Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Saturday, January 17, 2015

SITTI MTEMVU ATEMBELEA KITUO CHA WENYE ULEMAVU WA NGOZI HOSPITALI YA MKOA ILALA


Mbunge wa Jimbo la Ilala Mhe Mussa Azzan Zungu akiongea na Waandishi wa Habari ( pichani hawapo) mara baada ya kupokea vifaa mbalimbali vya kuhifadhia taka na Sabuni.


Mwenyekiti wa Sitti Tanzania Faundation, Sitti Mtemvu (wa tatu kulia) akimkabidhi vifaa vya kuhifadhia taka Mbunge wa Jimbo la Ilala Mhe. Mussa Azzan Zungu (kushoto), kwa ajili ya Hospitali ya Mkoa wa Ilala Dar es Salam. kuanzia kushoto nyuma ya mbunge ni Diwani wa kata ya Kinyerezi kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Leah Mgitu katikati ni mama mzazi wa Sitti Mariam Mtemvu, wa kwanza kulia ni Diwani wa Kata ya Ilala kupitia Chama cha Mapinduzi Edson Fungo na anaefuatia ni Daktari Kiongozi wa Hospitali ya Mkoa Ilala
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Under The Sun Tanzania Bi. Vicky Ntetema (kulia) , akifafanua jambo wakati Mwenyekiti huyo alipotembelea kituo hicho

Afisa utetezi Bw. Kondo Seif (wa kwanza kushoto) akitolea maelezo ya ukosefu wa rangi asili mwilini ambayo huathiri ngozi, macho na nywele na kukosekana kwa melani mwilini, akisema miongoni mwa athari zake ni wepesi wa kuungua na jua unapotembea juani na ufanyapo kazi juani.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Under The Sun Tanzania Vicky Ntetema (kulia) akimuonyesha Mwenyekiti wa Sitti Tanzania Foundation, Sitti Mtemvu (kushoto) Picha ya mtoto alie tekwa akiwa mgongoni mwa mama yake. Wa pili kushoto ni Mama mzazi wa Sitti.

0 comments:

Post a Comment