Wasiliana Nasi
Saturday, June 20, 2015
OMBI LA KUPANDA KWA BEI ZA MAJI SAFI NA MAJI TAKA
12:32 AM
No comments
Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Ewura, Simon Sayore, Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, Mhandisi, Mutaekulwa Mutegeki.
Wadau mbalimbli wakiwa katika mkutano huo.
Mkutano ukiendelea.
Mmoja wa wadau wa mkutano huo akichangia hoja.
Wadau wakisiliza hoja za mjumbe aliyekuwa akichangia hayupo pichani pamoja na viongozi wengine waalikwa.
MAMLAKA ya Udhibiti wa Maji Safi na Maji Taka (EWURA), leo imekutana na Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) pamoja na Dawasco juu ya kujadili ombi lililotolewa na Dawasa la pendekezo la kupandisha bei ya maji.
Mkutano huo uliofanyika katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam, Mgeni Rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadick huku ukihusisha wadau mbalimbali kutoka maeneo tofauti.
Akizungumza katika mkutano huo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Mhandisi, Mutoekulwa Mutegeki, alisema kuwa, Ewura ilianzishwa chini ya Sheria ya EWURA sura namba 414 ya sheria ya Tanzania iliyoanzishwa mwaka 2006 kwa madhumuni ya kuhakikisha huduma za maji, umeme, gesi na mafuta zinaimarika kwa kusimamia ubora na bei ya huduma kwa wadau wote na taifa kwa ujumla.
Mutegeki alisema kuwa mkutano huo ni sehemu ya uchunguzi unaofanywa na Ewura kupata maoni ya wadau wa huduma ya maji safi na maji taka kabla ya kutoa maamuzi kuhusu maombi yaliyowasilishwa na DAWASA ya kurekebisha bei za huduma za maji.
Mutegeki aliweza kutoa fursa kwa wadau wote walioweza kufika ukumbini hapo kutoa michango yao ya mawazo juu ya kupandisha ama kupunguza bei kutokana na huduma zinazotolewa na mashirika hayo hivyo mapendekezo hayo yatachukukuliwa kwa ajili ya kufanyiwa kazi.
Aidha kwa upande wa DAWASA, wameiomba EWURA kurekebisha bei za huduma zao kwa makundi yote ya wateja wao na kutaka marekebisho hayo kufanyika kwa kipindi cha robo ya mwisho wa mwaka wa fedha 2014/15 hadi mwaka wa fedha wa 2015/16.
Na Denis Mtima/ GPL
TIGO YATOA DOLA 150,000 KWA HOSPITALI YA CCBRT KUSAIDIA WATOTO WENYE MIGUU ILIYOPINDA
12:23 AM
No comments
Meneja Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana wakati wa hafla fupi ya kutiliana saini mkataba wa kusisaidia Hospitali hiyo. Kutoka kulia ni Ofisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa Hospitali ya CCBRT, Erwin Telemans na Daktari Bingwa wa Mifupa wa Hospitali hiyo, Prosper Alute.
Meneja Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez (wa pili kushoto), akibadilishana hati na Ofisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa Hospitali ya CCBRT baada ya kutiliana saini mkataba wa kusaidi matibabu ya ulemavu wa miguu Dar es Salaam jana. Kushoto ni Daktari Bingwa wa Mifupa wa Hospitali hiyo, Prosper Alute na Meneja Uwajibikaji kwa Jamii, Woinde Shisael.
Joyce Moshi akiwa amembeba mtoto wake Gedion ambaye anatibiwa katika Hospitali hiyo kutokana na miguu yake kupinda ambapo sasa anaendelea vizuri.
Na Dotto Mwaibale
HOSPITALI ya CCBRT, imepokea dola 150,000
(zaidi ya sh. mil. 320) kutoka kwa Kampuni ya Mawasiliano ya Tigo kwa
ajili ya kugharamia matibabu ya watototo wanaozaliwa na ulemavu wa nyayo
zilizopinda kwa miaka mitatu ijayo.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Meneja
Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez alisema hiyo si mara ya kwanza kwa kampuni
hiyo kugharamia matibabu ya walewavu kwani miaka mitatu iliyopita pia
waligharamia matibabu ya watoto wenye ulemavu wa midomo.
