Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Wednesday, April 8, 2015

MAMA KANUMBA AONGOZA IBADA FUPI MAKABURINI KUMKUMBUKA MWANAYE STEVEN KANUMBA


Mama Kanumba akionesha uso wa huzuni baada ya kufika makaburini kwa ajili ya kumkumbuka mtoto wake marehemu, Steven Kanumba.
Mama Kanumba akiwasha mshumaa kama ishara ya kumbukumbu ya mwanaye.
Ndugu wa mama Kanumba wakiwasha mishumaa.
Mama Kanumba akiongoza ibada fupi ya kumwombea marehemu mwanaye.
Ibada ikiendelea
Kijana aliyekuwa shabiki wa Marehemu Kanumba akiomba, kama ishara ya kumbukumbu yake.

MAMA mzazi wa aliyekuwa msanii nguli wa filamu Bongo Marehemu Steven Charles Kanumba leo mchana aliongoza ibada fupi kama ishara ya kumbukumbu ya kifo cha mwanaye kilichotokea miaka mitatu iliyopita, shughuli iliyofanyika katika makaburi ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam.

Katika hafla hiyo fupi, mama Kanumba akiwa pamoja na ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu, waliwasha mishumaa baada ya kufanya usafi wa eneo la kaburi lake, kumkumbuka nyota huyo aliyefariki Aprili 7 mwaka 2012.

0 comments:

Post a Comment