Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Friday, February 27, 2015

CHID BENZ: ATOZWA FAINI, AAHIDI KUACHA MADAWA YA KULEVYA



Chid Benz (mwenye shati jeupe) baada ya kuachiwa na mahakama.

…Akiondoka mahakamani.

…Akielekea kwenye gari lililomleta.

MWANAMUZIKI
wa Bongo Fleva, Rashidi Makwilo maarufu kama ‘Chid Benz’, aliyekuwa
anatuhumiwa kwa kukutwa na dawa za kulevya aina ya heroin na bangi, leo
ameachiliwa huru kwa kulipa faini ya Sh. 900,000.

Katika
maelezo ya awali yaliyosomwa na mwendesha mashtaki wa Jamhuri Diana
Lukendo, mbele ya Hakimu Warialwande Lema, msanii huyo alimwambia
hakimu kuwa mshtakiwa alikamatwa na dawa hizo za kulevya akiwa Uwanja
wa Ndege wa Kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere, akitaka kusafiri
kuelekea mkoani Mbeya.

Hata hivyo mshtakiwa huyo ambaye alikiri
kosa mnano tarehe 18 Aprili mwaka huu, leo aliiomba mahakama
kumpunguzia adhabu na kwamba asingetumia tena ulevi huo na
atawaelimisha vijana wenzake juu ya madhara yake.

0 comments:

Post a Comment