Karibu Fadhaget Sanitarium Clinic

Tunapenda kukukaribisha katika Kitengo cha Sayansi ya Tiba Asilia.

Kitengo Cha Sayansi Ya Tiba Asilia

Kwa Muda mrefu tumekuwa tukisaidia wengi katika matibabu na kutengeneza dawa bora kabisa kiafya.

Je Unapenda Kufahamu Jinsi Ya Kupata Mapacha?

Tunafundisha jinsi ya kupata jinsia unayotaka, jinsi ya kupata mtoto kama umekosa mtoto kwa muda mrefu. Pia hata jinsi ya kupata watoto mapacha tunaweza kukusaidia.

Tunapatikana Katika Mikoa Zaidi ya 10 Tanzania

Tunazidi kuongeza matawi yetu nchini Tanzania na Nje ya Nchi. Kwa sasa tunapatikana katika mikoa zaidi ya 10 na tunazidi kuongeza matawi yetu. Karibu sana.

Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Wednesday, December 17, 2014

TAMBUA VIMBE MBALIMBALI KWA MWANAMKE NA JINSI YA KUZIONDOA PASIPO UPASUAJI



Leo tutazungumzia vimbe mbalimbali ambazo hutokea katika mwili wa mwanamke kwani wengi hawajui kama kizazi cha mwanamke kinaweza kutokewa na vimbe tofautitofauti katika maeneo tofauti kwa sababu vimbe zina vyanzo mbalimbali.

Jambo la msingi la kuzingatia leo ni kwamba aina zote hizi za vimbe tuna uwezo wa kuziondoa pasipo kufanya upasuaji.

AINA ZA VIMBE
Zipo aina tofautitofauti za vimbe katika mwili wa mwanamke, nazo ni kama;

VIMBE KATIKA MJI WA MIMBA {Uterus}
Vimbe hizi wataalamu wanaziita FIBROIDS au MAYOMA, na uvimbe huu hupatikana katika mji wa mimba iwe kwa juu au upande wa kushoto au upande wa kulia wa mji wa mimba. Na wanawake wengi sana wanakutwa na uvimbe kama huu.

VIMBE KATIKA VIFUKO VYA MAYAI YA UZAZI {Ovaries}
Katika vifuko vya mayai kunakua na vimbe za aina mbili, nazo ni kama;
Ovarian Cysts hii ni ile hali ya mwanamke kutokewa na uvimbe mmoja kwenye kifuko cha mayai ya uzazi, na kinaweza tokea upande mmoja au pande zote mbili za vifuko vya mayai, lakini vimbe hiyo inakua ni moja.

Polycystic ovarian syndromes {PCOS} au Multiple cysts na hizi ni zile vimbe ndogondogo nyingi zinazoweza kutokea kwenye kifuko cha mayai cha mwanamke, lakini nazo pia huweza kutokea katika pande zote mbili za vifuko vya mayai kwa mwanamke. Na hizi ndiyo vimbe kuu zilizokua zikitambulika kwa watu wengi sana lakini zipo nyingine nyingi sana.

KUVIMBA KWA MIRIJA YA UZAZI {Fallopian tubes}
Wataalamu wanaita salpingitise yaani kuvimba kwa mirija ya uzazi katika mwili wa mwanamke, na hii inawezekana ikatokea kwenye upande mmoja wa mrija wa uzazi na baadaye unaweza ukaambukiza mrija mwingine na yote ikawa imevimba, na hii nayo ni aina nyingine ya vimbe katika mwili wa mwanamke.

KUVIMBA KWA KIFUKO
CHA MAYAI {Ovary}
Wataalamu wanaita Ovary ties yaani kuvimba kwa kifuko chote cha mayai na hii inakua ni tofauti kidogo na uvimbe katika kifuko cha mayai au vimbe nyinginyingi ndogo katika kifuko cha mayai.

Kwa maana hiyo basi sote tutakuwa tumetambua aina mbalimbali za vimbe katika mwili wa mwanamke, na pale unapoambiwa una uvimbe au mke wako ana uvimbe katika mji wake wa uzazi basi ni bora kabisa ukauliza kuwa uvimbe huo ni wa aina gani ili iwe rahisi kuuondoa au kuutibia kwa haraka.

Na kama umeshawahi kupima na ukaambiwa kwamba una uvimbe katika mji wako wa mimba na hupendi kufanya upasuaji basi ni bora ukawasiliana nasi kupitia namba zetu.Kwa ushauri, vipimo na tiba dokta wetu anapatikana kwenye vituo vyake vya Dar es Salaam, Tanga, Morogoro na Mwanza.

Itaendelea wiki ijayo.

JINSI YA KUGUNDUA MAAMBUKIZI KWENYE UZAZI (DIAGNOSIS OF PID)


Baadhi ya wagonjwa watahitajika kulazwa hospitali ambapo watapewa dawa za saa na kuwa chini ya uangalizi wa haraka wa manesi na madaktari.Wagonjwa wanaohitaji kulazwa ni kama wale wanaodhaniwa kuwa wana uvimbe au jipu kwenye mfuko wa mayai yaani tube ovarian abscess au wale wenye kutapika sana na wenye homa kali pia wenye maumivu makali ya tumbo yanayofanana na kidole tumbo.

Wagonjwa ambao hawakupata nafuu baada ya matumizi ya dawa ya awali baada ya saa 48 ya kumaliza dawa na wale walioshindwa kumeza dawa pia wagonjwa wenye rirusi vya ukimwi watahitajika kulazwa.

Dawa zinazotumika kwa wale waliolazwa ni kama vile cefoxitin na clindamycine ikichanganywa na gentamycine.Nafuu ya mgonjwa itajulikana baada ya mgonjwa kujisikia vizuri na homa itashuka, pia maumivu ya tumbo yatapoa na vipimo vya maabara vitaonyesha kuwa vijidudu vimeisha.

Baadhi ya wagonjwa watahitaji upasuaji kama kutakuwa na madhara makubwa (complications) kama vile vijidudu kuingia kwenye utumbo, jipu kwenye viungo vya uzazi (pelvic abscess) usaha kwenye mfuko wa mayai (turbo ovarian abscess).

JINSI YA KUJIKINGA (PREVENTION)
Kwanza, matabibu wana wajibu wa kuelimisha jamii juu ya maambukizi yanavyotokea na kujiepusha nayo.

Pili, jamii iepushwe mwanamke kuwa na uhusiano wa kingono na wanaume wengi (multiple sexual partiners) na watu wajue matumizi sahihi ya kondom.

Mwanamke lazima amlete mwenza wake ili aweze kufanyiwa vipimo vya uhakika na akithibitika hana maambukizi ya kisonono basi ataweza kupewa dawa za kuua vijidudu vya clamydia maana ni vigumu kuweza kugundua vijidudu vya clamydia. Mwenza wake yaani atumie dawa kwa muda wa siku saba.

Ufuatiliaji wa mgonjwa kwa kumpima ufanyike baada ya wiki moja baada ya wote kutibiwa.
Kwa mwanamke apimwe kila anapomaliza hedhi na majibu yaonyeshe kuwa hana ugonjwa, upimaji ufanyike mara tatu mfululizo na majibu yaonyeshe kuwa hana ugonjwa. Mtu yeyote atakayejihisi ana tatizo hili asitumie dawa hizo bila kuonana na daktari ambaye atampima.

FAHAMU UGONJWA WA SARATANI YA TEZI DUME (PROSTATE CANCER)-4

Baada ya vipimo hivyo kama vitaashiria saratani ya tezi dume basi daktari anaweza kuamuru vipimo vingine ili kuthibitisha uwepo wa ugonjwa huo kama vile Transrectal Ultrasound au Prostatic Needle Biopsy. Tukumbuke kuwa kuwahi kugundua saratani mapema kabla ya dalili, kuna faida kubwa kwa muathirika kwani saratani ikigundulika mapema ni rahisi kutibika.

TIBA YAKE

Kuna njia kadhaa za matibabu ya saratani ya tezi dume. Hata hivyo uamuzi wa njia gani itumike unategemea ushauri na maoni ya daktari kulingana na hatua ya ugonjwa ulipofikia na umri wa mgonjwa husika.

Katika hatua za awali za ugonjwa, daktari anaweza kushauri mgonjwa atibiwe kwa kufanyiwa upasuaji na tiba ya mionzi. Hii ni katika hali ambayo kwa wagonjwa wazee, daktari anaweza kushauri mgonjwa kuwa chini ya uangalizi tu bila kufanyiwa upasuaji au bila kupatiwa tiba ya mionzi.

Iwapo saratani imesambaa na kuathiri sehemu nyingine za mwili, matibabu yake yanaweza kujumuisha upasuaji wa kuondoa korodani, matumizi ya dawa za kupunguza kiwango cha homoni ya testosterone katika damu au hormonal therapy, au matumizi ya kemikali za kuua seli za saratani (chemotherapy).

Saratani ya tezi dume ni ugonjwa wa kawaida kama yalivyo magonjwa mengine na uchunguzi na matibabu ya mapema huweza kuokoa maisha ya waathirika wengi wa ugonjwa huo.

