Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Tuesday, August 12, 2014

SABABU ZA MWANAMME KUOTA MATITI KAMA MWANAMKE (GYNAECOMASTIA)

Ni jambo la kawaida kwa mwanamke kuota matiti anapokuwa amefikisha umri wa kupevuka, lakini jambo hili linapotokea kwa mwanamme inakuwa ni kitu kisichokuwa cha kawaida. Ukuaji au uotaji wa matiti kwa mwanamme na kuwa kama ya mwanamke kitaalamu huitwa Gynaecomastia.
MWANAMME KUOTA MATITI
Kwa miaka ya zamani umri wa kupevuka na kuanza kuonekana mabadiliko katika mwili ilikuwa ni kuanzia miaka 17 au 18, lakini kwa miaka ya hivi karibuni kumetokea mabadiliko makubwa sana katika staili za maisha tunazoishi pamoja na mapinduzi makubwa katika sayansi na teknolojia na hivyo hata miili yetu inapata athari kwa kile ambacho tunaupatia kama chakula, dawa, vinyaji na vinginevyo. Hivi leo mabadiliko tuliyotegemea awe nayo mtu mwenye umri wa miaka 18, unayaona kwa mtoto wa miaka 12.
Katika ukuaji wa mwili wa binadamu, ufanyaji kazi wa viungo mbalimbali katika mwili pamoja na tabia za kijinsia anazokuwa nazo mtu, vyote hivi hutawaliwa na kemikali asilia zinazopatikana ndani ya miili yetu ambazo kwa kisayansi hujulikana kama hormones.
Tukibaki upande wa mada yetu, Gynaecomastia, kemikali hizi (hormones) ndizo zinazomfanya mtu awe na tabia za kike au tabia za kiume. Kwa kawaida mwili wa mwanadamu unazo homoni zote, yaani mwanamke anazo homoni za kike na pia anazo za kiume, pia mwanamme anazo homoni za kiume na pia homoni za kike.
Kinachomfanya mtu awe na tabia za kike ni kwa kuwa homoni za kike ni nyingi kuliko za kiume, na kinachomfanya mtu awe na tabia za kiume ni kwa kuwa homoni zake za kiume ni nyingi kuliko zile za kike.
Mabadiliko yanapotokea katika mwili wa mtu juu ya hizi homoni za kike (Estrogens) na zile za kiume (Androgens) ndipo tunapoyaona mabadiliko au tabia ambazo hazijazoeleka kuonekana kwa mtu wa jinsia fulani.
Mwanamme kuota matiti, gynaecomastia husababishwa na mabadiliko katika homoni zake ambapo homoni za kike (Estrogens) zimeongezeka na kuzifanya zile za kiume (Androgens) kuwa kwa kiwango kidogo mwilini mwake na hivyo kupelekea hata mwili wake uwe na mabadiliko anayopaswa kuwa nayo mwanamke (kuota matiti).
Miongoni mwa vitu vinavyo sababisha mwanamme awe na matiti kama ya mwanamke ni kama vile:
Matumizi ya dawa – baadhi ya dawa zinazotumika katika tiba mbalimbali huchangia mwanamme kuota matiti, mfano baadhi ya dawa zinazotumika katika tiba ya vidonda vya tumbo, tiba za magonjwa ya moyo na tiba za vijidudu vinavyosababisha UKIMWI.
Matumizi ya vipodozi – baadhi ya vipodozi vinavyotumika huwa na mchanganyiko unaofanya uwiano wa homoni katika mwili ubadilike, mfano vipodozi vilivyo na mchanganyiko wa , (tea trea oil pamoja na lavender oil), michanganyiko hii pia huwa katika baadhi ya sabuni, losheni na shampoo.
Vyakula – mapinduzi katika sayansi pia yamechangia kuwe na aina mbalimbali ya uandaaji au uzalishaji wa chakula ambapo baadhi ya vyakula vinakuwa na michanganyiko inayo badili uwiano wa homoni katika mwili wa binadamu, mfano ni baadhi ya vyakula vilivyozalishwa kwa tekinolojia za baiolojia (Genetic Modified Organisms ) au kwa kifupi GMOs.
Ili tuweze kupambana na hali hii, gynaecomastia, ni vyema tukawa waangalifu katika vyakula, vinywaji na vipodozi tunavyotumia pia tuzingatie ushauri tunaopewa na wataalamu wa afya juu ya mambo mbalimbali yanayohusu afya zetu pamoja na matumizi sahihi ya dawa tunazozitumia katika kutibu matatizo ya kiafya.

0 comments:

Post a Comment