata kuunguruma, unahisi unahitaji kunywa dawa ili litulie. Katika makala ya leo utajifunza njia bora ya kutuliza mchafuko wa tumbo kwa kutumia vyakula badala ya dawa za kisasa ambazo hutuliza dalili na haziondoi tatizo.

CHANZO

Kabla ya kukimbilia kwenye tiba, ni vizuri kwanza kujua chanzo cha tatizo na katika hili unahitaji kujua ni vyakula gani ukila vinasababisha matatizo ya tumbo. Aina ya vyakula inaweza kutofautiana kati ya mtu na mtu lakini kuna aina ya vyakula vinajulikana zaidi kusababisha matatizo ya tumbo.
Vyakula na vinywaji vinavyochangia tumbo kujaa na ukosefu wa choo kwa muda mrefu huwa ni soda, ulevi (hasa bia), vyakula vyenye mafuta mengi na vyenye chumvi nyingi.

Vyakula hivyo vinapoingia tumboni, huwa na tabia ya kuchelewesha usagaji wa chakula na uondoaji wa uchafu kwenye utumbo, hivyo huwa kikwazo katika mfumo mzima wa usagaji chakula kwa urahisi.
Ili kujiepusha na matizo ya tumbo ya muda mrefu na hata kuzuia uwezekano wa kuumwa na tumbo mara kwa mara, unashauriwa kula vifuatavyo, karibu kila siku ili kulifanya tumbo lako kuwa safi wakati wote:

PAPAI (PAPAYA)

Baadhi ya utafiti uliyopo, unaonesha kwamba ‘enzyme’ waliyomo kwenye papai husaidia usagaji wa chakula tumboni na hivyo kulifanya tunda hili kuitwa na mtafiti wa zama za kale Christopher Columbus kama ‘tunda la malaika’.

Watafiti wamebaini kuwa tunda hili, lenye ladha tamu na harufu nzuri, huboresha mfumo wa usagaji chakula, husafisha utumbo, huzuia magonjwa ya uvimbe tumboni na huimarisha mfumo wa kinga ya mwili.


“Vitamini na virutubisho vya papai vina faida nyingi, lakini faida kubwa ya papai ipo kwenye kirutubisho (Enzyme) aina ya ‘Papain’ ambacho hujulikana kwa uwezo mkubwa ilionao wa usagaji mzuri wa chakula tumboni,” anasema Dk. Cari Case mwandishi wa blog ya masuala ya afya.

Mwandishi huyo anaongeza kwa kusema kuwa papai limekuwa likitumika kama tiba tangu karne ya 18, lakini utafiti wa kisayansi haukugundua faida za papai hadi mwaka 1870 wanasayansi walipogundua kirutubisho cha ‘papain kilichomo kwenye papai na tangu wakati huo tafiti nyingi zimekuwa zikifanywa kuhusu faida za tunda hili na uwezo wa tiba iliyonalo.

MTINDI (YOGURT)

Hata kama wewe si mpenzi wa mtindi, jaribu kunywa na utaupenda, hasa uwezo wake wa kuondoa matatizo ya kujaa gesi tumboni pamoja na matatizo mengine. Mtindi mzuri ni ule ‘plain’ ambao haujachanganywa na ladha au vitu vingine kwa lengo la kuongeza ladha. Bakteria asilia waliyomo kwenye maziwa mtindi ndiyo hufanya usagaji wa chakula kuwa mwepesi.

Mwisho, ili kupata faida ya papai na mtindi kama ilivyoelezwa hapo juu, ni vizuri ukala mara kwa mara kama siyo kila siku, kabla au mara baada ya kula vyakula ambavyo vinaweza kukuletea shida tumboni, au ukaweka mazoea ya kula kila siku ili kuliweka tumbo lako katika hali salama.

Health Benefits Of Carrot Juice.

What makes Carrot Juice so nutritious is that it contains a large amount of beta-carotene, vitamins and potassium in it.



  • Improves Immunity And Controls Heart Diseases: Beta-carotene makes it a rich source of vitamin A. It also helps improve the immune system. The abundance of vitamin A in carrot juice can help improve your sight and the daily intake can prevent the onset of heart diseases and strokes (1). Vitamin A in addition keeps the lining of the internal organs healthy in order to prevent it from being infected by pathogenic organisms.
  • Reduces Cholesterol: Here comes an amazing benefit of carrot juice. The potassium present in carrot juice can reduce cholesterol levels (2). It is good for the liver as it reduces fat and bile in it. Potassium, along with manganese and magnesium stabilizes blood sugar level, thus helping to reduce the risk of diabetes.
  • Aids In Clotting Of Blood: Vitamin K present in carrot juice helps blood to clot.
  • Heals External Wounds And Gums: Vitamin C helps to heal wounds and keeps the gums healthy.
  • Prevents Cancer: It also acts like an anti-cancer agent. Increased intake of carotenoids in carrot juice has been said to decrease instances of bladder, prostate, colon and breast cancer  
  • Protein Building and Bone Health: Vitamin K, present in Carrot juice is essential for the protein building process in the body. It also helps in the binding of calcium that in turn leads to the faster healing of broken bones (4). Potassium present in carrot also helps to improve bone health.
  • Cleanses the Liver: Carrot juice cleanses and detoxifies the liver. Toxins in the liver are released from the system and excreted after regular consumption of carrot juice (5). The bloodstream cannot rid the body of toxins and bile through the kidneys. This has to be ejected from the skin. Carrot juice aids this process and ensures harmful bile is removed from the body. When the liver functions well, it prevents the accumulation of fat and aids in its rapid digestion, preventing weight gain and obesity.

