Wasiliana Nasi
Friday, May 20, 2016
Friday, March 25, 2016
Huduma Ya The Fadhaget Sanitarium Clinic Imezidi Kukua kwa Kasi sana. Zifahamu Sababu zake.
The Fadhaget Sanitarium Clinic imezidi kuongeza matawi yake kote nchini. Hii ni kutokana na ubora ambao imekuwa ikitoa kwa wateja wake. Tunajitahidi sana kuhakikisha kuwa tunawasaidia watu mbalimbali wanaofika kwetu na tumehakikisha huduma yetu ikiwafurahisha. Tunazidi kuongeza ubora wetu na tunazidi kuhakikisha kuwa watu wengi wanapona na kufurahia Afya zao tena. Waliokata tamaa katika magonjwa ya uzazi, jinsia, magonjwa sugu na ambayo imeshindikana kutibu, tumejitahidi kuwasaidia wengi.
Tunapenda kuzidi kuwakaribisha na msisite kufika ofisini kwetu na tutakusaidia. Kama hufahamu tunapatikana wapi, tembelea Blog yetu, kwenye Menu (Juu) utaona tunapatikana wapi, fungua link na utaona mpaka Picha za majengo yetu na maelekezo yake. Pia tumeweka na namba za simu kwa watakaotaka kuonana au kuwasiliana nasi watutafute nasi bila shaka tutawaelekeza vyema.
Asanteni sana na endeleeni kujali Afya zenu kwa Mimea na Matunda mbalimbali. Chakula ni Dawa nzuri.
Wednesday, January 20, 2016
Je unafahamu Undani Kuhusu Endometriosis?
7:14 AM
No comments
Je unafahamu Undani Kuhusu Endometriosis? Dr Fadhili Emily ameelezea vyema matatizo hayo na jinsi ya kudhibiti. Tazama video za mafunzo ya kiafya kupitia Channel Hii ya Dr. Fadhili Emily na pia Fuatilia habari zaidi katika account yake ya instagram ya @fadhaget.
Friday, January 1, 2016
Tunapenda kuwatakia Heri ya Mwaka Mpya
Kitengo Cha Sayansi ya Tiba Asilia, The Fadhaget Sanitarium Clinic kinapenda kuwatakia Heri na Baraka za Mwaka Mpya. Tutazidi kuboresha huduma zetu pote nchini kwa kusaidia wenye matatizo mbalimbali ya kiafya kwa kutumia Tiba Asilia Kutibu.

Tuesday, December 29, 2015
Monday, December 21, 2015
Sunday, December 6, 2015
Dr. Fadhili Emily Kwenye Mkutano na Resolution Insurance.
Dr. Fadhili Emily akiiwakilisha The Fadhaget Sanitarium Clinic wiki hii alishiriki katika moja ya mkutano ulioweza kutoa elimu kuhusiana na Insurance za Afya. Katika wiki hii aliweza kuonea na kutoa elimu kuhusiana na Madhara ya Matumizi ya simu za mikononi na adhari zake pamoja na njia sahihi za kutumia simu za mikononi kiuslama.
Friday, November 13, 2015
Maumivu ya Tumbo ya Mata kwa Mara kwa Wanawake.
3:40 AM
No comments
Wanawake wanaosumbuliwa na maumivu ya tumbo chini ya kitovu mara kwa mara hupata athari nyingi baadaye endapo kama hawatagundua chanzo cha maumivu hayo.
Katika tumbo la mwanamke kuna mfumo wa kawaida wa tumbo ambao ni tumbo la chakula na mfuko wa haja kubwa, kuna kibofu cha mkojo na mfumo wa mkojo.
Pia kuna mfumo wa uzazi ambao ndiyo tunaozungumzia leo kwa undani.
Mfumo wa chakula una matatizo yake mengi ambayo huambatana na kichefuchefu na kufunga choo, mfumo wa mkojo nao una shida nyingi tu ambazo ni maambukizi au ‘UTI’ au Yutiai ambayo huambatana pia na maumivu katika njia ya mkojo.
Matatizo ya mfumo wa uzazi huambatana na dalili mbili, mojawapo ni ile ya kutokwa na uchafu ukeni.