"Tuna amini watoto wenye ulemavu wa
unyayo uliopinda watapatiwa matibabu mapema, hivyo tunaomba wazazi wenye
watoto wao wanaozaliwa na ulemavu huo kujitokeza CCBRT kupatiwa
matibabu kwani ni bure na kwa mwaka tunatoa dola 500," alisema
Gutierrez.
Kwa upande wa Daktari wa Mifupa wa
hospitali hiyo, Prosper Alute akizungumzia ugonjwa huo, alisema
unasababishwa na kurithi kutoka kwa wazazi au ndugu na kunywa pombe
kupindukia au kutumia dawa zenye viambata kali.
Alisema asilimia 50 ya watoto wanaozaliwa
hupata ugonjwa huo kwa miguu yote ambapo tangu kuingia kwa mwaka huu
hadi Aprili, watoto 117 wamegundulika kuwa na ugonjwa huo ambao ni sawa
na wastani wa watoto 10 kwa wiki.
Alisema ugonjwa huo usipotibiwa kwa haraka unaweza kumsababishia mtoto kutembea kwa shida na wakati mwingine kutotembea kabisa.
Kwa upande wa Joyce Mosha, Mkazi wa
Mwenge, ni mmoja wa wazazi ambaye mtoto wake, Gidion ana miezi miwili
alikutwa na tatizo hilo na kufanyiwa upasuaji, alisema mara baada ya
kujifungua madaktari waligundua mtoto wake kuwa na tatizo hilo, hivyo
waliamua aanze kupatiwa matibabu.
"Namshukuru Mungu alifanyiwa upasuaji
mdogo na hivi sasa anaendelea vizuri, alipogunduliwa ana tatizo hilo
kwanza walimfunga plasta ngumu (POP) kwa wiki tano na kisha kumfanyia
upasuaji mdogo wa mfupa na kumpa viatu maalumu vya kuvaa na vingine huwa
anavaa usiku tu wakati wa kulala," alitoa ushuhuda Joyce.
ALIYETEKA ALBINO TABORA AFUNGWA JELA MIAKA 10
12:10 AM
No comments
Masanja Mwinamila (44) mara baada ya kufikishwa katika kituo cha Polisi Wilaya ya Nzega Juni 15, 2015.
Mtoto Margreth baada ya kufikishwa Kituo cha Polisi Wilaya ya Nzega usiku wa manane.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, ACP Juma Bwire akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na tukio hilo Juni 16, 2015.
Na Daniel Mbega, Nzega
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi
ya Wilaya ya Nzega leo hii imemhukumu Masanja Mwinamila (44), mkazi wa
Kitongoji cha Kona Nne, Kijiji cha Ugembe II, Kata ya Mwakashanhala,
Tarafa ya Puge wilayani Nzega katika Mkoa wa Tabora kwenda jela miaka 10
kwa kosa la kuteka mtoto mwenye albinism, Margreth Hamisi (6).
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo,
Saraphine Nsana, alitoa hukumu hiyo baada ya mshtakiwa kusomewa shtaka
na kukiri kutenda kosa hilo.
Ilielezwa mahakamani hapo kwamba, mnamo
Juni 15, 2015 majira ya saa 3:00 usiku katika Kijiji cha Ugembe II, Kata
ya Mwakashanhala wilayani Nzega, mtuhumiwa alimteka binti huyo kwa
lengo la kwenda ‘kumuuza’ ili ajipatie fedha (kiasi kimehifadhiwa).
Hii ni mara ya kwanza kwa kesi
inayohusisha utekaji nyara, kujeruhi na mauaji dhidi ya watu wenye
albinism kuchukua muda mfupi zaidi, kwani ndiyo kwanza kesi hiyo ya
Jinai Namba 116/2015 imefikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza na
kutolewa hukumu.
