Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Monday, May 18, 2015

MSANII BONGO MUVI ALIVYONUSA KIFO!

Mayasa Mariwata
Pole! Msanii wa sinema za Kibongo, Ummy Mohammed amenusa kifo baada ya kunusurika kwenye ajali ya Basi la Al-Saeed alilopanda akitokea mkoani Morogoro kwenda Dar ambapo ameumia mkono wa kushoto.


Msanii wa sinema za Kibongo, Ummy Mohammed akionekana na jeraha lake baada ya kunusurika katika ajali.

Akilisimulia Ijumaa Wikienda mkasa mzima, Ummy ambaye ni mwigizaji mkongwe aliyeibuka staa kwenye Sinema ya Mke Mchafu, alisema kuwa basi hilo liligongana na lori maeneo ya Mikese Morogoro na kupondeka.

Jeraha alilapata msanii wa sinema za kibongo baada ya kunusurika kwenye ajali likionekana kwa karibu.

Ummy alisema kilichosababisha ajali hiyo ni kutokana na mwendo kasi wa basi hilo ambapo abiria wengi walipata majeraha akiwemo yeye.

Basi ambalo alipata nalo ajali msanii wa sinema za kibongo Ummy Mohammed.

“Kwa jinsi ile ajali ilivyokuwa sikutegemea kabisa kama ningenusurika kifo, nilikuwa nasali sala ya mwisho, namshukuru Mungu nimeambulia jeraha la mkono japokuwa ninapata maumivu makali ya mwili,” alisema Ummy.

0 comments:

Post a Comment