Chanzo cha tatizo
Maumivu ya mara kwa mara ya tumbo kwa wanawake yanahusiana zaidi na mfumo wa uzazi. Maumivu haya yanaweza kuwa maambukizi katika mfumo wa uzazi ambayo huathiri kuta za ndani za uzazi, maambukizi yanasambaa hadi katika mirija ya uzazi hali iitwayo ‘Salpingitis’ na huweza kusababisha mirija kujaa maji ‘Hydrosalpinx ’ au kujaa usaha ‘Pyosalpinx’.
Maambukizi pia husambaa hadi katika vifuko vya mayai ‘Oophoritis’.
Maambukizi pia huwa ukeni na kitaalamu huitwa ‘Vaginitis’ na hushambulia kuta za uke, yakifika katika mlango wa shingo ya kizazi huitwa ‘Cervicitis’.
Pamoja na kushambulia ndani ya uke na shingo ya kizazi, pia hushambulia nje kabisa ya uke ambapo mwanamke hulalamika muwasho nje ya uke kwenye midomo au mashavu ya uke na hata kutokwa vipele.
Dalili za tatizo
Mwanamke mwenye tatizo ukeni hulalamika muwasho ukeni na kutokwa na uchafu ambao mara nyingi huwa na harufu kama shombo la samaki. Pia hulalamika maumivu wakati wa tendo la ndoa.
Mwanamke ambaye maambukizi yamefika katika mlango wa shingo ya kizazi hupatwa na maumivu wakati wa tendo la ndoa na wakati mwingine hutokwa na damu wakati wa kujisafisha huona damu kidogo au kama hakuna damu atahisi mdomo wa kizazi umevimba na kushika kitu kama kigololi ndani ya uke.
Mwanamke pia hulalamika kama kuna kitu kinasukumwa wakati wa tendo la ndoa.
Maumivu ndani ya kizazi hasa katika kuta za ndani hupatwa na maumivu baada ya tendo la ndoa, vilevile hupatwa na maumivu chini ya tumbo muda wote yaani kila siku na kumnyima raha. Maumivu wakati wa hedhi na kutokwa na damu nzito nyeusi na wakati mwingine hutoa harufu.
Maumivu yakiwa katika mirija ya uzazi husambaa chini ya tumbo kulia na kushoto, maumivu pia huwa ya muda mrefu na hali hii humfanya mgonjwa apate haja kubwa kwa shida.
Maambukizi katika vifuko vya mayai husababisha siku za hedhi zivurugike na ziwe hazina mpangilio maalum, huathiri upevushaji na uzalishaji wa mayai hivyo kushindwa kupata ujauzito.
Maambukizi nje ya kizazi humfanya mwanamke aumwe tumbo lote na kupata hali iitwayo ‘Perionitis’, hupata homa za mara kwa mara na mwili kuwa mnyonge.
Maumivu ya muda mrefu hudhoofisha afya ya mwanamke, hukosa hamu ya kula na kupoteza raha ya tendo la ndoa na uzazi husumbua.
Maambukizi hushambulia kwa njia ya kupitia ukeni, mfano magonjwa ya ngono, kuharibika au kutoa mimba na hata kwa kufanyiwa upasuaji wa tumbo pia huathiri mfumo wa uzazi.
Vyanzo vingine vinavyoathiri mfumo wa uzazi na kusababisha maumivu ya chini ya tumbo mara kwa mara ni matatizo katika mfumo wa homoni au vichocheo, uvimbe katika kizazi, mirija na vifuko vya mayai.
Athari za tatizo
Maambukizi sugu katika mfumo wa uzazi huathiri mzunguko wa hedhi, uzalishaji mayai ya uzazi, kuziba mirija ya uzazi, kupoteza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa.
Kwa ujumla mwanamke mwenye tatizo hili anaweza kupoteza uwezo wa kuzaa na kuwa mgumba.
Matatizo haya hutokea zaidi kwa mwanamke aliye katika umri wa kuzaa.
Uchunguzi
Matatizo haya hufanyiwa uchunguzi katika kliniki za magonjwa ya kinamama. Vipimo mbalimbali vitafanyika kadiri daktari atakavyoona inafaa.
Matibabu Tiba inaweza kuwa dawa, upasuaji au yoyote ambayo daktari ataona inafaa kutegemea aina na ukubwa wa tatizo.
Sunday, November 8, 2015
Subscribe to:
Posts (Atom)


