USHAURI

Wanaume wanashauriwa kufanyiwa uchunguzi wa saratani ya kibofu cha mkojo au prostate cancer kwa kuwa imegundulika kuwa wanaume wengi wakiziona na kuzihisi dalili hizo huona soni kwenda kumwona daktari na kufanyiwa uchunguzi.

Baadhi ya watu huzihusisha na magonjwa ya zinaa au na dhana potofu za kishirikina. Wapo wanaokwenda mbali zaidi hata kuuita ugonjwa huo kuwa ni wa walawiti huku wengine wakiurahisisha kwa kuuita kuwa ni ugonjwa wa utu uzima kana kwamba saratani ya tezi dume ni jambo la kawaida kwa watu wazee.

Kwa ajili hiyo tunatoa wito kwa wanaume kutoona soni na kuwa na tabia ya kufanyiwa uchunguzi wa afya kwa jumla, hasa tezi dume angalau mara moja kwa mwaka.

Thursday, December 11, 2014

JE, VIDONDA VYA TUMBO VINATIBIKA?-3


Wiki iliyopita tulizungumzia sana madhara yanayoweza kumkuta mtu mwenye vidonda vya tumbo. Lakini leo sanasana tutaweza kuangalia dalili kubwa za tatizo hili ni zipi na mtu anapoziona katika mazingira yake ya kawaida basi aweze kufika katika vituo vya afya kwa ajili ya kuweza kuliondoa tatizo hili kwa urahisi kabisa.

DALILI ZA VIDONDA VYA TUMBO
Dalili za tatizo hili la vidonda vya tumbo hutegemeana sana na tatizo linakuwa limefikia katika kiwango gani hasa, lakini tutazizungumzia kwa jumla lakini pia kwa kuzingatia tatizo kwa kila mtu. Dalili hizo ni kama zifuatazo;

Dalili kubwa ni maumivu kama ya kuungua maeneo ya kifua, mara nyingi mtu mwenye vidonda vya tumbo anaweza akawa anasikia maumivu makali sana maeneo ya kifuani kwa mwanaume au mwanamke na wakati mwingine mtu huyu akawa anakisikia au anakihisi chakula kikiwa kinashuka hasa wakati wa kula na wakati mwingine inakuwa ni kama moto unatembea kifuani kuja tumboni na hiyo ndiyo inakuwa dalili kubwa kabisa ya tatizo hili la vidonda vya tumbo.

Lakini kuna dalili nyingine pia mfano kusikia maumivu katika tumbo, mara nyingi maumivu haya katika tumbo huwa ni kama hali ya kuungua tumboni na hii ni kwa sababu kubwa ya kwamba mtu huyu kuta zake za tumbo zinakuwa zimeathirika sana na hasa maumivu haya huwa makali zaidi wakati tumbo likiwa halina kitu au pale mtu huyu akiwa anapata chakula.

Kupungua kwa uzito wa mtu na kukonda zaidi, na hii ni kwa sababu mtu huyu mwenye vidonda vya tumbo anakuwa anapata maumivu wakati anapopata chakula na pia anakuwa akila kidogo anahisi tumbo kujaa lakini kihalisia anakuwa na chakula kichache sana ndani ya tumbo basi matokeo yake ni kudhoofu mwili wa mwanadamu huyu na hivyo kukonda sana. Kama kuna mtu unamjua anakuwa anakumbwa na dalili kama hiyo basi ni vema kufika kwenye vituo vya afya bado mapema kwa ajili ya matibabu zaidi au tupigie simu kwa msaada zaidi.

Wednesday, December 10, 2014

FAHAMU UGONJWA WA SARATANI YA TEZI DUME (PROSTATE CANCER)-3


TUMEELEZA kuhusu kansa ya tezi dume, leo tutafafanua vihatarishi vinavyochangia mwanamume kupata saratani ya tezi dume. Vifuatavyo ni baadhi yake: Kwanza kabisa ni umri. Nafasi ya kupata saratani ya tezi dume huongezeka sana hasa ukifikia umri wa karibu miaka 50 na kuendelea.

Nasaba ni kihatarishi kingine ambapo wanaume wenye historia ya tatizo hili kwenye familia zao, yaani wale ambao mmoja wa ndugu zao wamewahi kuugua ugonjwa huu huwa katika hatari ya kupata kansa hiyo kutokana na kurithi ‘gene’ za ugonjwa huo.

Suala lingine ni lishe ambapo wanaume wanaopenda kula nyama nyekundu (red meat) na walaji wa chakula chenye kiasi kikubwa cha mafuta hasa ya wanyama huwa katika hatari kubwa ya kupata saratani ya tezi dume.

Vilevile wanaume wasiopenda kufanya mazoezi, wanene na wenye upungufu wa virutubisho vya Vitamin E pia wako kwenye hatari zaidi ya kupata saratani ya kibofu cha mkojo. Wanaume wengine walio katika hatari kubwa ya kupata saratani ya tezi dume ni pamoja na wale wakulima wanaotumia aina fulani ya mbolea za kemikali, wanaofanya kazi katika viwanda vya kutengeneza matairi na wachimbaji madini, hususan aina ya cadmium.

Dalili za saratani ya tezi dume hazitofautiani na zile za kuvimba kwa tezi dume au BPH. Dalili hizo ni pamoja na, kupata shida wakati wa kuanza kukojoa, kutiririka kwa mkojo baada ya kumaliza kukojoa, kukojoa mkojo wenye mtiririko dhaifu, kukojoa mara kwa mara hasa nyakati za usiku, kujikakamua wakati wa kukojoa na kushindwa kumaliza mkojo wote na kutoa mkojo uliochanganyika na damu.

Pamoja na kueleza dalili hizo wapenzi wasomaji mnapaswa kutambua kuwa, mwanaume anapoanza kuona na kuhisi baadhi ya dalili hizo, anapaswa kujua kuwa, seli za saratani katika tezi dume lake huwa zina umri wa takribani miaka saba na kuendelea.

Iwapo saratani imesambaa mwilini kiasi cha kuhusisha sehemu nyigine za mwili, mgonjwa anaweza kuwa na maumivu makali ya mifupa katika maeneo ya nyonga, mapajani na kiunoni. Aidha mgonjwa huwa na dalili nyingine zinazoweza kumpata mgonjwa mwingine yeyote wa saratani kama vile kupungua uzito, kuhisi kichefuchefu, uchovu, kizunguzungu na kadhalika.

UCHUNGUZI

Kuna vipimo viwili ambavyo daktari anaweza kumpima mwanaume ikiwa ni hatua ya kwanza ya kugundua ugonjwa huo. Vipimo hivyo vya kwanza ni “Digital Rectal Exam (DRE)” na cha pili ni “Prostate Specific Antigen (PSA)”. DRE pamoja na PSA huonesha uwepo wa tatizo kwenye tezi dume, lakini vipimo hivi havina uwezo wa kutofautisha iwapo tatizo hilo linamaanisha saratani au uvimbe katika tezi dume. Hivyo basi, ili kuweza kutofautisha kati ya magonjwa hayo mawili, kipimo kiitwacho Prostate biopsy hufanywa.

Itaendelea wiki ijayo.

Tuesday, December 9, 2014

UTAGUNDUAJE MAABUKIZI KWENYE UZAZI (DIAGNOSIS OF PID)


Kama tulivyokwisha kusoma wiki iliyopita katika safu hii dalili za maambukizi kwenye viungo vya uzazi kwa mwanamke kama vile kutokwa uchafu sehemu za siri, homa, maumivu chini ya kitovu, kutokwa na hedhi bila mpangilio, maumivu wakati wa tendo la ndoa na maumivu wakati wa kutoka hedhi na nyinginezo, hivyo basi ili kugundua ugonjwa wa PID ni lazima kuchukua historia vizuri ya mgonjwa.

Daktari atampima tumbo mama ili kugundua maumivu ya tumbo kama yapo sehemu gani na pia kufanyia vipimo kama vile kupima uchafu kutoka ukeni na vipimo vingine kama Ultrasound.

Magonjwa mengine yanayofanana na PID: Hayo ni kama kidole tumbo (appenditis), mimba kutunga nje ya mji wa mimba hasa ikitungwa kwenye mirija na kupasuka (ruptured actopic pregnance), kupasuka uvimbe kwenye mfuko wa mayai (reptured ovarian mass) au maambukizi ya vidudu kwenye mkojo (urinary tract infection).

MADHARA YA PID
Madhara ya haraka (immediate complication) ni magonjwa yanayoweza kusababishwa na maambukizi kwenye mji wa mimba, vijidudu huweza kusambaa na kuingia kwenye utumbo (peritonitis) au wadudu kuingia kwenye mfuko wa damu (septichemia) ambapo huweza kuathiri viungo kama magoti na mgonjwa kupata ugonjwa wa arthritis na moyo (myocarditis).

