Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Friday, May 2, 2014

UGONJWA WA KASWENDE UNAVYOSUMBUA WATU WENGI DUNIANI..NINI CHA KUFANYA KUONDOKANA NA UGONJWA HUU?

Kaswende ni ugonjwa wa zinaa unaosababishwa na bakteria ya spirochete Treponema pallidum baadhi ya spishi pallidum. Njia ya kawaida zaidi ya kuambukizwa ni kupitia kufanya ngono; hata hivyo, kaswende pia inaweza kuambukizwa kutoka kwa mama hadi kwa fetasi wakati wa ujauzito au wakati wa kuzaliwa kwa mtoto, na kusababisha kuzaliwa na kaswende. Magonjwa mengine ya binadamu yanayohusiana niTreponema pallidumbakteria inajumusiha buba (baadhi ya spishi pertenue), pinta (baadhi ya spishi carateum) na bejel (baadhi ya spishi endemicum).

Dalili na ishara za kaswende hutofautiana kulingana na hatua iliyoko kati ya hatua nne. Hatua ni ya kwanza, ya pili, fiche, na ya mwisho. Hatua ya kwanza kawaida inajitokeza kimoja na shanka utokeaji wa kidonda kwa ngozi isiyowasha, ngumu, isiyokuwa na uchungu). Hatua ya pili ya kaswende hujitokeza na upele ambayo mara kwa mara inahusisha viganja vya mikono na nyayo za miguu. Hatua fiche ya kaswende hujitokeza na dalili kiasi au hata bila. Hatua ya mwisho ya kaswende hujitokeza na guma, dalili zinazohusiana na mfumo wa neva, au zinazohusiana na moyo.

Hata hivyo, kaswende imeitwa "mwiigaji mkuu" sababu mara nyingi hujitokeza kwa njia isiyo ya kawaida.
(Bonyeza hapa kuangalia picha sehemu ya uume iliyoathirika. Uwe na umri wa miaka zaidi 18)

Kwa kawaida kaswende hutambulika kwa uchunguzi wa damu;hata hivyo, bakteria inaweza kuonekana kwa kutumia hadubini. Kaswende inaweza kutibiwa kwa njia inayofaa kwa kutumia antibiotiki, haswa ndani ya misuli penisilini G. Hii inapendekezwa kwa watu walio na aleji ya penisilini, seftriaksoni. Inaaminika kwamba kufikia mwaka wa 1999 watu milioni 12 walikuwa wameambukizwa kaswende ulimwenguni na zaidi ya asilimia 90 ya hali hizi kutoka kwa nchi zinazoendelea. Hali za kaswende zilipungua kwa kasi baada ya penisilini kupatikana kwa urahisi katika miaka ya 1940, lakini viwango vya maambukizi vimeongezeka tangu mwaka 2000 katika nchi nyingi. Mara nyingi kaswende hupatikana pamoja na virusi vinavyosababisha UKIMWI (VVU). Hii imehusishwa na sehemu ya matendo ya ngono yasiyokuwa salama kati ya wanaume wanaofanya ngono na wanaume wengine;Ongezeka la uasherati; ukahaba; na kupungua kwa matumizi ya kondomu


Dalili na ishara
Kaswende inaweza kuwa katika hatua moja kati ya hatua nne tofauti: ya kwanza, ya pili, fiche, na ya mwisho,[4] na pia inaweza kujitokeza wakati wa kuzaliwa.[5] ilirejelewa kama "mwiigaji mkuu" na Sir William Osler kutokana na njia mbalimbali inavyojitokeza[4][6]
Hatua ya kwanza

