Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Thursday, January 22, 2015

TATIZO LA NYAMA KUJITOKEZA NJIA YA HAJA KUBWA {HEMORRHOID}

Wiki iliyopita tuliweza kuona nini maana kubwa ya tatizo hili la kutokwa na kijinyama katika sehemu au maeneo ya haja kubwa na leo tutaweza kuona basi vyanzo au visababishi hasa vya tatizo hili kwa mwanadamu.

VISABABISHI
Sasa wataalamu bado hawajawa na majibu kamili kuhusiana na tatizo hili la kutokwa na kijinyama katika maeneo ya haja kubwa husababishwa na kitu gani hasa lakini wameweza kutoa baadhi ya vitu ambavyo vinaaminika kwa kiwango kikubwa sana husababisha hali hii kujitokeza kwa mwanadamu, na vitu hivyo basi ni kama vifuatayo;

Kupata choo kigumu kupita kiasi kwa mwanadamu wataalamu wanaita constipation mara nyingi imekuwa ni chanzo kikubwa sana cha tatizo hili la mtu kutokwa na kinyama katika maeneo ya haja kubwa na kuna uwezekano ikawa ni bawasili ya ndani au ya nje yenye kuonekana, kwa hiyo kama mtu anakumbwa na hali ya kupata choo kigumu basi kunauwezekano mkubwa sana mtu huyo akasumbuliwa na tatizo hili la bawasili.

Hali ya kuharisha sana {heavy diarrhea}, kwa mtu ambaye anapatwa na hali ya kuharisha kwa muda mrefu basi naye pia anauwezekano mkubwa sana wa kukumbwa na tatizo hili la kutokwa na kijinyama katika maeneo ya haja kubwa au bawasili {hemorrhoid}.

Kukosekana kwa baadhi ya vyakula, kuna baadhi ya vyakula vinapokosekana katika mwili wa mwanadamu au visipotumika sana kwa mtu huweza kusababisha mtu kupata choo
kigumu kupita kiasi na kama anapatwa na hali hii basi kunauwezekano mkubwa sana mtu huyo akakumbwa na tatizo la bawasili na vyakula hivyo ni mboga za majani na matunda kwa wingi ndani ya mwili.

Hali ya ujauzito kwa akina mama, hii pia imekuwa ni sababu kubwa sana inayosababisha suala zima la kutokwa na kijinyama maeneo ya haja kubwa na hii ni kwa sababu hali ya ujauzito kwa mama husababisha kukua au kuongezeka kwa mji wa mimba ambao hutumika hasa kumuhifadhi mtoto na kwa sababu hii basi inaweza kusababisha vascular structure au vijinyama katika maeneo ya haja kubwa kwa mama kuongezeka ukubwa na hivyo basi kuwa ni tatizo,

lakini mara nyingi mwanamke akishajifungua kunauwezekano kikapotea lakini kama kinabaki basi ni vema kufika katika vituo vya afya kwa ajili ya matibabu zaidi.Kukaa kwa muda mrefu, hali ya kukaa kwa muda mrefu kwa mwanadamu nayo pia imekuwa ni kisababishi kikubwa sana cha tatizo kubwa la tumbo kujaa gesi na kupata choo kigumu kupita kiasi {constipation}.

Mara nyingi watu wanaokumbwa na shida hii kunauwezekano mkubwa sana wa kutokwa na kinyama au bawasili, hasa kwa wanaotumia sana vyoo vya kukaa na kufanya hivyo kwa muda mrefu.
Hali ya wanadamu kunyanyua vitu vizito kupita kiasi kwa mwanadamu na ikawa ni zoezi endelevu kwa muda basi hali hii inaweza sababisha mtu kupatwa na tatizo la kutokwa na kijinyama au bawasili.
Itaendelea wiki ijayo.

, na hata kwa mtu anaefanya kazi mgumu sana pia kunauwezekano akakutwa na tatizo hili.
Na pia kunasababu ya kurithi, hali hii ya ya kutokwa na kijinyama kwa upande mwingine wataalamu wametoa sababu ya kwamba inakua ni hali ya kurithi kutoka kizazi kimoja kwenda kizazi kingine {genetic}, na ni vema kulitibia pale tu linapojitokeza.

Na kama unapatwa na hali kama hiyo basi na wewe pia unaweza wasiliana nasi kupitia namba zetu kwa ajili ya ushauri na tiba zaidi. Kwa ushauri, vipimo na tiba dokta anapatikana kwenye vituo vyake vya Dar es Salaam, Tanga, Morogoro na Mwanza.Nawatakia afya iliyo njema kabisa.
Itaendelea wiki ijayo. Asante.

0 comments:

Post a Comment