Madhara ya muda mrefu ni kama maumivu wakati wa tendo la ndoa (Dyspareunia), kukosa kupata mimba (infertity), maambukizi kuwa sugu (chronic imflammatory diseases) na uwezekano wa mimba kutunga nje ya mji wa mimba yaani ectopic pregnance.

MATIBABU
Mgonjwa atapatiwa tiba kwa muda usiopungua siku 14 dawa zinazotumika ni kama levoflaxacin ikichanganywa na metronidozole.

Pia dawa zingine kama cefriaxone, dnycyline hutumika kwa kipindi cha siku 14. Matibabu haya hutumika kwa wagonjwa wa nje (out patient), wagonjwa watahitaji kuonwa na daktari baada ya siku 2 baada ya kumaliza dawa. Itaendelea wiki ijayo.

Friday, December 5, 2014

MTOTO ALIYEZALIWA AKIWA NA UZITO WA KILO 13 NA UREFU WA INCHI 22

Tumezoea kusikia watoto wakizaliwa na uzito wa kilo mbili na nusu hadi tano lakini hii inaweza kuwa sehemu ya maajabu kwani si rahisi mama kujifungua mtoto mmoja na si mapacha mwenye uzito mkubwa kama huyu aliyezaliwa huko Marekani.
Mwanamke huyo mw enye makazi yake nchini Marekani ameushangaza umma baada ya kujifungua mwanaye wa kike mwenye uzito wa kilo 13 kwa mara ya kwanza ikiwa ni uzao wake wa tano.

Mtoto huyo aliyepewa jina la Mia Yasmin amezaliwa akiwa na urefu wa inchi 22 baada ya mama yake kukaa chumba cha kujifungua kwa muda wa siku tatu.
Mama yake Alisha Hernandez alitarajia kujifungua mtoto mwenye uzito wa kilo saba lakini alijifungua mtoto huyo siku ya jumatatu.
Binamu yeka Alisha alisema baada ya kuzaliwa kwa mtoto huyo,aliamua kwenda kwenye hospitali ya watoto kwa ajili ya kumfanyia uchunguzi wa kisayansi na kubaini hana tatizo lolote na kwa sasa yuko katika hali nzuri.

Baba wa mtoto huyo Fransisco Garcia amefurahia ujio wa mtoto wake huyo na kusema ameshukuru kupata mtoto wa tano wa kike ndani ya familia yake baada ya kutangulia wengine wanne wa kike ambao ni Britney, Ximena, Yulissa na Yuliana Hernandez.

HUYU NDIYE DAKTARI ANAYETUMIA PAMPU YA BAISKELI KUFANYA UPASUAJI.



Daktari anayetumia pampu ya baiskeli kulifurisha tumbo la mwanamke anayetaka kukatwa kizazi nchini India.

Jimbo moja nchini India limesitisha shughuli ya kufungwa kizazi wanawake baada ya daktari mmoja kupatikana akitumia pampu ya kuweka pumzi kwenye baiskeli kuweka hewa kwenye matumbo ya wanawake waliokuwa wanafanyiwa operesheni hizo.

Daktari Chandra Rout, aliyetumia pampu hiyo kwa wanawake 56, Ijumaa wiki jana, aliambia BBC kuwa pampu hizo hutumiwa sana katika jimbo hilo la Orissa.
Maafisa wa serikali walisema gesi ya kaboni, ndio inapaswa kutumiwa kwa operseheni hizo wala sio pampu za kuweka hewa baiskeli.

Maafisa hao wamesema kuwa watu wanaweza kutumia hewa ya kaboni lakini utumizi wa pampu hiyo ni hatari kwa maisha ya binaadamu.

Mwezi Uliopita ,kashfa nyingine ilizuka kuhusu ukataji wa kizazi baada ya wanawake 15 kufariki walipofanyiwa upasuaji katika jimbo jengine.
Madawa ya kulevya yalitumika wakati wa upasuaji huo katika jimbo la Chhattisgarh.

Kambi za ukataji kizazi hufanyika mara kwa mara ili kuwakata kizazi kwa pamoja wanawake nchini India kama mojawapo ya mipango ya kudhibiti ongezeko la idadi ya watu nchini humo.Ripoti kwamba daktari Rout alitumia pampu ya baiskeli ili kuyafurisha matumbo ya wanawake kwa lengo la kupata nafasi ya vifaa vya upasuaji kuingia ndani, imezua pingamizi nchini India tangu habari hizo zitangazwe.

Maafisa wa serikali wamesema kuwa utumizi wa hewa ya kawaida badala ya ile ya kaboni unaweza kusababisha magonjwa kadhaa.
Mkuu wa afya katika jimbo la Orrisa Arati Ahuja amesema kuwa ukataji wa kizazi katika jimbo hilo sasa utafanyika katika hospitali zenye vifaa vyote .

''Madaktari watalazimika kuambatana na maagizo ya kimataifa ili kukinga maambukizi yoyote '',bi Ahuja alsema.Ukataji wa kizazi hufanyika kupitia kuzifunga tubu zinazobeba mayai ya mwanamke.

Hii hufanyika kupitia kufunga na kamba na baadaye kukata tubu hizo,swala linalozuia mayai na mbegu za kiume kukutana ili kutengeza mimba.

Lakini daktari Rout amesema kuwa amekuwa akitumia pampu kwa zaidi ya mara 100 lakini hakujawahi kutokea tatizo lolote.
Anasema kuwa waliamua kutumia pampu hiyo wakati kifaa kinachojulikana kama Insafleta kilipokosekana kwa upasuaji.

FAHAMU UGONJWA WA SARATANI YA TEZI DUME (PROSTATE CANCER)-2


Wiki iliyopita nilianza kuelezea ugonjwa wa saratani ya tezi dume, leo nitafafanua dalili za ugonjwa huu kama ifuatavyo:

Daktari mmoja ambaye ni miongoni mwa waathirika wa saratani hiyo na mwanzilishi wa kampeni ya kuangamiza saratani ya tezi dume nchini Tanzania ya ‘50 Plus Campaign’ anasema kuwa, ugonjwa huu ukitambuliwa mapema huweza kutibika kwa urahisi.

Kuna vihatarishi vingi vinavyochangia mwanamume kupata saratani ya tezi dume. Vifuatavyo ni baadhi yake; kwanza kabisa ni umri. Nafasi ya kupata saratani ya tezi dume huongezeka sana hasa ukifikia umri wa karibu miaka 50 na kuendelea.

Nasaba ni kihatarishi kingine ambapo wanaume wenye historia ya tatizo hili kwenye familia zao, yaani wale ambao mmoja wa ndugu zao wamewahi kuugua ugonjwa huu huwa katika hatari ya kupata kansa hiyo kutokana na kurithi ‘gene’ za ugonjwa huo. Suala lingine ni lishe ambapo wanaume wanaopenda kula nyama au (red meat) na walaji wa chakula chenye kiasi kikubwa cha mafuta hasa ya wanyama huwa katika hatari kubwa ya kupata saratani ya tezi dume.

Wanaume wasiopenda kufanya mazoezi, wanene na wenye upungufu wa virutubisho vya Vitamin E pia wako kwenye hatari zaidi ya kupata saratani ya kibofu cha mkojo. Wanaume wengine walio katika hatari kubwa ya kupata saratani ya tezi dume ni pamoja na wale wenye asili ya Afrika (weusi) ikilinganishwa na wazungu, wakulima wanaotumia aina fulani ya mbolea za kemikali, wanaofanya kazi katika viwanda vya kutengeneza matairi na wachimbaji madini, hususan aina ya cadmium.

DALILI
Katika hatua zake za awali, dalili za saratani ya tezi dume hazitofautiani na zile za kuvimba kwa tezi dume au BPH. Dalili hizo ni pamoja na, kupata shida wakati wa kuanza kukojoa, kutiririka kwa mkojo baada ya kumaliza kukojoa, kukojoa mkojo wenye mtiririko dhaifu, kukojoa mara kwa mara hasa nyakati za usiku, kujikakamua wakati wa kukojoa na kushindwa kumaliza mkojo wote na kutoa mkojo uliochanganyika na damu.

Pamoja na kueleza dalili hizo wasomaji wanapaswa kutambua kuwa, mwanaume anapoanza kuona na kuhisi baadhi ya dalili hizo, anapaswa kujua kuwa, seli za saratani katika tezi dume lake huwa zina umri wa takribani miaka saba na kuendelea.

Iwapo saratani imesambaa mwilini kiasi cha kuhusisha sehemu nyingine za mwili, mgonjwa anaweza kuwa na maumivu makali ya mifupa katika maeneo ya nyonga, mapajani na kiunoni. Aidha mgonjwa huwa na dalili nyingine zinazoweza kumpata mgonjwa mwingine yeyote wa saratani kama vile kupungua uzito, kuhisi kichefuchefu, uchovu, kizunguzungu na kadhalika.

JE, VIDONDA VYA TUMBO VINATIBIKA?-2



Kama tulivogusia wiki iliyopita kuhusiana na visababishi vinavyoweza sababisha tatizo hili la vidonda vya tumbo, navyo ni kama;•Kutofuata ratiba nzuri ya chakula.
•Mawazo (Stress).