Hatua ya kwanza shanka ya kaswende kwa mkono

Hatua ya kwanza ya kaswende kawaida hupatikana kwa kuwasiliana kwa njia ya moja kwa moja kwa ngono na vidonda vilivyoambukizwa vya mtu mwingine.[7]Takriban siku 3 hadi 90 baada ya kuathiriwa hapo awali ( wastani ya siku 21 ) kidonda kwa ngozi, iitwayo shanka, hutokea mahali palipogusana.[4] Huu ni mfano hasa (Asilimia 40 ya wakati) kidonda kimoja, kigumu, kisichokuwa na uchungu, kisichowasha na sehemu yake ya chini iliyokuwa safi na mipaka mikali kati ya sentimita 0.3 na 3.0 kwa ukubwa .[4] Hata hivyo, kidonda, kinaweza kuonekana kuwa tofauti sana. [8] Katika viwango, hugeuka kutokamacule hadi kipelena kisha kwa uyeyukaji au donda.[8] Mara chache, kutakuwa na vidonda kadhaa. (~40%),[4] Hii pia ni ya kawaida mtu anapoambukizwa Virusi Vya Ukimwi

Shanka yanaweza kuwa na uchungu au nyororo (30%), na zinaweza kutokea nje viungo vya uzazi (2–7%). Mahali pa kawaida zaidi pa chanikeri kwa wanawake ni kwa seviksi(44%). Mahali pa kawaida zaidi kwa wanaume wanaovutiwa na jinsia tofauti ni Kwa uume (99%). Wakati mwingine shanka hutokea kwa tupu ya nyama au rektamu kwawanaume wanaojishirikisha ngono na wanaume wengine (34%).[8]Tenzi kuvimba mara kwa mara (80%)hutokea pahali palipo ambukizwa,[4] hutokea siku 7 hadi 10 baada ya kutokea kwa shanka[8]kidonda kinaweza kuendelea kutokea wiki watatu hadi sita bila matibabu[4]
Hatua ya pili


 Mfano hasa unaojitokeza kwa hatua ya pili ya kaswende na upele kwa viganja vya mikono


Nyekundu vipele na vipele kuzidi mwilini kutokana na hatua ya pili ya kaswende

Hatua ya pili ya kaswende hutokea takriban wiki nne hadi kumi baada ya hatua ya kwanza ya maambukizi.[4] hatua ya pili ya ugonjwa unaweza kujitokeza kwa njia nyingi tofauti, lakini kwa kawaida dalili sana sana huhusisha ngozi, membreni ute, na tezi ya limfu.[9] kunaweza kuwa na upele mwekundu-waridi-isiyokuwa na mwasho kwa kiwiliwili pamoja na limbu (miguu na mikono), ikiwa ni pamoja na viganja na nyayo.[4][10] Vipele vinaweza kuwa makulopapula au yenye pustuli. inaweza kutengeneza chunjua kama vidonda iliyopana, nyeupe na sawa sawa inayojulikana kama kondiloma latum kwa membreni yenye utes. Vidonda hivi vyote vinamaambukizi na yanahifadhi bakteria. Dalili zingine inaweza ni pamoja na homa, uchungu wa koo, hitilafu ya mwili,kupunguza uzito, kutokwa na nywele, na maumivu ya kichwa.[4] matokeo yasiyo kuwa ya kawaida ni pamoja na hepatitisi, figo ugonjwa, athritisi,periostitisi, neuritsi ya kuona, uveitisi, na keratitisi ya interstitial.[4][11]

Kwa kawaida dalili kali uyeyuka baadaye kati ya wiki tatu hadi sita;[11] hata hivyo, katika hali iliyokaribia 25%, dalili ya hatua ya pili yanaweza kurudi. Watu wengi walio katika hatua ya pili ya kaswende (40–85% ya wanawake, 20–65% ya wanaume) hawatoi ripoti kuwa na shanka ya kiwango kilicho juu cha hatua ya kwanza ya kaswende.[9]
Hatua fiche

