Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Monday, May 4, 2015

ESTER: JAMANI MASTAA ACHENI KUIBA WAUME ZA WATU!

Gladness Mallya
Funguka! Mwanadada mwenye mvuto wa aina yake katika kiwanda cha filamu Bongo, Ester Kiama ameibuka na kuwachana mastaa wa kike wanaopenda kuiba waume za watu kwamba waache kwani si tabia nzuri.


Ester Kiama.

Akizungumza na Ijumaa Wikienda, Ester alifunguka kuwa mastaa wanaochukua waume za watu, tabia zao siyo nzuri na kibaya zaidi wakishawachukua wanajigamba ili watu wawaone wako juu mjini wakati hawana lolote.

“Siyo kwamba sijawahi kuwa na mume wa mtu, nilishawahi lakini nimetokea kuwachukia sana kwani hawana faida zaidi ya kuwapotezea wasichana muda wao, nimejifunza mengi na sitarudia tena hivyo nawasihi wenzangu waache kuiba waume za watu kwani watarogwa tu,” alisema Ester.

0 comments:

Post a Comment