•Kula chakula kingi kupita kiasi, hii imekuwa kama hali ya kawaida hasa kwa wanaume wengi na hata wengine kudiriki kusema kwamba “Sifa ya mwanaume ni kula sana”

wakati hii siyo sahihi na kama mwanadamu anakuwa na tabia hii ya kula sana basi kunauwezakano mkubwa wa kupata tatizo hili la vidonda vya tumbo hasa kwenye utumbo mwembamba ndiyo maana wanaume wanapatwa na tatizo hili mara mbili zaidi ya wanawake na hasa kwa wanaume wenye umri kuanzia miaka 40 – 55, lakini hii haimaanishi kwamba kwa watu wenye umri chini au juu zaidi ya hapo hawawezi kupatwa na tatizo hili.

Inaaminika kwamba asilimia 15 ya Watanzania wote wana tatizo hili la vidonda vya tumbo na nusu tu ya watu wenye tatizo hilo wanakuwa wamefanyiwa vipimo na wako tayari kwa matibabu.

MADHARA YA TATIZO HILI (CONSTIPATION)
Basi leo tutayaona madhara makubwa yanayowakuta watu wanaopatwa na tatizo kama hili na wanakuwa hawachukui hatua za haraka kulitibu moja kwa moja. Na madhara hayo ni kama;
•Kupatwa na hali ya tumbo kujaa gesi na miungurumo ya hapa na pale.

MAGONJWA YA KIKE NA JINSI YA KUKABILIANA NAYO (GYNO PROBLEMS)-2


Uvimbe katika viungo vya uzazi vya mwanamke ‘Pelvic Mass’
Uvimbe katika viungo vya uzazi vya mwanamke ni tatizo sugu linalosumbua wanawake wengi walio katika umri wa kuzaa.

\Hakuna chanzo halisi cha uvimbe ingawa baadhi husababishwa na matatizo katika mfumo wa homoni.
Uvimbe katika viungo vya uzazi vipo nje na ndani. Uvimbe unaweza kuwa mkubwa kama mimba au mdogomdogo na mwingi.

Uvimbe pia unaweza kuwa katika vifuko vya mayai ‘Ovarian Cyst’ ambapo hizi zipo aina mbili. Kuna Lutel Cyst ambayo hupona yenyewe na nyingine huwa ndogo tu katika vifuko vya mayai na hupona kwa dawa.

Kuna Cyst nyingine huwa kubwa kiasi kwamba humsababishia mwanamke apate maumivu makali upande mmoja wa tumbo kwa chini. Uvimbe ukifikia hali hii tiba yake ni upasuaji.Kuna aina nyingine ya uvimbe unakuwa nje ya kizazi, nje ya mrija na nje ya kifuko cha mayai ‘Tubal Ovarian Mass’ au kwa kifupi huitwa ‘TOM’. Aina hii ya uvimbe husababisha maumivu.

Uvimbe huu wa Cyst na TOM daima huwa na maji tu na wakati mwingine damu. Ukiwa na damu ndipo huwa na maumivu makali chini ya tumbo aidha kulia au kushoto. Uvimbe wa damu tiba yake ni upasuaji.

Kuna tatizo lingine ambalo ni vivimbe katika vifuko vya mayai. Tatizo hili hutokea katika vifuko vyote viwili vya mayai na husambaa na mwanamke hufunga kupata hedhi bila ya kuwa na mimba. Tatizo hili pia husababisha mabadiliko kwa mwanamke mikononi, miguuni na wengine huota ndevu na hata sauti hubadilika na kuwa nzito.

Athari za kuwepo na uvimbe katika viungo vya uzazi ni kutoshika mimba, mimba kuharibika, maumivu yasiyoisha chini ya kitovu, maumivu wakati wa tendo la ndoa, damu kutoka ukeni bila ya mpangilio.
Uchunguzi na tiba ya tatizo hili hufanyika katika hospitali za mikoa kwenye kliniki za magonjwa ya kike na matatizo ya uzazi. Endapo uvimbe utakuwa mkubwa sana kwa kuchelewa kutibiwa, athari zake ni kuondolewa kizazi.

Maumivu wakati wa hedhi
Maumivu wakati wa hedhi ni tatizo li nalowasumbua wanawake.
Zipo aina mbili za maumivu, kwanza ni ‘Primary Amenorrhoea’ ambapo ni maumivu yanayowasumbua sana wasichana hasa baada ya kuvunja ungo.

Maumivu haya husababishwa na matatizo katika mfuko wa homoni kutokana na kizazi cha usichana kuwa hakijatanuka vizuri na bado kinaendelea kukua.Tatizo hili huisha kwa tiba baada ya uchunguzi wa kina katika mfumo wa homoni, vilevile likiendelea kwa muda mrefu huwa linaisha baada ya kujifungua.

Msichana pia anaweza kupatwa na tatizo la kutokwa na damu kidogokidogo au nyingi kwa muda mrefu hata zaidi ya mwezi. Hii inatokana na tatizo katika mfumo wa homoni.

Aina nyingine ya maumivu haya ni Secondary Dysmenorrhoea. Hii huwapata wanawake ambao awali hawakuwa na maumivu wakati wa usichana na wanafikia utu uzima wanaanza kupata maumivu. Maumivu haya ya hedhi katika umri wa zaidi ya miaka ishirini huweza kusababishwa na maambukizi sugu katika mfumo wa uzazi.

Matatizo ya maumivu wakati wa hedhi huchunguzwa na kutibiwa kwenye hospitali ya mkoa katika kliniki za magonjwa ya kike na uzazi. Tiba inaweza kuwa ni dawa au upasuaji kutegemea na ukubwa wa tatizo.

Matatizo katika mfumo wa uzazi wa watoto
Matatizo haya yapo mengi ambayo huwasumbua watoto wadogo wa kike na wa kiume kabla ya balehe na kuvunja ungo.Watoto kama ilivyo watu wazima hupatwa na matatizo katika mfumo wa uzazi na athari kubwa hutokea baadaye ukubwani. Tunazungumzia mfumo wa uzazi wa watoto na jinsi ya kuyagundua katika makala zijazo.

Monday, December 1, 2014

SIKU YA UKIMWI DUNIANI; MKOA WA NJOMBE BADO UNAONGOZA KWA MAAMBUKIZI




Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS), Dkt. Fatma Mrisho akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kuhusu Kauli Mbiu ya Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani isemayo, Tanzania Bila Maambukizi Mapya ya VVU, Vifo Vitokanavyo na Ukimwi na Ubaguzi na Unyanyapaa inawezekana inayolenga kupunguza maambukizi Mapya ya Ukimwi, kupunguza vifo vitokanavyo na Ukimwi na kukomesha vitendo vya unyanyapaa kwa asilimia Sifuri.

LEO ni Siku ya Ukimwi Dunia ambapo Kitaifa maadhimisho hayo yanafanyika mkoani Njombe. Kwa takwimu zilizotolewa na Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (Tacaids) 2011/12, Mkoa wa Njombe, Mbeya na Iringa ni vinara wanaoongoza kwa maambukizi ya Virusi vya Ukimwi nchini huku Pemba na Unguja zikiwa chini kwa maambukizi hayo.



Mkoa wa Njombe unaongoza kwa maambukizi ukiwa na asilimia 14.8, ukifuatiwa na Iringa yenye maambukizi asilimia 9.1 na Mkoa wa Mbeya unashika nafasi ya tatu kwa asilimia 9.

Mikoa mingine na asilimia za maambukizi katika mabano ni Shinyanga (7.4), Ruvuma (7.0), Dar es Salaam (6.9) Rukwa (6.2), Katavi (5.9), Pwani (5.9),Tabora (5.1), Kagera (4.8) na Geita (4.7).

Mikoa mingine aliyoitaja ni Mara (4.5), Mwanza (4.2), Mtwara (4.1), Kilimanjaro (3.8), Morogoro (3.8), Simiyu (3.6), Kigoma (3.4), Singida (3.3), Arusha (3.2), Dodoma (2.9), Lindi (2.9), Tanga (2.4), Manyara (1.5), Unguja (1.2) na Pemba (0.3).

Nchi nzima, asilimia 5.1 ya wanawake na wanaume wenye miaka 15-49 wana maambukizi ya VVU. Wanawake wana kiwango kikubwa cha maambukizi kuliko wanaume mijini na vijijini. Asilimia 7.2 ya wakazi wa mijini wana maambukizi ya VVU ukilinganisha na asilimia 4.3 ya wakazi wa vijijini.

Katika takwimu hizo, Watanzania walioonesha kuwa na ufahamu sahihi wa elimu kuhusu Virusi vya Ukimwi (VVU) na Ukimwi wanafikia asilimia 60 jambo linalosababisha kuwepo mwamko mdogo wa kubadili tabia.

Kuhusu tohara kwa wanaume, takwimu zilionyesha inapunguza maambukizi ya Ukimwi kwa asilimia 60 na kusisitiza kuwa ipo haja ya kutoa elimu zaidi juu ya uelewa wa ugonjwa huo.

