Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Monday, May 4, 2015

MTOTO WA FAMILIA YA KIFALME UINGEREZA ATOLEWA HOSPITALI

MTOTO wa kike katika familia ya kifalme ya Uingereza ya Prince William na Kate Middleton aliyezaliwa jana ametolewa hospitali na kupelekwa nyumbani kwenye Ikulu ya Kensington.

Mtoto huyo wa kike ambaye ni wa pili katika familia hiyo alizaliwa jana Jumamosi katika Hospitali ya St Mary jijini London.

Familia hiyo mpaka sasa bado haijaamua mtoto huyo apewe jina gani.

Mtoto huyo ataendelea kubaki katika Ikulu ya Kensington ambapo leo anatarajiwa kutembelewa na Malkia wa Uingereza, Prince Charles na familia ya Kate.


Mtoto wa kike wa Prince William na Kate Middleton aliyezaliwa jana.

Prince William na Kate Middleton wakiwa wamembeba binti yao.

Prince William na Kate Middleton wakitoka Hospitali ya St Mary jijini London.

Prince William na Kate Middleton wakiwaaga watu waliofika hospitali wakati wakielekea Ikulu ya Kensington.

Prince William akiwa amembeba mtoto wao wa kwanza, Prince George eneo hilo la hospitali.

Bado haijafahamika ni jina gani atapewa mtoto huyu.

0 comments:

Post a Comment