Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Wednesday, March 25, 2015

NDEGE YA UJERUMANI YAANGUKA IKIWA NA WATU 150

Ndege ya shirika la ndege la Germanwing inayofanana na ile iliyoanguka.

NDEGE ya abiria inayomilikiwa na shirika la ndege la Germanwing Airbus A320 imeanguka katika milima ya Alps nchini Ufaransa.

Mchoro ukionyesha eneo ambalo ndege hiyo ilipoteza mawasiliano na rada.

Ndege hiyo ilikuwa imebeba abiria 142 na wahudumu sita ikitokea jijini Barcelona nchini Uhispania kuelekea Duesseldorf, Ujerumani.


Ubao wa kuonyesha ndege zilizowasili kwenye uwanja wa ndege wa Duesseldorf, Ujerumani.

Ndege hiyo inayomilikiwa na shirika la ndege la Ujerumani Lufthansa chini ya nembo Germanwings imeripotiwa kuanguka katikati ya Barcelonnette na Digne.

Rais wa Ufaransa amesema: "Mazingira ya ajali hiyo ambayo bado hayajawekwa bayana, yanawapa wasiwasi kufikiri kama kuna mtu yeyote aliyenusurika"

0 comments:

Post a Comment