Visababishi vya Ukimwi:
Miongoni mwa vipengele muhimu ni pamoja na vifuatavyo:
-Uasherati
-Matumizi madogo na yasiyo endelevu ya kondomu
-Ngono za marika yanayotofautiana sana
-Kuwa na wapenzi wengi.
-Ukosefu wa elimu ya maambukizo ya UKIMWI
-Kuwepo kwa maradhi mengi ya ngono kama vile tutuko, homa,
-Jando kwa wanaume
-Sababu za mahali husika, za kushamiri kwa janga nchini ni:
-Umaskini na biashara ya ngono pamoja na ongezeko la wafanyabiashara wa ngono
-Tabia mbaya za ngono za wanaume kutokana na kuruhusiwa kimila kuwa na nguvu
-Kukosekana usawa wa kijamii, kiuchumi, kisiasa na kijinsia pamoja na unyanyaswaji wa wanawake na wasichana walio ndani na nje ya mahusiano.
-Matumizi ya pombe na dawa za kulevya.
-Tabia za kimila (kama vile utakasaji wajane na jando na unyago)
-Safari za aina zote zinazosababisha kuwa mbali kwa wanandoa na ongezeko la mahawara
-Kutokutahiriwa

Thursday, November 27, 2014

JE, VIDONDA VYA TUMBO VINATIBIKA?

watu wengi wanahangaika sana na tatizo la vidonda vya tumbo, pasipo kuwa na uhakika kama wanaweza kupona. Lakini leo tutaweza kujua maana ya vidonda vya tumbo (Ulcers), dalili zake, visababishi vyake na hata jinsi gani Watanzania waweze kujiepusha na maradhi hayo na tiba yake.


MAANA YA VIDONDA VYA TUMBO (ULCERS)

VIDONDA VYA TUMBO hotokea pale kuta za tumbo zinapotoa asidi iitwayo Hydrochrolic acid katika tumbo ambayo kazi yake ni kufanya mmeng’enyo wa chakula aina ya protein ndani ya tumbo, na ikumbukwe kwamba kuta za tumbo asili yake ni protein (protein in nature), na kwa maana hiyo basi kama kuta za tumbo zimeshatoa asidi hii katika tumbo kwa ajili ya mmeng’enyo wa chakula ndani ya tumbo na ikakuta ndani ya tumbo hakuna chakula cha kumeng’enywa basi mmeng’enyo huu huanza kufanyika katika kuta za tumbo na baadaye kuta zinakuwa zimelika hivyo kusababisha tatizo kubwa la vidonda hivyo.

Wataalamu wamegawanya vidonda vya tumbo katika makundi makubwa mawili, nayo ni;
Vidonda vya tumbo vinavyotokea tumboni (Gastric ulcers), hii ni ile hali ya kulika kwa kuta za tumbo, inapotokea hali hiyo huweza kuambatana na maumivu makali maeneo ya tumbo;

Vidonda vya tumbo vinavyotokea kwenye utumbo mwembamba (Duodenary ulcers), hii ni ile hali ya kulika kwa kuta za utumbo mwembamba ulio karibu na tumbo, na utumbo mwembamba unaweza kupata vidonda hadi inchi 11 kutoka sehemu inayopokelea chakula kutoka tumboni, na kwa maana hiyo maumivu huweza kusambaa hadi maeneo ya chini ya tumbo.

VISABABISHI
Kutokufuata ratiba nzuri ya chakula, kama mwanadamu anakua hapati chakula kwa wakati sahihi na anakaa muda mrefu bila kula, basi husababisha vidonda vya tumbo kwani kuta za tumbo zinapotengeneza asidi hii kwa ajili ya kumeng’enya chakula na wakati huo huo anakuwa hajapata chakula kwa muda mrefu basi mmeng’enyo huu huanza kufanyika kwenye kuta za tumbo na baadaye inaweza kusababisha vidonda hivyo.

Mawazo (stress), kwa mwanadamu anayekumbwa na msongo wa mawazo (stress) na wakati huo huo akawa hali vizuri, anaweza kukumbwa na maradhi hayo kwani husababisha kutengenezwa kwa Hydrochrolic acid ndani ya tumbo.

Kwa ushauri, vipimo na tiba dokta anapatikana kwenye vituo vyake vya Dar es Salaam, Tanga, Morogoro na Mwanza.Nawatakia afya iliyo njema kabisa.

Itaendelea wiki ijayo.

FATUMA RAMADHANI RASHID AKIMBIWA NA MUNGU KISA TUMBO KUJAA MAJI

Stori: Waandishi Wetu
MAMA wa watoto watano, Fatuma Ramadhani Rashid (37) amejikuta akitelekezewa watoto hao na mumewe Matola, kisa akidai ni yeye tumbo lake kujaa maji. Tukio hilo la kusikitisha lilitokea Juni 12, mwaka huu, Ukonga-Mongolandege, Dar ambapo mama huyo alikuwa akiishi na mume wake huyo lakini mara baada ya kuanza kwa dalili za ugonjwa huo mumewe alianza visa na kutoweka nyumbani.


Mama wa watoto watano, Fatuma Ramadhani Rashid aliyetelekezwa na mumewe kutokana na tumbo kujaa maji.

“Tulikuwa tukiishi vizuri lakini kutokana na maradhi yaliyonikumba mume wangu aliamua kunikimbia na kunitelekezea watoto hawa, sasa watoto wamekuwa ombaomba,’’alisema mwanamke huyo.
Hata hivyo, kufuatia na hali ya maisha yao kuendelea kuwa ngumu, nyumba hiyo waliyopanga walifukuzwa na kubaki wakitangatanga huku wakisaidiwa na majirani waliokuwa wakiwaonea huruma.
Nyaraka za hospitali za Fatuma Ramadhani Rashid.

Alielezea kuwa watoto wake wameamua kuishi mitaani baada ya kushindwa kwenda shule kwa kukosa ada ambapo mmoja wao alikuwa kidato cha kwanza katika Shule ya Sekondari Mbuyuni- Chanika wilayani Ilala, Dar.

Watoto watano aliotelekezewa Fatuma Ramadhani Rashid.

Mama huyo alisema kwa ugonjwa wake huo, alikwenda Hospitali ya Amana na kuambiwa tumboni kumejaa maji lakini anaweza kutibiwa pasipo kufanyiwa oparesheni ila anatakiwa kuwa na Sh. 500,000.
Mama huyo aliomba yeyote atakayeguswa na tatizo la familia yake na yeye mwenyewe anaweza kumchangia kwa simu; 0783 521 180 Fatuma Ramadhani.

Wednesday, November 26, 2014

JK APOKEA SALAMU ZA KHERI TOKA KWA RAIS BARACK OBAMA WA MAREKANI


Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mh.Liberata Mulamula akiwasilisha kwa Rais Dkt.Jakaya M rishoKikwete salamu za kumtakia kheri na afya njema kutoka kwa Rais wa Marekani Barack Obama jijini Baltimore, Maryland, Marekani.


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea kwa furaha na ujumbe kutoka Ubalozi wa Tanzania ulioko jijini Washington DC uliomtembelea kumjulia hali na kwasilisha salamu za Rais Barack Obama.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Balozi Liberata Mulamula na ujumbe wake wa maafisa waandamizi wa ubalozi wa Tanzania nchini Marekani baada ya kupokea salamu maalumu za kumtakia kheri na afya njema kutoka kwa Rais Barack Obama wa Marekani jijini Baltimore, Maryland, Marekani.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na maafisa waandamizi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani uliopo Washington D.C. wakati walipomtembelea mjini Baltimore Maryland ambapo balozi Liberata Mulamula aliwasilisha kwa Rais Kikwete Salamu maalum za kumtakia kheri na afya njema kutoka kwa Rais Barack Obama jijini Baltimore, Maryland, Marekani. Picha na Freddy Maro

STEVEN JOHN ANATESEKA NA SARATANI YA TUMBO..TUMSAIDIE

Stori: Makongoro oging’
“Maishi yangu yako hatarini, nachungulia kaburi, nimeteseka kwa muda mrefu bila kupona wala msaada, nimetoka katika ukoo maskini unaotegemea kwa asilimia kubwa kilimo cha jembe la mkono, nitapata wapi shilingi milioni moja na laki tano na arobaini na tano elfu ili nikatibiwe?”
Hii ni sehemu ya kilio cha Steven John anayesumbuliwa na ugonjwa wa saratani ya tumbo.


Steven John anayesumbuliwa na ugonjwa wa saratani ya tumbo.

AMETOKA WAPI?
John ni mkazi wa Kijiji cha Sokoni One, mkoani Arusha, amekua akisumbuliwa na ugonjwa huo kwa kipindi cha miaka miwili bila kupata nafuu na hali yake inazidi kubadilika kila mara ingawa ametakiwa na madaktari wa Hospitali ya Taifa Muhimbili kufanyiwa upasuaji wa pili baada kufanyiwa hivyo huko nyuma.
Mgonjwa huyu anazunguka huku na kule kutafuta fedha bila mafanikio na kwa sasa anawaomba watu wenye huruma wamchangie ili akamilishe tiba yake.

