Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Wednesday, August 27, 2014

EBOLA BADO TISHIO AFRIKA MAGHARIBI




TAARIFA iliyotolewa hivi karibuni na Shirika la Afya Duniani (WHO), inaonyesha jinsi gonjwa hatari la Ebola linavyozidi kuangamiza wananchi katika eneo hilo.
Agosti 22 mwaka huu, WHO walitoa taarifa kuwa, jumla ya wagonjwa walioripotiwa kuwa na Ebola ni 2,615 kwenye nchi nne za Afrika Magharibi ambapo kati yao 1,427 wamepoteza maisha kwa ugonjwa huo.
Nchini Liberia ambapo ugonjwa huo ulianzia, wagonjwa 1,082 wameripotiwa kuwa nao, huku 624 kati yao wakifariki dunia.
Guinea, 607 wamethibitishwa kuwa na Ebola, huku 406 kati yao wakiwa wamepoteza maisha.
Sierra Leone, watu 392 wameripotiwa kufariki kwa ugonjwa huo na nchini Nigeria, watu watano wamepoteza maisha kwa Ebola kati ya 13 walioripotiwa kuwa na ugonjwa huo.

0 comments:

Post a Comment