Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Wednesday, December 17, 2014

TAMBUA VIMBE MBALIMBALI KWA MWANAMKE NA JINSI YA KUZIONDOA PASIPO UPASUAJI



Leo tutazungumzia vimbe mbalimbali ambazo hutokea katika mwili wa mwanamke kwani wengi hawajui kama kizazi cha mwanamke kinaweza kutokewa na vimbe tofautitofauti katika maeneo tofauti kwa sababu vimbe zina vyanzo mbalimbali.

Jambo la msingi la kuzingatia leo ni kwamba aina zote hizi za vimbe tuna uwezo wa kuziondoa pasipo kufanya upasuaji.

AINA ZA VIMBE
Zipo aina tofautitofauti za vimbe katika mwili wa mwanamke, nazo ni kama;

VIMBE KATIKA MJI WA MIMBA {Uterus}
Vimbe hizi wataalamu wanaziita FIBROIDS au MAYOMA, na uvimbe huu hupatikana katika mji wa mimba iwe kwa juu au upande wa kushoto au upande wa kulia wa mji wa mimba. Na wanawake wengi sana wanakutwa na uvimbe kama huu.

VIMBE KATIKA VIFUKO VYA MAYAI YA UZAZI {Ovaries}
Katika vifuko vya mayai kunakua na vimbe za aina mbili, nazo ni kama;
Ovarian Cysts hii ni ile hali ya mwanamke kutokewa na uvimbe mmoja kwenye kifuko cha mayai ya uzazi, na kinaweza tokea upande mmoja au pande zote mbili za vifuko vya mayai, lakini vimbe hiyo inakua ni moja.

Polycystic ovarian syndromes {PCOS} au Multiple cysts na hizi ni zile vimbe ndogondogo nyingi zinazoweza kutokea kwenye kifuko cha mayai cha mwanamke, lakini nazo pia huweza kutokea katika pande zote mbili za vifuko vya mayai kwa mwanamke. Na hizi ndiyo vimbe kuu zilizokua zikitambulika kwa watu wengi sana lakini zipo nyingine nyingi sana.

KUVIMBA KWA MIRIJA YA UZAZI {Fallopian tubes}
Wataalamu wanaita salpingitise yaani kuvimba kwa mirija ya uzazi katika mwili wa mwanamke, na hii inawezekana ikatokea kwenye upande mmoja wa mrija wa uzazi na baadaye unaweza ukaambukiza mrija mwingine na yote ikawa imevimba, na hii nayo ni aina nyingine ya vimbe katika mwili wa mwanamke.

KUVIMBA KWA KIFUKO
CHA MAYAI {Ovary}
Wataalamu wanaita Ovary ties yaani kuvimba kwa kifuko chote cha mayai na hii inakua ni tofauti kidogo na uvimbe katika kifuko cha mayai au vimbe nyinginyingi ndogo katika kifuko cha mayai.

Kwa maana hiyo basi sote tutakuwa tumetambua aina mbalimbali za vimbe katika mwili wa mwanamke, na pale unapoambiwa una uvimbe au mke wako ana uvimbe katika mji wake wa uzazi basi ni bora kabisa ukauliza kuwa uvimbe huo ni wa aina gani ili iwe rahisi kuuondoa au kuutibia kwa haraka.

Na kama umeshawahi kupima na ukaambiwa kwamba una uvimbe katika mji wako wa mimba na hupendi kufanya upasuaji basi ni bora ukawasiliana nasi kupitia namba zetu.Kwa ushauri, vipimo na tiba dokta wetu anapatikana kwenye vituo vyake vya Dar es Salaam, Tanga, Morogoro na Mwanza.

Itaendelea wiki ijayo.

0 comments:

Post a Comment