FAMILIA INAISHIJE?
“Nina familia ya mke na watoto nane, walikuwa wakiishi kwa kunitegemea lakini kwa kipindi cha miaka miwili sasa wamekosa msaada wangu, kwani nimekuwa nikizunguka hospitali kadhaa huku nikiwa na mke wangu kutafuta matibabu lakini tunakumbana na vikwazo vingi kikiwemo cha ukosefu wa fedha.

“Jambo hilo linanifanya niwe na mawazo mengi sana ya kumtaka Mola aichukue roho yangu, kwani nimeanza kuchungulia kaburi kuliko kuisumbua familia yangu inayoteseka kwa kukosa matunzo nami kuteseka kwa maumivu makali, nimekuwa ombaomba hapa mjini ili nipate fedha lakini hakuna mafanikio.


Muonekano wa sehemu za kutolea haja kubwa na ndogo.

UGONJWA ULIANZAJE?
“Nakumbuka ugonjwa huu ulinianza Oktoba mwaka juzi, ulianza kwa tumbo kuunguruma pia nilipoteza hamu ya kula hali iliyonifanya niende katika zahanati ya kijijini kwetu, wao walinieleza kwamba nina vidonda vya tumbo walinipa dawa nikapata nafuu kidogo lakini baada ya muda hali ilibadilika na kuwa mbaya.

“Ikatokea kwa siku kumi na saba sikwenda haja kubwa, tumbo lilivimba kiasi cha kutaka kupasuka, nikaenda Hospitali ya Mount Meru, Arusha, nilifanyiwa vipimo kikiwemo cha x-ray, wakagundua kuwa sehemu ya haja kubwa kumeziba ikabidi wanifanyie upasuaji, pia walitoboa tumbo nikawa najisaidia kwa kutumia mpira.

“Baada ya siku mbili tangu nifanyiwe upasuaji huo, kibofu cha mkojo kikawa kinauma baada ya mrija kuziba, nilifanyiwa upasuaji nikawa najisaidia kwa kutumia mpira baada ya tumbo kutobolewa tena, huu mfuko wa kulia ni wa haja ndogo na wa kushoto ni wa haja kubwa.

AKATWA KIPANDE CHA NYAMA
“Nikiwa bado nipo Mount Meru madaktari walikata kipande cha nyama pajani na kukipeleka Hospitali ya Nairobi nchini Kenya kwa vipimo na majibu yalipokuja iligundulika kuwa nina saratani ya utumbo mpana.
“Walinieleza nije hapa Dar, Hospitali ya Ocean Road ambapo niliendelea na matibabu, ilipofika Septemba 16, mwaka huu nilishauriwa niende Muhimbili nikafanyiwe vipimo kama saratani imeisha.

“Lengo lilikuwa kama ugonjwa hakuna, niweze kurejeshewa mfumo wa haja kubwa na ndogo katika hali ya kawaida. Hata hivyo, nilipofika Muhimbili nilifanyiwa kipimo kimoja cha City Scan na vingine bado, ndiyo maana nahangaika kutafuta fedha ili nikakamilishiwe vipimo hivyo kisha nifanyiwe upasuaji mwingine.

“Kwa kuwa sina fedha, nawaomba wasamaria wema wanisaidie ili nifanyiwe vipimo na upasuaji mwingine, sina raha hapa nilipo. Napatikana kwa simu namba 0712 820440 au 0752 225061,” alisema John kwa huzuni.

BABY MADAHA ADAIWA KUAMBUKIZWA GONJWA BAYA

Na Mwandishi Wetu
MSANII wa Bongo Fleva, Baby Madaha anadaiwa kuambukizwa gonjwa hatari la zinaa ambalo halikutajwa jina lakini likielezwa kuwa linampa wakati mgumu kisaikolojia. Chanzo kimoja kimeiambia show bize kuwa, nyota huyo amekuwa akitumia dawa za kusafisha haja ndogo kwa muda mrefu lakini bila mafanikio.


Msanii wa Bongo Fleva, Baby Madaha.

Show bize ilimsaka Baby Madaha mwenyewe ambapo aling’aka kwa ukali.
“Hizo habari nani kakupa wewe? Hayo si moja ya maisha ya wanadamu kwani kipi kibaya hapo? Oke, sawa naumwa na hao wanaume wanaotaka nikatibiwe wanajua mimi naumwa nini? Magonjwa ya zinaa si yana dawa?” alihoji.

Hata hivyo, mrembo huyo alisema yeye ana tatizo la haja ndogo kuwa chafu lakini si ugonjwa wa zinaa.

MTOTO CAREEN MPONDO (4) ANATESEKA NA UGONJWA WA FIGO ANAHITAJI MSAADA WAKO

Stori: Imelda Mtema
Mtoto Careen Mpombo (4) (pichani), mkazi wa Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam, yuko katika mateso makali kufuatia kusumbuliwa na figo moja ambayo haifanyi kazi.


Mtoto Careen anayesumbuliwa na figo moja ambayo haifanyi kazi.

Licha ya kuugua figo, mtoto huyo pia ana ugonjwa wa mafindofindo (Tonsillitis) unaomfanya akose raha kutokana kuwa na maumivu makali yanayosababisha ashindwe kula.
Akizungumza na gazeti hili, mama mzazi wa mtoto huyo ambaye pia huitwa Careen, alisema mwanaye alianza kuumwa kwa kuvimba mashavu akadhani ana mafindofindo hivyo aliamua kumpeleka katika Hospitali ya Kisarawe iliyopo mkoani Pwani.

“Hospitalini walimpa dawa ya PEN V na kumchoma sindano wakijua ni mafindofindo lakini kadiri siku sinavyozidi kusonga mbele ndivyo anavyozidi kuumwa.“Imefikia sasa anashindwa kulala kabisa, tulimrudisha hospitali baada ya kuona tumbo limeanza kuvimba, tukashauriwa kumpeleka Hospitali ya Taifa Muhimbili.


Mtoto Careen akiwa na maumivu makali kutokana na ugonjwa wa figo.

“Madaktari waliniambia nimpeleke Hospitali ya Regency kwa vipimo zaidi ambapo waligundua kuwa figo yake moja haifanyi kazi na ana mafindofindo, wakaniambia anatakiwa kupima kipimo ambacho atakatwa nyama gharama yake ni Shilingi 140,000,” alisema mama huyo.

Aliongeza kuwa, baada ya kuambiwa hivyo aliumia sana kwa kuwa alijua mtoto wake atazidi kuteseka kwa kuwa hana uwezo ya kupata kiasi hicho cha fedha kwa sababu mume wake alipata ajali ya gari na bado ni mgonjwa na yeye hana kazi na isitoshe anaumwa.

“Nilivyoambiwa nahitaji kutoa shilingi laki moja na elfu arobaini niliumia na kutoka machozi kwa kuwa nilijua wazi mtoto wangu atazidi kuteseka kwa kuwa sina fedha hizo, sasa nashinda nikilia, naomba Watanzania wanisaidie,” alisema mama huyo.

Kama umeguswa na habari ya mtoto Careen na unapenda kumsaidia, wasiliana na mama yake kwa namba 0657 628 889, KUTOA NI MOYO SIYO UTAJIRI.

MWIGIZAJI WA FILAMU TANZANIA DK CHENI ALISHWA SUMU TENA!

Stori: Imelda Mtema
Staa wa kiume wa sinema za Kibongo, Mahsein Awadh ‘Dk Cheni’, kwa mara nyingine alilazwa katika Hospitali ya TMJ iliyopo Mikocheni jijini Dar baada ya kudaiwa kula chakula kinachosadikika kuwa na sumu (poisonous food).

Mahsein Awadh ‘Dk Cheni’ akiwa hoi hospitalini.

Akizungumza na mwandishi wetu wikiendi iliyopita Dk Cheni alisema kuwa alikuwa mshehereshaji (MC) kwenye harusi moja iliyofanyika maeneo ya Sinza jijini Dar ndipo akala chakula hicho ambapo muda mfupi baadaye alianza kujisikia vibaya ‘kichina’.

Staa huyo alisema kuwa baada ya hatua chache kutoka ukumbini, tumbo lilianza kumuuma kisha akaishiwa nguvu ndipo akaweka gari pembeni na kupiga simu kwa ndugu kuomba msaada.
Dk Cheni aliendelea kueleza kuwa baada ya kupata msaada moja kwa moja alipelekwa kwenye Hospitali ya Burhani jijini Dar.

‘Dk Cheni’,

Alisema kuwa baadaye alihamishiwa kwenye Hospitali ya TMJ ambapo madaktari walipompima waligundua alikuwa amekula chakula chenye sumu ndipo wakampatia matibabu na kulazwa.
Alisema siku ya pili yake aliruhusiwa huku akisema kitendo hicho kimemsikitisha mno.

