Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Wednesday, October 29, 2014

UVIMBE KWENYE MJI WA MIMBA (FIBROID)-3

Uvimbe huweza pia kukandamiza viungo jirani na uzazi (pressure effets) ambapo mirija ya mkojo na kibofu cha mkojo na utumbo mkubwa wa haja kubwa na uvimbe unaweza kusababisha usipate choo(consipation) wakati mwingine huweza kusababisha mkojo usitoke (urinal retention), dalili zingine ni kama kupata maumivu wakati wa tendo la ndoa (dyspararemia), uchafu sehemu za siri na kushindwa kubeba mimba (infertity) asilimia kati ya 27- 40 ya wenye uvimbe hupata tatizo la kutokushika mimba.

Dalili zingine ni kutokwa au kuharibika mimba (spontaneous abortion), hii hutoka kwa wagonjwa kati ya asilimia 40 kabla ya kutoa uvimbe na asilimia 20 baada ya upasuaji wa kutoa uvimbe.

Vipimo
Vipimo muhimu kujua au kutambua uvimbe kwenye kizazi ni kama vile mgonjwa anapohudhuria hospitali anavyopimwa tumboni (bimanual pelvic examination).Vipimo vya mahabara ni kama kujua wingi wa damu ili kujua kama mgonjwa amepungua damu (andemia) na aina ya pili ni upimaji kugundua kama mtu husika ana upungufu wa madini ya chuma (iron defficienty).

Vipimo vya damu kujua kama mgonjwa amepata maambukizi kwenye uvimbe, tunapima ESR kuona kama imepanda.Vipimo vingine Ultasound husaidia kugundua aina ya uvimbe na kutofautisha kama mgonjwa ana ujauzito au ni uvimbe pekee.

Vipimo vingine ni kama dawa kupitishwa kwenye mirija na baada ya hapo kupigwa x-ray pia husaidia kugundua kama uvimbe uko ndani.Vipimo vingine ni kama MRI hivyo ni vya uhakika zaidi na ni uhakika kwani hujua ukubwa wa uvimbe na madhara yake, vipimo vingine kama IVP husaidia kuona kama uvimbe umeenea kwenye mfumo wa mkojo hasa kibofu cha mkojo.

Kipimo kingine ni HYSTROSCOPY hiki husaidia kugundua na kuondoa uvimbe kama aina ya subrmucous myoma.Magonjwa yanayofanana na uvimbe kwenye kizazi (differential diagnosi) mara nyingi ni muhimu na husaidia kutofautisha na ujauzito pia kutofautisha uvimbe mwingine kwenye maeneo ya mfumo wa kizazi, pia kutofautisha na saratani ya mfuko wa mayai (avarian cancer).

Itaendelea wiki ijayo.

0 comments:

Post a Comment