Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Tuesday, September 16, 2014

KUPITIA THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC ZIFAHAMU FAIDA ZA KULA LIMAO

Limau lina manufaa chungu nzima kama vile kutuliza, kutibu, kupunguza sumu mwilini n.k.

Shinizo la Mawazo:
Huondoa uchovu wa akili, kisunzi, na pia wasiwasi. Limau lina uwezo wa kutuliza akili kwa kuondoa mawazo. Aidha unapumua harufu ya limau unaweza kujiongezea umakinifu.

Usingizi:
Utumiaji wa limau husaidia kumpa mtu usingizi na kuepusha tatizo la kupata usingizi.

Mfumo wa Kinga:
Limau lina kiwango kikubwa cha Vitamini kwa hivyo ni zuri kwa kuimarisha kinga mwilini, kwa kuzipa nguvu chembechembe nyeupe za damu, na kuimarisha mzunguko wa damu mwilini.

Homa:
Linaweza kutumika kuponya maradhi ya kuambukiza kama homa, malaria na homa ya matumbo.

Matatizo ya Tumbo:
Hutibu maradhi tofauti ya tumbo kama shida za usagaji chakula, , maumivu ya tumbo, na mshipa.

Kupunguza Uzani:
Hutumika na wengi kupunguza Uzani.

Pumu:
Inaaminika kwamba limau linasaidia kutibu pumu.

Nywele:
Aidha limau hutumiwa kwa utunzaji nywele. Limau huzifanya nywele kuwa na afya na za kuvutia, na huondoa uyabisi.

Ngozi:
Limau hutumiwa kutunza ngozi, kwa kuipa afya. Hutibu vidodosi na mba.

0 comments:

Post a Comment