Jitihada za Polisi
Mafanikio ya kukamatwa kwa Masanja
Mwinamila akiwa katika harakati za kutaka kumuuza mtoto Margreth Hamisi,
ambaye ni mpwa wake, yametokana na umakini wa Jeshi la Polisi nchini
ambapo maofisa wake wa Kikosi Kazi cha Taifa waliweka mtego na
kufanikiwa kumnasa mtuhumiwa kabla hajamdhuru mateka wake.
Tukio hilo limefanikisha kuubomoa mtandao
hatari wa mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) kwani ni
takriban wiki tatu tu tangu maofisa usalama walipofanikiwa kuwanasa watu
wengine sita wakiwa katika harakati za kuuza mifupa inayodhaniwa kuwa
ya binadamu (albino) mjini Kahama Mei 22, 2015 ambapo tayari
wamekwishafikishwa mahakamani pamoja na wengine watatu waliokamatwa
baadaye.
Matukio hayo mawili makubwa yaliyotokea
katika kipindi hicho yamedhihirisha namna serikali kupitia jeshi hilo na
vyombo vingine vya usalama inavyoshughulikia mitandao hiyo hatari usiku
na mchana ili kuhakikisha Watanzania wote wanaishi kwa amani na
usalama.
Kukamatwa na hatimaye kuhukimiwa kwa
Masanja Mwinamila kumedhihirisha kwamba matukio mengi ya kuuawa au
kujeruhiwa kwa watu wenye albinism yanapangwa na kufanikishwa na
wanandugu wenyewe kwa sababu ya mawazo potofu ya kutafuta utajiri kwa
njia za mkato.
Kama alivyoeleza Kaimu Kamanda wa Polisi
Mkoa wa Tabora, ACP. Juma Bwire, Juni 16, 2015, Masanja alithubutu
kwenda kumnyakua mtoto huyo Margret Hamisi (6) majira ya saa 3 usiku na
kukimbia naye gizani akiwa na lengo la kumuuza ajipatie utajiri.
Lakini habari kutoka eneo la tukio
zinaeleza kwamba, haikuwa kazi rahisi kwa wanausalama kumwokoa binti
huyo akiwa hai na kumtia mbaroni mtuhumiwa, kwani walilazimika kujifanya
‘wanunuzi’ ili kuweka mtego wa kumkamata mtuhumiwa na kumwokoa mateka.
Taarifa za uchunguzi zinaeleza kwamba,
mtuhumiwa huyo alianza mchakato wa kutafuta ‘soko’ la kumuuza mtoto wa
dada yake mapema mwezi Juni 2015, lakini wasamaria wema wakawaarifu
wanausalama kuhusu kinachotaka kutokea katika eneo hilo.
Ilibidi maofisa wawili wa usalama
wapangiwe kazi ambapo mmoja alijifanya mnunuzi na mwingine mganga wa
jadi anayeambatana na ‘tajiri’ huyo feki ambao walikutanishwa na
mtuhumiwa huyo aliyewaeleza kwamba ‘dili la albino lipo’.
“Alisema kuna dada yake mwenye albinism
ambaye ana watoto wawili – wa kiume na wa kike – ambaonao wana albinism,
huyo dada ni mtoto wa baba yake mdogo ambaye alifariki mwaka jana
(2014), hivyo nyumbani hakuna mtu wa kiume wa kuleta upinzani.
“Akasema kwamba biashara hiyo ingefanyika
sana, kwani alipanga kuanza kumuuza mtoto wa kike, halafu angemuuza
yule wa kiume na hatimaye kummalizia dada yake!” kilisema chanzo cha
ndani kutoka eneo la tukio.
Kwa kawaida asilimia kubwa ya wakazi wa
Kanda ya Ziwa ni wapagani na wanawaamini waganga wa jadi kuliko mtu
yeyote, hiyo alipokutanishwa na watu hao wawili, mtuhumiwa Masanja
Mwinamila aliamini kila alichoambiwa na ‘mganga’.
