Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Friday, September 26, 2014

JINSI YA KUZIONDOA VIMBE MBALIMBALI KATIKA MWILI WA MWANAMKE PASIPO KUFANYA UPASUAJI




Wiki iliyopita tulizitazama aina za vimbe, tuliishia katika kipengele cha pili kilichosema:
Fibroids au Mayoma:Hizi ni vimbe zinazotokea katika mji wa mimba na hizi ndizo vimbe zinazowasumbua watu wengi sana katika jamii yetu ya sasa, na dalili zake ni kama;

Hapa mwanamke hupatwa na maumivu chini ya kitovu lakini ni katikati siyo upande wa kulia wala upande wa kushoto na mara nyingi maumivu haya huambatana na maumivu ya kiuno, maumivu ya mgongo na maumivu hayo huenda hadi sehemu za mapaja na kushuka hadi miguuni na maumivu haya huwa makali sana hasa wakati wa hedhi. Sasa ukiona unaandamwa na dalili hizi basi ujue kuna uwezekano ukawa na Fibroids au Mayoma.

Kuongezeka kwa ukubwa wa tumbo, mwanamke ukiona tumbo linaongezeka ukubwa na unasikia kama kuna kitu kinatembea ndani ya tumbo, wakati huohuo unaandamwa na maumivu makali chini ya kitovu kwa katikati na maumivu makali sana wakati wa hedhi basi ni dalili kubwa sana nawe ukawa na Fibroids au Mayoma.
SASA ENDELEA…

Polycystic ovarian syndromes {PCOS} au Multiple cysts: Hizi ni zile vimbe ndogondogo nyingi zinazoweza kutokea kwenye kifuko cha mayai cha mwanamke, lakini nazo pia huweza kutokea katika pande zote mbili za vifuko vya mayai kwa mwanamke. Nazo zina dalili zake mbalimbali, nazo ni kama;

Hapa napo tunapata dalili tofauti, ya kwanza ni mwanamke kuwa na vinyweleo vingi sana katika mwili wake hasa kwenye mikono au kwenye miguu au anakuwa na ndevu au kifuani (garden love) na hii ni kwa sababu mwanamke huyu anakuwa na hormone nyingi sana za androgen yaani anakuwa na hormone nyingi za kiume, basi ukiona dalili kama hizo ni vema kuwahi hospitali.

Pia kuna hali ya kuvurugika hedhi ya mwanamke na kuwa haieleweki na kuwa na maumivu ya kiuno upande wa kulia au wa kushoto nayo pia inakuwa ni dalili kubwa sana ya PCOS au Multiple cysts hivyo ni vema kuchukua hatua za haraka.

Pia hali ya kutokwa na uchafu sehemu za siri kwa mwanamke ni moja ya dalili, na hasa uchafu huo unapokuwa hauna harufu wala hauwashi basi ujue kuwa kuna uwezekano mkubwa nawe ukawa na PCOS au Multiple cysts.

Hydrosulpinx:Hii ni ile hali ya mwanamke kujaa maji katika mirija yake ya kizazi na mirija hiyo inakuwa haipitishi mayai ya uzazi.

Dalili yake kubwa ni kuwa na maumivu makali sana kwenye kiuno ambayo huweza kutokea upande mmoja au yakatokea pande zote mbili na huenda hata maumivu yanayotokea upande, yote haya yanaisha bila kufanya upasuaji.

Dalili zipo nyingi sana na tukianza kuziongelea zote basi zinaweza kuchukua hata mwezi. Lakini tutaishia hapo kwa sasa na wiki ijayo tutaendelea na kuona Vyanzo vya Vimbe Katika Mwili wa Mwanamke.
Kama umeshawahi kupima na ukaambiwa kwamba una uvimbe katika mji wako wa mimba na hupendi kufanya upasuaji basi ni bora ukawasiliana nasi kupitia namba zetu.

Kwa ushauri, vipimo na tiba dokta wetu anapatikana kwenye vituo vyake vya Dar es Salaam, Tanga, Morogoro na Mwanza.

Itaendelea wiki ijayo.

0 comments:

Post a Comment