Hatua fiche ya kaswende imefafanuliwa kama kuwa na serologic utambuzi wa maambukizi bila dalili ya magonjwa.[7] Imeelezwa zaidi kama ya hapo awali (chini ya mwaka wa 1 mwaka mmoja baada ya hatua ya pili ya kaswende) katika Marekani[11] Uingerezani, masaa hizi huitwa miaka miwili ya hatua fiche ya kaswende ya mapema na iliyochelewa.[8] Dalili ya hatua fiche ya kaswende ya mapema huweza kurudi tena. Hatua fiche ya kaswende iliyochelewa huwa haina dalili za magonjwa (hayana dalili), na hatua fiche ya kaswende iliyochelewa haiambukizwi kwa urahisi kama hatua fiche ya kaswende ya mapema.[11]
Hatua ya mwisho

Hatua ya mwisho ya kaswende inaweza kutokea takriban miaka mitatu hadi 15 baada ya maambukizi ya kwanza, na inaweza kugawanywa kwa aina tatu tofauti: kaswende iliyosababishwa na guma (15%), iliyochelewa kaswende katika mfumo wa neva (6.5%), na kaswende inayoathiri moyo na mishipa ya damu (10%).[4][11] Bila matibabu, theluthi moja ya watu ambao wameambukizwa kaswende hupata hatua ya mwisho ya kaswende.[11] Watu walio na awamu ya mwisho ya kaswende hawawezi kuambukiza wengine.[4]

Kaswende inayosababishwa na gum, pia inayoitwa hafifu kaswende, kwa kawaida hutokea moja kwa miaka 46 baada ya maambukizi ya awali, kwa wastani wa miaka.15 Hatua hii ni sifa ya muundo sugu wa guma, ambayo ni uvimbe nyororo zinazofanana na vidonge vya inflamesheni vinavyoweza kuwa zinabadilika kulingana na ukubwa. Kawaida huathiri ngozi, mifupa, na ini, lakini inaweza kutokea mahali popote.[4]

Kaswende katika mfumo wa neva inamaanisha maambukizi inayohusisha mfumo mkuu wa neva. Unaweza kutokea mapema, ikiwa aidha isiyo kuwa na dalili ya ugonjwa au ya kusababisha kaswende meninjitisi; au inaweza kuchelewa, kama kaswende ya veni za tando za ubongo, paresi ya jumla, au tabesi dorsalisi, ambayo inahusu usawa wa mwili na uchungu mkali kwa limbu za chini. Kaswende ya neva iliyochelewa huja kabisa baada ya miaka minne hadi 25 baada ya maambukizi ya hapo awali. Kaswende ya veni za utando za ubongo hufanana hasa ikiwa haiwezi kuzuiliwa kifafa, na paresi ya jumla hufanana hasa na dimenshia na tabtesi dorsalisi.[4] Pia, kunaweza kuwa na Mboni za Agryll Robertson ambazo ni mboni ndogo kwa macho zinazofinyika mtu anapotazama vitu vilivyokaribu, lakini hayafinyiki zikiwa wazi kwa mwanga mkali.

Kaswende ya moyo na mishipa kwa kawaida hutokea miaka 10 hadi30 baada ya maambukizi ya awali. Tatizo la kawaida kabisa ni ule wa kaswende ya kuvimba kwa aota, ambayo inaweza kusababisha aneurisimi kuundwa.[4]
Ya kuzaliwa nayo Kaswende ya kuzaliwa nayo inaweza kutokea wakati wa mimba au wa kuzaa. Theluthi-mbili ya watoto wazawa wanazaliwa bila dalili. Dalili ambazo huendelea zaidi ya miaka michache ya kwanza ya maisha ni pamoja na: kunenepa nenepa kwa ini au wengu (70%), upele (70%), joto jingi mwilini (40%), kaswende ya neva (20%), na ugonjwa wa mapafu kuvimba (20%). Ikiwa haita tibiwa, kaswende ya kuzaliwa ya baadae inaweza kutokea kwa 40 %, ikiwa ni pamoja na: pua lenye umbo la tandikoulemavu, Higoumenakis sign, saber shin, au Clutton's joints, miongoni mwa zingine

0 comments:

Post a Comment