Siyo mara ya kwanza kwa Dk Cheni kulishwa chakula chenye sumu kwani safari hii ni mara ya pili ambapo mwaka jana alilazwa tena kwa ishu kama hiyo, jambo ambalo haelewi kwa nini inakuwa hivyo

FAHAMU UGONJWA WA SARATANI YA TEZI DUME (PROSTATE CANCER)



Wiki hii wasomaji wengi wamependa nijadili kuhusu kansa ya tezi dume au Prostate Cancer kwa kitaalamu zaidi.Ugonjwa huu huweza kusababisha vifo. Ili kuujua vyema ugonjwa huo tafadhali fuatilia makala haya.

Saratani ya tezi dume upo katika nafasi ya tatu kwa kusababisha vifo vinavyotokana na kansa kwa wanaume duniani. Pia ni chanzo kikuu cha vifo vinavyosababishwa na saratani kwa wanaume wenye umri wa miaka 50 na kuendelea. Hata hivyo, satarani ya tezi dume kwa sasa inawapata sana wanaume kuanzia miaka 25.

Lakini kabla ya kuendelea mbele hebu kwanza tujue tezi dume ni zipi. Kama tulivyosema, neno saratani ni jina la ugonjwa ambalo hutokea wakati chembechembe za uhai au seli katika sehemu fulani ya mwili zinapoanza kukua bila kufuata utaratibu wa mfumo wa mwili na kutengeneza vijiuvimbe vidogovidogo.

Kwa kawaida seli huwa zinajigawa, kupevuka na baadaye kufa kwa kufuata taratibu za mfumo wa mwili. Lakini seli za saratani hazifuati mfumo huo. Badala ya kufa, zenyewe huishi muda mrefu kuliko chembechembe za kawaida na wakati huohuo huendelea kutengeneza seli nyingine na kuwa uvimbe wa saratani au tumour.

Tezi dume linapatikana katika mwili wa mamalia dume tu na pale seli katika kiungo hicho zinapoanza kukua bila kufuata utaratibu wa mfumo wa mwili hapo ndipo mtu hupata saratani ya tezi dume.
Saratani ya tezi dume huwapata wanaume tu na hasa wenye umri wa takribani miaka 50 na kuendelea. Saratani hii imethibitika kushika nafasi ya pili, ukiachia mbali saratani ya mapafu kwa kusababisha vifo vya wanaume wenye umri wa takribani miaka 50 na kuendelea.

Tafiti za Chama cha Saratani cha Marekani (ACS) na cha Afrika Kusini (CANSA) zimebaini kuwa, mwanaume mmoja kati ya sita hupata saratani ya tezi dume katika uhai wake. Kutokana na takwimu za mwaka 2010 za dunia nzima, malaria iliua watu laki tano, kifua kikuu watu milioni 2.1, Ukimwi watu milioni 1.8 na saratani watu milioni 9.9.

Kwa mujibu wa takwimu hizo, idadi ya watu waliofariki dunia kutokana na ugonjwa wa saratani ni kubwa ikilinganishwa na ya magonjwa mengine. Itaendelea wiki ijayo.

Monday, November 24, 2014

TARATIBU ZA TIBA ZA RAIS WA TANZANIA DKT. J.K KIKWETE ZAKAMILIKA




Taratibu za matibabu ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete (Pichani), zimekamilika leo, Jumatatu, Novemba 24, 2014.

Taratibu hizo za matibabu za Mheshimiwa Rais Kikwete zimekamilika kiasi cha saa 12 asubuhi ya leo wakati madaktari bingwa katika Hospitali ya Johns Hopkins iliyoko mjini Baltimore, Jimbo la Maryland, Marekani, walipomfanyia hatua ya mwisho ya tiba.

Hata hivyo, Rais Kikwete ataendelea kupumzika na kuangaliwa kwenye Hoteli Maalum inayohusiana na Hospitali ya Johns Hopkins kwa siku mbili hadi tatu kabla ya kuanza safari ya kurejea nyumbani.
-----------------------------------------------------
Taratibu za matibabu ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete (Pichani), zimekamilika leo, Jumatatu, Novemba 24, 2014.

Taratibu hizo za matibabu za Mheshimiwa Rais Kikwete zimekamilika kiasi cha saa 12 asubuhi ya leo wakati madaktari bingwa katika Hospitali ya Johns Hopkins iliyoko mjini Baltimore, Jimbo la Maryland, Marekani, walipomfanyia hatua ya mwisho ya tiba.

Hata hivyo, Rais Kikwete ataendelea kupumzika na kuangaliwa kwenye Hoteli Maalum inayohusiana na Hospitali ya Johns Hopkins kwa siku mbili hadi tatu kabla ya kuanza safari ya kurejea nyumbani.

Kama kila kitu kitakwenda kama ilivyopangwa na madaktari, Rais Kikwete anatarajiwa kurejea nyumbani Jumamosi, Novemba 29, 2014.

Rais Kikwete aliondoka nchini Alhamisi ya Novemba 6, 2014, kwenda kufanyiwa uchunguzi wa afya yake lakini madaktari katika Hospitali ya Johns Hopkins waliamua kumfanyia upasuaji wa tezi dume Jumamosi ya Novemba 8, 2014.

Rais Kikwete anaendelea kuwashukuru Watanzania kwa sala na maombi yao ya kumtakia heri ya kupona haraka na kurejesha afya njema katika kipindi chote cha ugonjwa wake.

Imetolewa na:



Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.
24 Novemba,2014

JINSI YA KUTUNZA NGOZI YENYE MAFUTA


Ngozi yenye mafuta kwa kawaida huwa inang'ara, nene na yenye rangi iliyotitia. Mara nyingi ngozi yenye mafuta mengi sana huwa na chunusi nyingi na vipelepele na mara nyingine huwa na chunusi zenye vichwa vyeusi. Katika aina hizi za ngozi mafuta hutokana na tezi za sebaceous na kuzalisha mafuta zaidi ya kiwango kinachotakiwa. Mafuta hayo husambaa katika ngozi na kuifanya iwe na mafuta mafuta.
Sababu zinazosababisha ngozi kuwa na mafuta:
• Kuridhi.
• Lishe.
• Kiwango cha homoni mbalimbali mwilini.
• Ujauzito.
• Vidonge vya kuzuia mimba.
• Baadhi ya vipodozi .
• Hali ya unyevu (humidity) na hali ya hewa ya joto.

Namna ya kutunza ngozi zenye mafuta
Faida kubwa ya kuwa na ngozi yenye mafuta ni kuwa haizeeki kwa haraka ikilinganishwa na aina nyinginezo za ngozi. Miongoni mwa mambo yanayosaidia ili kuitunza ngozi yenye mafuta na kuiepusha na chunusi na hali isiyopendeza ni:-

1. Ngozi yenye mafuta inahitajia kusafishwa vyema kwa maji ya moto na sabuni ili kuzuia vinyweleo visizibwe na mafuta.

2. Epusha vifaa vigumu visikwaruze uso wako na kupelekea ngozi kubanduka, kwani suala hilo husababisha tezi za mafuta kufanya kazi zaidi ili kujaza sehemu iliyopotea ya mafuta.

3. Epuka kutumia vipodozi ambavyo huifanya ngozi yako ipotze maji au kukauka. Kwani husababisha sehemu ya juu ya ngozi inyauke, na hivyo kusababisha mafuta kuziba vinyweleo na kupelekea kutokea vichwa vyeusi.

4. Jitahidi kuitunza vyema ngozi yako na kuisafisha vizuri. Jaribu kuosha uso mara mbili au tatu kwa siku. Usioshe mara nyingi kwani kufanya hivyo huufanya uso kutoa mafuta zaidi.

5. Chagua kile unachosafishia kwa makini, jiepushe kutumia cream nzito nzito au vifaa vugumu wakati wa kuosha uso wako. Ni bora utumie sabuni za kawaida zisizokuwa na madawa. Unaweza kutumia lotion ya kuua bacteria au sabuni zisizo na dawa nyingi (lightly medicated), au sabuni zenye madini mbalimbali. Ni bora usioshe au kutumia lotion au michanganyiko yenye alkoholi.

6. Tumia maji ya moto au ya vuguvugu wakati unaosha uso wako.

7. Wakati unapoosha uso wako, ukande kwa kutumia ncha za vidole, jiepushe kupaka sabuni moja kwa moja usoni, inaweza kuganda na kuzuia vinyweleo kuziba.

8. Kutumia mask za udongo (clay) na tope (mud) husaidia katika ngozi za aina hii. Ni bora utumie mask mara moja au mbili kwa wiki.

9. Jitahidi kutumia vipodozi vya uso ambavyo vimetengenezwa kwa ajili ya ngozi yenye mafuta.

JINSI YA KUONDOA MADOA YA CHUNUSI

JUISI YA LIMAO NA MAJI YA ROSE
Chukua maji ya rose kiasi kama ni kijiko kimoja na maji ya limao nayo yawe kijiko kimoja paka eneo liloathiriwa na madoa, kaa kwa muda wa nusu saa mpaka saa moja kisha osha uso wako, fanya hivyo kwa muda wa wiki tatu utapona madoa doa yote usoni.