Mganga huyo feki, mbali ya kumpigia ramli
na kumwogesha dawa kwenye njiapanda, alimtaka mtuhumiwa kuleta mtoto
huyo akiwa hai kwa maelezo kwamba inabidi ‘afanye tambiko ili dawa
zifanye kazi’, lakini lengo likiwa kumzuia mtuhumiwa asimdhuru mtoto na
hivyo kupata nafasi ya kumwokoa.
Akiwa na shauku kubwa ya kupata mamilioni
ya fedha, baada ya kukubali masharti ya mganga, Masanja alimuomba
‘tajiri’ atafute bunduki ili wakati yeye atakapomnyakua mtoto, wafyatue
risasi hewani kuwatisha watu watakaokimbilia eneo la tukio mara yowe
litakapopigwa.
Taarifa zinasema, wanausalama waliposikia
kauli hiyo wakahisi mtuhumiwa angeweza kwenda hata na panga na
kuwajeruhi watu atakaowakuta eneo la tukio ili amchukue mtoto, hivyo
mganga huyo akatoa masharti kwamba hata kama bunduki itapatikana, lakini
asingependa kuona damu inamwagika kwa yeyote huku akimwaminisha kwamba
dawa atakazoogeshwa zitamfanya awe ‘kiza’ asionekane na mtu yeyote.
Takriban mara tatu zoezi hilo
liliahirishwa kwa kuangalia mazingira ya kiusalama, lakini baada ya
wanausalama kujipanga vyema, ndipo Juni 15, 2015 wakafanikisha mtego huo
na kumkamata mtuhumiwa akiwa amembeba mtoto ambaye alinyakuliwa akiwa
usingizini.
“Ilikuwa ni kazi ngumu, lakini kama siyo
imani kwa mganga, ingekuwa hatari sana hata kwa wanausalama wenyewe.
Jamaa alipewa masharti kwamba, mtoto huyo anayeuzwa anatakiwa afikishwe
kwa mganga akiwa hai bila kujeruhiwa mahali popote; Familia
itakayovamiwa pia isimwage damu; Fedha za manunuzi kabla ya kukabidhiwa
mlengwa lazima zifanyiwe tambiko na masharti ya matumizi; hakutakiwa
kufanya zianaa siku nne kabla ya tukio; na lazima kuogeshwa dawa wale
wote watakaokwenda kwenye tukio,” kilifafanua chanzo kingine.
Bi. Joyce Mwandu Nkimbui (33), ambaye ni
mama wa Margret, anasema siku tatu mfululizo kabla ya tukio, mtuhumiwa
huyo ambaye ni kaka yake anayeishi jirani na hapo alikuwa akija asubuhi
na jioni akijifanya kuja kusalimia na wakati mwingine hata kupikiwa
chakula.
Hata hivyo, alishangaa kukuta kwamba
ndiye aliyevamia nyumbani kwao usiku wa Juni 15, 2015 na kumwamuru
asikimbie kabla yeye hajaingia ndani na kumkwapua mtoto.
“Walikuja usiku, sijui walikuwa wangapi,
lakini wakanilazimisha ‘wewe mama tulia’, nikaogopa na kukimbilia kwenye
majani, nikaanguka kwa sababu sioni vizuri usiku, nikakutana na
mwenyekiti wa kitongoji, ambaye tulikwenda naye nyumbani na kukuta
tayari mtoto hayupo,” Joyce alisema kwa masikitiko.
Matukio mbalimbali.
Tangu mwaka 2006 serikali imekuwa
ikipambana na matukio ya kuuawa na kujeruhiwa kwa watu wenye albinism
nchini, ambapo tayari watu zaidi ya 10 wamehukumiwa kunyongwa, wengine
kesi zao ziko mahakamani na watuhumiwa wengine wanaendelea kusakwa kwa
kuhusika na matukio hayo ya kutisha.
Wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku
ya wenye albinism duniani jijini Arusha Juni 13, 2015, Rais Jakaya
Kikwete alisisitiza kuwa kati ya watu 13 waliohukumiwa kunyongwa wawili
kesi zao zipo katika hatua ya mwisho kufikishwa kwake na kuahidi
zitakapofika mezani kwake atazitendea haki stahiki.