Beauty Benefits Of Carrot Juice:

But for the women, carrot juice is not just about good health, but also about looking beautiful. Beauty benefits include:

  • Reduces Dryness And Scarring: Potassium helps reduce skin dryness and reduces scars and blemishes. It also gives life to your skin by improving the skin tone. It will also help improve hydration and thus keep your skin moisturized.
  • Prevents Acne: Since it is high in essential oils, it also helps prevent acne by detoxifying your body.
  • Source Of Vitamins Needed For Skin: This juice effectively acts as a vitamin supplement for your skin. It also contains so many healthy nutrients that it can reduce skin related problems like eczema which is caused by deficiency of vitamin A, dermatitis and rashes.
  • Controls Sun Damage: The beta-carotenoids which help in photosynthesis in plants, help reduce sunburn and also increase the skin’s resistance towards sun damage.
  • Fights Ageing: The beta-carotenoid when entering the body changes into vitamin A and reduces cell degeneration and thus slows down the aging of the body. It largely improves the amount of collagen in the skin and thus helps in maintaining elasticity and hence reducing the visible signs of aging like sagging skin and wrinkles, as collagen is what accumulates in our body and keeps it firm and healthy.
  • Hair Care: It also increases hair growth.
  • Nail Care: It also increases nail strength.

Carrot Juice For Prenatal Care:

Carrot juice is especially considered to be beneficial for prenatal care as it improves the health of the expectant mother and child.


  • Lactation: Carrot juice intake during pregnancy improves the quality of their breast milk, as it will be enriched in vitamin A. Since vitamin A helps in cell growth it is especially beneficial in fetal growth.
  • Prevents Infections In Unborn Child: When taken during the last 3 months of pregnancy, it reduces the chance of dangerous infections in the child.
  • Calcium Supply: It also acts as a very rich source of calcium.

Carrot Juice and Weight loss:

Definitely an eye catching topic among the uses for carrot juice! Carrot juice is extremely filling, and because of low calorie count, it is the best natural health drink for a person who is trying to lose weight. It contains a large amount of natural sugar, so you don’t have to add additional sugar to it. Juicing together carrot, apple, celery and cucumber is a very healthy recipe for a good weight loss drink.


  • Muscle Growth: Vitamin A helps our body to heal after a strenuous workout and aid in muscle growth. Phosphorous in carrot juice builds, repairs, and maintains muscle;
  • Increases Metabolism: Carrot Juice also contains a large amount of Vitamin B complexes which help in breaking down glucose, fat and protein. So it helps in building muscle, increasing our metabolism and thus helping in weight loss. Vitamin B complexes also help to reduce stress and depression, which usually holds back weight loss. Phosphorous in Carrot juice boosts the body’s metabolic rate; ensures optimal use of energy in the body and decreases pain after a workout.
  • Increases Oxygen Carrying Capacity: The amount of Iron in carrot juice can increase the oxygen carrying capacity of the body, thus helping us do more workouts to lose weight
  • Energy Consumption: Phosphorous helps the body to use up more energy while doing work.
  • Controls Sugar Levels: Magnesium and Manganese present in Carrot Juice can stabilize sugar levels and help to reduce weight due to diabetes.
  • Aids Digestion: Since carrot contains a large amount of fiber, it can help in digestion and makes you feel fuller for longer.
  • Cleanses the Body: Carrot juice cleanses the body and rids it of any toxins, aiding weight loss. Fresh raw carrot juice cleanses the digestive tract of toxins, waste, indigestible material, which in turn cures and prevents obesity.

How to Consume it Right?

It should be mentioned that although carrot is such a healthy vegetable, eating carrot as Halwa with loads of ghee, sugar, cashew and raisins cannot be considered healthy. No matter how healthy you say it is, it will never be as good as carrot juice with no added sugar and milk. Yes, No carrot milk either. But it’s just as yummy without the milk too. Many people love the natural taste of carrot juice, but you can also add other fresh juices, such as orange, lemon, ginger or mint to give it a different flavor. Juice of carrot and cinnamon together forms a very healthy antioxidant rich drink which can reduce cancer, high blood pressure and diabetes. It is said that drinking fresh carrot juice is better than eating it raw because the nutrient content will be even more concentrated in the juice. 

 Ensure you drink at least one tall glass of carrot juice each day to burn fat and get the fab, svelte body you have always yearned for! Get that glowing and beautiful skin you love! Do you drink juice as part of your weight loss regime? Is carrot juice a part of your diet? Do share with us in the comments section.