Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Thursday, October 23, 2014

TAMBUA SABABU ZA KUHARIBIKA KWA MIMBA (MISCARRIAGE)


Wiki iliyopita tuliongelea sana tatizo la kuharibika kwa mimba na tukagusia baadhi ya dalili ambazo zinaweza kumpata mwanamke anayeweza kukutwa na tatizo hili la kuharibika kwa mimba. Na dalili hizo ni kama;

DALILI ZA KUHARIBIKA KWA MIMBA (Miscarriage)

  • Dalili kubwa kabisa ya kwanza ni damu nyepesi kutoka kwa mwanamke mwenye mimba.
  • Dalili kubwa ya pili ni mwanamke kutokwa na damu yenye mabonge mabonge na inakuwa nzito.
  • Dalili nyingine kubwa ni uchovu na maumivu makali ya kiuno na mgongo {miscarriage}. Wiki iliyopita tuliishia hapo, na sasa wiki hii;

Maumivu makali ya tumbo, wakati mwanamke anapokuwa ni mjamzito lakini wakati huo huo anapatwa na maumivu makali ya tumbo ya mara kwa mara yakiambatana na maumivu ya kiuno pamoja na kutokwa na damu nyepesi au nzito basi ujue ujauzito wako uko kwenye hatari ya kutoka, ni vizuri ukawasiliana na kituo cha karibu cha afya au ukawasiliana nasi kwa matibabu zaidi.


VYANZO VYA KUHARIBIKA KWA MIMBA {Miscarriage}

Vyanzo vikubwa vya kuharibika kwa mimba ni kama vifuatavyo;
Chromosome abnormalities, mimba nyingi ambazo huharibika hadi wiki ya ishirini husababishwa na tatizo hili la chromosomes, na chromosomes huwa zinabeba genes ambazo huyatambulisha maumbile ya mwanadamu kwa nje, yaani jinsia yake, ngozi yake itakuaje, macho yake na vitu vingine vingi nisingependa tuingie ndani sana lakini matatizo haya ya chromosomes huchangia sana kuharibika kwa mimba.

Maambukizi katika mji wa uzazi wa mwanamke {Infections}, kuna kitu kinaitwa Pelvic Inflammatory Diseases {PID} yaani kuvimba kwa kuta za mji wa mimba au kuvimba kwa mirija ya uzazi nayo pia huchangia sana kuharibika kwa mimba kwa mwanamke, lakini pia Candida au fangasi nazo pia huchangia sana kuharibika kwa mimba.

Chanzo kingine kikubwa ni utoaji wa mimba za mara kwa mara, wanawakie au wasichana wenye tabia ya kutoa mimba moja au mbili au tatu basi nao pia hukutwa na tatizo hili la kuharibika kwa mimba kwani uingizaji wa vyuma ndani huweza kuharibu shingo ya kizazi ya mwanamke na pia kukumbwa na tatizo hili la miscarriage au kuharibika kwa mimba.

Chanzo kingine kikubwa ni magonjwa ya zinaa {sexually transmitted diseases}, magonjwa kama gonorrhea, kaswende mara nyingi sana huathili mfumo wa uzazi wa mwanamke na hasa hasa kwenye mji wa mimba na kuufanya kuwa legevu na hata ujauzito unapotunga basi huweza kutoka kwa haraka zaidi na hivyo kusababisha tatizo hili la kutoka kwa mimba {Miscarriage}.

Chanzo kingine cha mimba kuharibika ni tatizo la kisukari kwa mwanamke, hii nayo huchangia kwa kiasi kikubwa sana kuharibika kwa mimba na mtu ambaye hafanyi uangalizi wa karibu wa tatizo la sukari basi husababisha glucose isitumike kama energy na hivyo kuleta madhara katika kizazi hasa ujauzito.

Kitu kingine ni hormones {homoni} kuvurugika, kwa mfano hormone ya progesterone mara nyingi hufanya ile kazi ya kutunza mimba iendelee kukuwa, na kama kunatokea unbalance au kuvurugika kwa homoni hii basi mara nyingi tatizo hili la mimba kuharibika hutokea. Kama unakumbwa na moja ya mambo kama haya na usingependa kupatwa na tatizo hili la kutokwa kwa mimba basi ni vema kama utaawasiliana nasi kwa ushauri na tiba zaidi.Kwa ushauri vipimo na tiba dokta anapatikana kwenye vituo vyake vya Dar es Salaam, Tanga, Morogoro na Mwanza.Nawatakia afya iliyo njema kabisa.
Itaendelea wiki ijayo.

0 comments:

Post a Comment