"Lakini mwaka 2014 hadi 2015 serikali
tumepambana na watu wakatili dhidi ya walemavu kwa kuwakamata watu
25 kati yao sita kesi zao zipo mahakamani, huku watano upelelezi
unaendelea na 11 wameachiwa huru kwa kutopatikana na hatia," alisema.
Rais Kikwete pia aliwahakikishia wenye
albinism kupatiwa vifaa vya kupambana na kansa ya ngozi bure kwenye
hospitali za serikali.
Mwaka 2009, Waziri Mkuu Mizengo Pinda
aliangua kilio bungeni kuonyesha uchungu alionao dhidi ya vitendo vya
mauaji ya kikatili ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino), na machozi
yake yakayeyusha hoja ya wabunge wa upinzani waliokuwa wamepania
kumbana, ili ajiuzulu kwa madai kwamba, alitoa amri ya kuua wauaji
ambayo ni kinyume na katiba ya nchi.
JENGO LA EKAMASUITES LODGE YA KIJITONYAMA DAR LATEKETEA KWA MOTO
12:05 AM
No comments
Jengo la nyumba ya wageni ijulikanayo kama Ekamasuites Lodge iliyopo kijitonyama jijini Dar, linavyoteketea kwa moto.
Jengo moja la Nyumba ya wageni ijulikanayo kama Ekamasuites Lodge iliyopo eneo la Kijitonyama karibu na Kituo cha Polisi cha Mabatini jijini Dar es Salaam, imeteketea vibaya kwa moto muda mfupi uliopita, Kikosi cha Zima Moto kimechelewa kufika eneo la tukio na taarifa zinasema, kikosi hicho ndipo kinawasili eneo hilo tayari kuuzima moto huo.
Friday, June 19, 2015
KUMUONA MTOTO WA ZARI, MIL.20
11:58 PM
No comments
AMA
kweli Mbongo-Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Mama Kijacho,
Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, sasa ni wa kimataifa zaidi ambapo
wakati mwanamama huyo akijiandaa kujifungua, tayari mtoto ajaye
ameandaliwa chumba maalum cha kulala na gharama za kumuona kwa
atakayehitaji picha hasa za kwenye vyombo vya habari, itakuwa si chini
ya Sh. milioni 20.
CHANZO KUTOKA WCB
Kwa mujibu wa chanzo makini ambacho kipo ndani ya Wasafi Classic Baby (WBC), Diamond na Zari wameamua kutenga chumba maalum cha mtoto wao atakapozaliwa.
Kwa mujibu wa chanzo makini ambacho kipo ndani ya Wasafi Classic Baby (WBC), Diamond na Zari wameamua kutenga chumba maalum cha mtoto wao atakapozaliwa.
MASHARTI YA KUMWAGA
Ilidaiwa kwamba, chumba hicho kitakuwa mahususi kwa mtoto tu na wala hakuna mtu mwingine atakaye ruhusiwa kuingia kumuona bila malipo zaidi ya mama, baba na familia yao ambao nao wataingia kwa sharti la kutopiga picha.
“Naona Zari anampeleka Diamond kimataifa kila kukicha maana nimeshuhudia chumba kina ‘full’ mazagazaga ya mtoto na nilipouliza nikaambiwa hicho ni chumba cha mtoto wa Zari mara tu atakapozaliwa.
Ilidaiwa kwamba, chumba hicho kitakuwa mahususi kwa mtoto tu na wala hakuna mtu mwingine atakaye ruhusiwa kuingia kumuona bila malipo zaidi ya mama, baba na familia yao ambao nao wataingia kwa sharti la kutopiga picha.
“Naona Zari anampeleka Diamond kimataifa kila kukicha maana nimeshuhudia chumba kina ‘full’ mazagazaga ya mtoto na nilipouliza nikaambiwa hicho ni chumba cha mtoto wa Zari mara tu atakapozaliwa.
“Kwa watu wa media (vyombo vya habari) lazima watoe si chini ya milioni 20 kwa picha na interview (mahojiano) na Zari.
