Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Thursday, November 27, 2014

JE, VIDONDA VYA TUMBO VINATIBIKA?

watu wengi wanahangaika sana na tatizo la vidonda vya tumbo, pasipo kuwa na uhakika kama wanaweza kupona. Lakini leo tutaweza kujua maana ya vidonda vya tumbo (Ulcers), dalili zake, visababishi vyake na hata jinsi gani Watanzania waweze kujiepusha na maradhi hayo na tiba yake.


MAANA YA VIDONDA VYA TUMBO (ULCERS)

VIDONDA VYA TUMBO hotokea pale kuta za tumbo zinapotoa asidi iitwayo Hydrochrolic acid katika tumbo ambayo kazi yake ni kufanya mmeng’enyo wa chakula aina ya protein ndani ya tumbo, na ikumbukwe kwamba kuta za tumbo asili yake ni protein (protein in nature), na kwa maana hiyo basi kama kuta za tumbo zimeshatoa asidi hii katika tumbo kwa ajili ya mmeng’enyo wa chakula ndani ya tumbo na ikakuta ndani ya tumbo hakuna chakula cha kumeng’enywa basi mmeng’enyo huu huanza kufanyika katika kuta za tumbo na baadaye kuta zinakuwa zimelika hivyo kusababisha tatizo kubwa la vidonda hivyo.

Wataalamu wamegawanya vidonda vya tumbo katika makundi makubwa mawili, nayo ni;
Vidonda vya tumbo vinavyotokea tumboni (Gastric ulcers), hii ni ile hali ya kulika kwa kuta za tumbo, inapotokea hali hiyo huweza kuambatana na maumivu makali maeneo ya tumbo;

Vidonda vya tumbo vinavyotokea kwenye utumbo mwembamba (Duodenary ulcers), hii ni ile hali ya kulika kwa kuta za utumbo mwembamba ulio karibu na tumbo, na utumbo mwembamba unaweza kupata vidonda hadi inchi 11 kutoka sehemu inayopokelea chakula kutoka tumboni, na kwa maana hiyo maumivu huweza kusambaa hadi maeneo ya chini ya tumbo.

VISABABISHI
Kutokufuata ratiba nzuri ya chakula, kama mwanadamu anakua hapati chakula kwa wakati sahihi na anakaa muda mrefu bila kula, basi husababisha vidonda vya tumbo kwani kuta za tumbo zinapotengeneza asidi hii kwa ajili ya kumeng’enya chakula na wakati huo huo anakuwa hajapata chakula kwa muda mrefu basi mmeng’enyo huu huanza kufanyika kwenye kuta za tumbo na baadaye inaweza kusababisha vidonda hivyo.

Mawazo (stress), kwa mwanadamu anayekumbwa na msongo wa mawazo (stress) na wakati huo huo akawa hali vizuri, anaweza kukumbwa na maradhi hayo kwani husababisha kutengenezwa kwa Hydrochrolic acid ndani ya tumbo.

Kwa ushauri, vipimo na tiba dokta anapatikana kwenye vituo vyake vya Dar es Salaam, Tanga, Morogoro na Mwanza.Nawatakia afya iliyo njema kabisa.

Itaendelea wiki ijayo.

0 comments:

Post a Comment