Juisi ya limao na liwa
Chukua juisi ya limao kiasi changanya na liwa kisha paka eneo lililoathirika, kaa kwa muda wa dakika tano utaona matokeo.
Juisi ya limao na unga wa mdalasini pia ni tiba nzuri ya kusafisha uso kuondokana na madoa yote.


Asali na mdalasini
Chukua vijiko vitatu vya asali na kimoja cha mdalasini changanya kisha paka usoni pia ni tiba nzuri inasaidia kwa kiasi kikubwa.

Apple na asali
Chukua apple liponde changanya na asali kiasi, kisha paka usoni mbali na kutibu madoa pia inatibu chunusi.

Maji ya kitunguu swaumu
chukua maji ya kitunguu swaumu paka kwenye madoa yote utaona matokeo.
Nyanya
chukua kipande cha nyanya paka usoni kisha kaa kwa muda wa saa moja nayo ni tiba nzuri.

Tango
Tango pia ni tiba, chukua kipande sugua uso wako kila siku asubuhi utaona matokeo.


Papai

Chukua papai liponde kisha paka usoni litakusaidia kuondoa tatizo la madoa yote usoni.

Saturday, November 22, 2014

MAADHIMISHO YA SIKU YA UKIMWI DUNIANI KUFANYIKA KITAIFA MKOANI NJOMBE


Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya Taifa ya kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) , Dkt. Fatma Mrisho akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kuhusu Kauli Mbiu ya Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani isemayo, Tanzania Bila Maambukizi Mapya ya VVU, Vifo vitokanavyo na Ukimwi na Ubaguzi na Unyanyapaa inawezekana inayolenga kupunguza maambukizi Mapya ya Ukimwi, kupunguza vifo vitokanavyo na Ukimwi na kukomesha vitendo vya unyanyapaa kwa asilimia Sifuri.

Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya Taifa ya kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) , Dkt. Fatma Mrisho akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya Siku ya Ukimwi duniani yatakayofanyika kitaifa mkoani Njombe kuanzia Novemba 24, 2014 na kufikia kilele chake Desemba 1, 2014.

Mkurugenzi wa ufuatiliaji wa Tathmini wa Ofisi ya Taifa ya kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) Dkt. Jerome Kamwela akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kuhusu utoaji wa huduma na upatikanaji wa dawa za kufubaza makali ya Virusi vya Ukimwi kwa watu wanaoishi na VVU katika maeneo mbalimbali nchini.

Mkurugenzi wa ufuatiliaji wa Tathmini wa Ofisi ya Taifa ya kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) Dkt. Jerome Kamwela akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kuhusu utoaji wa huduma na upatikanaji wa dawa za kufubaza makali ya Virusi vya Ukimwi kwa watu wanaoishi na VVU katika maeneo mbalimbali nchini.

Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa TACAIDS akiwaonesha waandishi wa habari (hawapo pichani) mbinu na elimu inayotolewa na TACAIDS katika maeneo mbalimbali ikiwemo matumizi ya mipira ya kike kwa wanawake ili kuzuia maambukizi mapya ya VVU.

RAIS KIKWETE ATOLEWA NYUZI KATIKA MSHONO, AFYA YAKE YAZIDI KUIMARIKA


Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akitoka katika hospitali ya Johns Hopkins iliyopo Baltimore Maryland baada ya kutolewa nyuzi katika mshono baada ya kufanyiwa upasuaji wiki iliyopita. Rais Kikwete anatarajiwa kurudi tena hospitalini hapo Jumatatu kwa ukaguzi wa maendeleo ya kidonda na ushauri. Kulia kwake ni Daktari wa Rais Profesa Mohamed Janabi.…



Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akitoka katika hospitali ya Johns Hopkins iliyopo Baltimore Maryland baada ya kutolewa nyuzi katika mshono baada ya kufanyiwa upasuaji wiki iliyopita. Rais Kikwete anatarajiwa kurudi tena hospitalini hapo Jumatatu kwa ukaguzi wa maendeleo ya kidonda na ushauri. Kulia kwake ni Daktari wa Rais Profesa Mohamed Janabi.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa amepumzika kwenye hoteli maalumu baada ya kutoka katika hospitali ya Johns Hopkins iliyopo Baltimore Maryland alikotolewa nyuzi katika mshono baada ya kufanyiwa upasuaji wa Tezi Dume wiki iliyopita. Rais Kikwete anatarajiwa kurudi tena hospitalini hapo Jumatatu kwa ukaguzi wa maendeleo ya kidonda na ushauri.

(Picha na Freddy Maro)

Thursday, November 20, 2014

HOSPITALI YA AGA KHAN YATOA VIPIMO VYA BURE KWA WABUNGE DODOMA‏

Mbunge wa jimbo la Mbinga Magharibi John Komba akipimwa urefu kwenye viwanja vya Bunge na jopo la madaktari kutoka hospitali ya Aga Khan. Zaidi ya wabunge 200 pamoja na wafanyakazi wa bunge walipata semina ya afya pamoja kupima afya zao bure mwishoni mwa wiki kwenye zoezi ambalo liliongozwa na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Mh. Seif Rashid.


Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Mh. Margaret Sitta akichukuliwa damu kwa ajili ya vipimo na mshauri wa afya kutoka hospitali ya Aga Khan kwenye jengo la Bunge. Zaidi ya wabunge 200 pamoja na wafanyakazi wa bunge walipata semina ya afya pamoja kupima afya zao bure mwishoni mwa wiki kwenye zoezi ambalo liliongozwa na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Mh.Seif Rashid.

Waziri wa Ofisi ya Rais, Prof. Mark Mwandosya akijiandaa kupimwa urefu na mshauri wa afya kutoka hospitali ya Aga Khan kwenye jengo la Bunge. Zaidi ya wabunge 200 pamoja na wafanyakazi wa bunge walipata semina ya afya pamoja kupima afya zao bure mwishoni mwa wiki kwenye zoezi ambalo liliongozwa na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Mh.Seif Rashid.

NABO PHILIPO ASUSIWA WATOTO NA MKE WAKE MARIANA SILAYO ETI WANA KIFAFA


MAMA AWAKIMBIA WANAYE WENYE KIFAFA



Bw. Nabo Philipo aliyekimbiwa na mkewe.

HILI nalo ni tukio! Mwanaume mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Nabo Philipo ameibuka na kudai kuwa, mkewe Mariana Thomas Silayo (pichani) amekimbia nyumbani na kumwachia watoto wawili wenye ugonjwa wa kifafa.

Akizungumza kwa uchungu na gazeti hili hivi karibuni, Nabo alisema alifunga ndoa na Mariana mwaka 2002 na kujaliwa kupata watoto wawili, Madelin na Joyce Nabo na ndani ya miaka 13 ya ndoa waliishi kwa amani.


Mke wa Bw. Nabo Philipo, Mariana Thomas Silayo.

“Visa vilianza hivi karibuni baada ya mimi kupata hundi ya shilingi milioni 50 kupitia kazi zangu za ufundi wa kusuka mashine za magari, za kusaga na kukoboa na za matofari.“Nilimuonesha mke wangu hundi ili tupange tuzifanyie nini fedha hizo, lakini baada ya siku mbili hundi ikiwa benki kusubiri iwe tayari kutumika, nilianza kuumwa vitu visivyoeleweka na kuishiwa nguvu.


Mmoja wa watoto wa Bw. Nabo Philipo na mkewe, Mariana Thomas Silayo.

“Nilikimbizwa Hospitali ya Aga Khan (Dar) na kugundulika kuwa nilipewa sumu kwenye chakula.
“Nilimuuliza mke wangu ni nani atakuwa ameniwekea sumu akasema sijui. Siku nyingine nilimkuta ana dawa za ajabuajabu, nikamkalisha chini na kumsema aachane na habari za dawadawa.
“Nilishangaa sana kwani mambo mengi mke wangu alianza kuyafanya kuanzia hapo. Niligundua pia kwamba alikuwa akichukua nguo zake kidogokidogo na kuhamishia sehemu nyingine, ndipo siku moja akatoroka nyumbani moja kwa moja.


Mmoja wa watoto wa Bw. Nabo Philipo na mkewe, Mariana Thomas Silayo.

“Kinachoniuma ni kitendo cha kuniachia watoto wagonjwa, hasa huyu mdogo (Joyce) ambaye hushikwa na kifafa mara kwa mara, wakati mwingine humwangusha asubuhi na kumwachia jioni.
“Nilijaribu kumsihi mke wangu arudi kwa ajili ya watoto lakini kwake imekuwa ngumu. Nimeeleza haya ili jamii imfahamu ni mwanamke wa aina gani kwani hana huruma, maana nilishangaa hata alipoondoka watoto walifurahi,” alisema Nabo.

Mariana alipotafutwa ili kusikia kauli yake kufuatia madai hayo ya mumewe hakupatikana, waandishi wetu wanaendelea kumsaka.