KAMA KANYE NA KIM
“Wameamua kufanya hivyo ili kuendana na wasanii wengine wa Marekani kama Kanye West na Kim Kardashian au Jay Z na Beyonce ambao wamekuwa wakifanya hivyo.
“Wameamua kufanya hivyo ili kuendana na wasanii wengine wa Marekani kama Kanye West na Kim Kardashian au Jay Z na Beyonce ambao wamekuwa wakifanya hivyo.
ULINZI USIPIME
“Nimeshuhudia hadi vitu vya mtoto na kitanda chake tayari vimeshaandaliwa mara tu mtoto atakapokuja atakuwa katika chumba hicho ambacho kipo ndani ya mjengo wao, Madale (Tegeta, Dar). Unaambiwa ulinzi utakuwa mkali usipime.
“Nimeshuhudia hadi vitu vya mtoto na kitanda chake tayari vimeshaandaliwa mara tu mtoto atakapokuja atakuwa katika chumba hicho ambacho kipo ndani ya mjengo wao, Madale (Tegeta, Dar). Unaambiwa ulinzi utakuwa mkali usipime.
BABA KIJACHO ANASEMAJE?
Baada ya kunyetishiwa mchongo huo, gazeti hili lilimtafuta Baba Kijacho, Diamond ili kuthibitisha ishu hiyo ambapo alisema ni kweli wameshaandaa chumba maalum kwa ajili yake, mara tu atakapozaliwa na kwamba haitaonekana sura yake kwani kutakuwa na bei maalum kwa yoyote atakayehitaji kumuona.
Baada ya kunyetishiwa mchongo huo, gazeti hili lilimtafuta Baba Kijacho, Diamond ili kuthibitisha ishu hiyo ambapo alisema ni kweli wameshaandaa chumba maalum kwa ajili yake, mara tu atakapozaliwa na kwamba haitaonekana sura yake kwani kutakuwa na bei maalum kwa yoyote atakayehitaji kumuona.
“Yeah! Ni kweli kuna chumba chake maalum na pia haitaonekana sura
yake maana kutakuwa na bei maalum kwa magazine au televisheni
itakayohitaji kuwa na ‘exclusive’ ya kuonesha sura yake kwa mara ya
kwanza.
“Bei ya mtu kumuona au kwa vyombo vya habari, hiyo itategemea na ukaribu wetu na chombo husika kitakachokuwa kikihitaji kurusha habari ya mtoto wetu,” alisema Diamond anayesumbua na kibao chake kipya cha Nana.
“Bei ya mtu kumuona au kwa vyombo vya habari, hiyo itategemea na ukaribu wetu na chombo husika kitakachokuwa kikihitaji kurusha habari ya mtoto wetu,” alisema Diamond anayesumbua na kibao chake kipya cha Nana.
DIAMOND PRESHA TUPU
Diamond kwa sasa yupo kwenye presha kubwa ya kuomba mashabiki wake wampigie kura kwa wingi katika Tuzo za MTV (Mama’s) baada ya kuteuliwa kuwania Vipengele vya Msanii Bora wa Kiume Afrika, Mtumbuizaji Bora wa Kiume Afrika na Nyimbo Bora ya Kushirikiana Afrika.
Diamond kwa sasa yupo kwenye presha kubwa ya kuomba mashabiki wake wampigie kura kwa wingi katika Tuzo za MTV (Mama’s) baada ya kuteuliwa kuwania Vipengele vya Msanii Bora wa Kiume Afrika, Mtumbuizaji Bora wa Kiume Afrika na Nyimbo Bora ya Kushirikiana Afrika.
ZARI ATAJIFUNGUA LINI?
Kwa upande wake, Zari anatarajiwa kujifungua mtoto wa kike kuanzia Agosti, mwaka huu na kuendelea.
Kwa upande wake, Zari anatarajiwa kujifungua mtoto wa kike kuanzia Agosti, mwaka huu na kuendelea.
Subscribe to:
Posts (Atom)




















