Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Wednesday, November 26, 2014

JK APOKEA SALAMU ZA KHERI TOKA KWA RAIS BARACK OBAMA WA MAREKANI


Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mh.Liberata Mulamula akiwasilisha kwa Rais Dkt.Jakaya M rishoKikwete salamu za kumtakia kheri na afya njema kutoka kwa Rais wa Marekani Barack Obama jijini Baltimore, Maryland, Marekani.


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea kwa furaha na ujumbe kutoka Ubalozi wa Tanzania ulioko jijini Washington DC uliomtembelea kumjulia hali na kwasilisha salamu za Rais Barack Obama.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Balozi Liberata Mulamula na ujumbe wake wa maafisa waandamizi wa ubalozi wa Tanzania nchini Marekani baada ya kupokea salamu maalumu za kumtakia kheri na afya njema kutoka kwa Rais Barack Obama wa Marekani jijini Baltimore, Maryland, Marekani.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na maafisa waandamizi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani uliopo Washington D.C. wakati walipomtembelea mjini Baltimore Maryland ambapo balozi Liberata Mulamula aliwasilisha kwa Rais Kikwete Salamu maalum za kumtakia kheri na afya njema kutoka kwa Rais Barack Obama jijini Baltimore, Maryland, Marekani. Picha na Freddy Maro

0 comments:

Post a Comment