Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Saturday, January 17, 2015

MTI WA AJABU WAGUNDULIKA MBEYA, UNADAIWA KUGAWA UTAJIRI



Wananchi wa kijiji cha Ijoka, Mkoani Mbeya wameingia kwenye imani za kishirikina baada ya kuandamana na kwenda kupasua mti ulianguka ambao wanadai una utajiri ndani yake.Wakazi hao walisema walielezwa na mganga wa jadi kutoka Malawi Peter Lungola, kuwa mti huo ukitumiwa vyema utaleta utajiri.Mganga huyo alifika kijijini humo miaka 20 iliyopita na kuwaeleza kuwa amti huo una asili kubwa ya utajiri na kuwa chini ya mti huo kuna nyumba za kifahari zilizojaa hazina kubwa ya fedha.Inasemekana mti huo ulianguka wiki iliyopita na kuanza kupumua kitendo kilichowashangaza wengi. Wazee wa kijiji hicho walishangazwa na hatua ya baadhi ya watu kula majani ya mti huo huku wengine wakichukua magome yake na kuyahifadhi majumbani mwao.

0 comments:

Post a Comment