Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Friday, June 13, 2014

THE FADHAGET INAPENDA KUKUPA DALILI ZA SARATANI YA KIZAZI SIKU YA LEO


Saratani ya kansa huwa na dalili zake za awali ambazo tutakuja kuziona. Tunapozungumzia saratani ya kizazi tunalenga zaidi saratani ya shingo ya uzazi ‘Carcionoma of Cerix’ na saratani ya mfumo wa uzazi au ‘Endometrial Carcinoma.

Saratani ya mfuko wa kizazi hushambulia zaidi tabaka la ndani la kizazi ‘Endometrium’ na kusababisha maumivu ya tumbo kwa muda mrefu na hata tumbo kuvimba.

Saratani hii siyo kubwa sana hivyo hatutaelezea kwa undani ila endapo utakuwa na maumivu chini ya tumbo na yanasambaa kulia na kushoto na upande wa juu, tumbo likiwa linaongezeka ukubwa na siku za hedhi zinavurugika, basi muone daktari wa kinamama kwa uchunguzi wa kina.

Saratani ya shingo ya uzazi huwapata wanawake walio katika umri wa kuzaa wenye wapenzi zaidi ya mmoja au ambao mara leo kaolewa na huyu,…


Saratani ya kansa huwa na dalili zake za awali ambazo tutakuja kuziona. Tunapozungumzia saratani ya kizazi tunalenga zaidi saratani ya shingo ya uzazi ‘Carcionoma of Cerix’ na saratani ya mfumo wa uzazi au ‘Endometrial Carcinoma.

Saratani ya mfuko wa kizazi hushambulia zaidi tabaka la ndani la kizazi ‘Endometrium’ na kusababisha maumivu ya tumbo kwa muda mrefu na hata tumbo kuvimba.

Saratani hii siyo kubwa sana hivyo hatutaelezea kwa undani ila endapo utakuwa na maumivu chini ya tumbo na yanasambaa kulia na kushoto na upande wa juu, tumbo likiwa linaongezeka ukubwa na siku za hedhi zinavurugika, basi muone daktari wa kinamama kwa uchunguzi wa kina.

Saratani ya shingo ya uzazi huwapata wanawake walio katika umri wa kuzaa wenye wapenzi zaidi ya mmoja au ambao mara leo kaolewa na huyu, anaachana naye anaishi na mwingine, yaani mara kwa mara hana msimamo, anabadilibadili wanaume, wanawake wanaofanya ngono na wanaume wasiofanyiwa tohara pia hupatwa na tatizo hili la saratani ya shingo ya uzazi.

Saratani ya shingo ya uzazi pamoja na kuchangiwa na mambo yote hayo hapo juu, husababishwa hasa na kirusi kiitwacho ‘Human Papilloma virus’ au kwa kifupi ‘HPV’. Kirusi hiki huenezwa kwa njia ya ngono, mwanaume huwa hakimuathiri bali yeye hukibeba na kukisambaza kwa wanawake kwa hiyo mwanamke anayechanganya wanaume hajui wapi atakipata.

Ukubwa wa tatizo
Saratani ya shingo ya kizazi ina tabia ya kusambaa endapo haitagundulika na tiba haitafanyika mapema. Saratani husambaa katika kizazi, nyonga hadi katika mapafu. Ikishambulia nyonga, mwanamke hulalamika maumivu chini ya tumbo.

Saratani hii ina tabia ya kusambaa kwa kasi na endapo hatua za haraka hazitachukuliwa husababisha kifo kwa mwanamke. Saratani huwa haiambukizi.

Dalili za awali za saratani ya shingo ya uzazi
Mwanamke mwenye tatizo hili hulalamika maumivu ya tumbo chini ya kitovu, kutokwa na majimaji yenye harufu ukeni na muwasho mara kwa mara. Tatizo hili hutibiwa na kujirudia tena mara kwa mara.

Mwanamke hulalamika kwamba ametibiwa sana kwa dawa za kumeza na kuingia ukeni lakini hapati nafuu. Hupoteza hamu ya tendo la ndoa, maumivu wakati wa tendo la ndoa na mwishowe hutokwa na damu ukeni baada ya tendo la ndoa.

Saratani inaposambaa na kushambulia shingo ya uzazi huathiri ukeni na kuumiza njia ya mkojo na kibofu.
Uke huvimba na kuonekana kuziba na mlango wa kizazi au ngozi ya ndani ya ukeni ikiguswa tu kidogo basi hutokwa na damu kwani huwa laini sana. Hii ni hatua mbaya na ya mwisho katika saratani inaposambaa.

Uchunguzi
Uchunguzi wa saratani ya shingo ya uzazi hufanyika katika vituo mbalimbali katika kampeni maalum dhidi ya saratani ya shingo ya uzazi.

Uchunguzi pia hufanyika katika hospitali za mikoa na wilaya katika kliniki za magonjwa ya kinamama ambapo vipimo mbalimbali hufanyika mojawapo ikiwa ni kuangalia mlango na shingo ya uzazi.

Kipimo cha Ultrasound pia kitafanyika kuangalia athari katika kizazi. Majimaji ya ukeni yatapimwa kuangalia maambukizi na uchunguzi wa awali wa saratani utafanyika.
Endapo mlango wa uzazi utakuwa umeathirika sana, basi kinyama kitatolewa na kupimwa katika maabara kubwa kuthibitisha tatizo.

Ushauri
Ni vema mwanamke yeyote anayejihisi maumivu chini ya tumbo na kutokwa na uchafu ukeni na muwasho uwepo au usiwepo awahi hospitali kwa uchunguzi. Waone madaktari wa kinamama kwa uchunguzi sahihi katika hospitali za mikoa.

0 comments:

Post a Comment