Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Saturday, April 25, 2015

ZARI AONYWA VIATU VIREFU NA UJAUZITO

MWANDISHI WETU

UBAVU wa Nasibu Abdul ‘Diamond’, Zarinah Hassan ‘Zari’ ameonywa kuacha viatu virefu kutokana na ujauzito alionao.
Kwa mujibu wa daktari mmoja ambaye hakupenda jina lake lichorwe gazetini, alisema kama anataka kujifungua salama basi ahakikishe anaachana na suala la kuvaa viatu virefu kwa wakati huu ambao ni mjamzito.


Ubavu wa Nasibu Abdul ‘Diamond’, Zarinah Hassan ‘Zari’.

“Kama anajipenda na anampenda mwanaye ajaye, anapaswa kuachana na mambo ya viatu virefu kwa sasa hadi pale atakapojifungua,” alisema daktari huyo.Katika picha za hivi karibuni ambazo Zari amepigwa, tumbo lake linaonesha kwamba tayari mimba yake ni kubwa na yuko mbioni kuelekea kujifungua.

0 comments:

Post a Comment