Karibu Fadhaget Sanitarium Clinic

Tunapenda kukukaribisha katika Kitengo cha Sayansi ya Tiba Asilia.

Kitengo Cha Sayansi Ya Tiba Asilia

Kwa Muda mrefu tumekuwa tukisaidia wengi katika matibabu na kutengeneza dawa bora kabisa kiafya.

Je Unapenda Kufahamu Jinsi Ya Kupata Mapacha?

Tunafundisha jinsi ya kupata jinsia unayotaka, jinsi ya kupata mtoto kama umekosa mtoto kwa muda mrefu. Pia hata jinsi ya kupata watoto mapacha tunaweza kukusaidia.

Tunapatikana Katika Mikoa Zaidi ya 10 Tanzania

Tunazidi kuongeza matawi yetu nchini Tanzania na Nje ya Nchi. Kwa sasa tunapatikana katika mikoa zaidi ya 10 na tunazidi kuongeza matawi yetu. Karibu sana.

Wasiliana Nasi

Wasiliana Nasi

Friday, June 12, 2015

TANZIA: MENEJA WA JAMBO LEO, RAMADHANI KIBANIKE AFARIKI DUNIA



Marehemu Ramadhani Kibanike enzi za uhai wake.


Mhariri Mkuu wa Gazeti la Jambo Leo, Julian Msacky na Mwandishi wa Habari, Stela Kessy (kulia), wakiendelea na kazi huku wakiwa na huzuni baada ya kupokea taarifa ya kifo cha Kibanike jana jioni.

Mwanahabari Celina Mathew akilia kwa uchungu baada ya kupokea taarifa hiyo.

Ofisa Matangazo, Kinai akiwa amepigwa butwaa kutokana na kifo hicho.


Wanahabari Nyendo Mohammed (katikati), Edith Msuya (kulia) na Magendela Hamisi wakiwa katika hali ya huzuni kufuatia kifo hicho.

Mwanahabari Magendela Hamisi akitafakari juu ya kifo hicho.

Msanifu kurasa wa gazeti la Jambo Leo, Elizabeth Mkeleja alishindwa kujizuia kulia.

Dereva wa Ramadhani Kibanike akiwa katika huzuni baada ya kupokea taarifa ya kifo hicho.

Mwanahabari Grace Gurisha akisaidiwa na wenzake baada ya kuishiwa nguvu muda mfupi baada ya kupata taarifa hizo za kifo cha Ramadhani Kibanike.


Na Dotto Mwaibale

KAMPUNI ya JL Comunications inayochapisha magazeti ya Jambo Leo, Staa Spoti, imepata pigo baada ya aliyekuwa Meneja wake Mkuu, Ramadhani Kibanike kufariki.
Kibanike alifariki dunia jana mchana nyumbani kwake Tabata Kimanga jijini Dar es Salaam, baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Akitoa taarifa ya kifo hicho kwa wafanyakazi wa kampuni hiyo, Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Theophil Makunga alisema Kibanike alikumbwa na mauti jana mchana.

Mipango ya mazishi bado inapangwa, na msiba upo nyumbani kwa marehemu Tabata Jijini Dar es Salaam.
(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com)

THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC NI MOJA YA WAFADHILI WA TAMASHA KUBWA LA FLORA MBASHA


DAKTARI: KAJALA HAWEZI KUZAA TENA!

Imelda mtema
MAJANGA juu ya majanga! Siku chache kufuatia kufanyiwa kipimo na kubainika kuna tatizo kwenye ubongo baada ya kupigwa chupa kichwani kwenye Klabu ya New Maisha, Masaki jijini Dar, mkali wa sinema za Bongo, Kajala Masanja ‘Kay’ amepata pigo lingine la daktari kumwambia hawezi kuzaa tena!


Mkali wa sinema za Bongo, Kajala Masanja ‘Kay’.

Kwa mujibu wa chanzo makini, Kajala alipewa maelezo hayo mapema wiki hii baada ya kufanyiwa kipimo na daktari bingwa wa hospitali moja iliyopo maeneo ya Morocco jijini Dar.

HISTORIA YA TATIZO
Kwa mujibu wa chanzo hicho, awali staa huyo alikuwa akisumbuliwa na tatizo la maumivu makali ya tumbo kwa kipindi kirefu na mara kwa mara hali iliyomlazimu kwenda kwenye hospitali mbalimbali za jijini Dar na kutibiwa lakini bila mafanikio.

“Unajua awali, aliamini amepata vidonda vya vitumbo (Ulcers).
“Pamoja na kupewa dawa mbalimbali kama ‘antibiotic’ kama Amoxicillin, Tetracycline, Clarithromycin na Metronidazole, dawa zenye uwezo wa kupunguza uzalishaji wa tindikali tumboni lakini wapi.

HALI YAZIDI KUWA MBAYA
“Kutokana na hali yake kuzidi kuwa mbaya ndipo mwanzoni mwa wiki hii alipojisikia maumivu ya kupindukia hivyo alikwenda kwenye hospitali ile iliyopo Morocco na majibu ya vipimo yakaonesha kuwa ana uvimbe mkubwa kwenye kizazi!” Kilisema chanzo hicho.

Mnyetishaji wetu alidai kuwa, daktari huyo alimshauri kufanyiwa upasuaji wa haraka ili kuondoa uvimbe huo kwa sababu anaweza pia kunyemelewa na tatizo la kansa achilia mbali ishu ya kutozaa tena.

KAJALA AISHIWA NGUVU
“Yaani Kajala aliishiwa nguvu kabisa alipoambiwa maneno hayo na kujikuta akimwaga machozi,” kilisema chanzo hicho.

KAJALA ASAKWA KUTHIBITISHA
Baada ya gazeti hili kupata habari hiyo, lilimtafuta Kajala ambapo alikiri kukutwa na tatizo hilo na ni kitu ambacho kimemchanganya sana hasa akimwangalia binti yake Paula (aliyezaa na Prodyuza wa Bongo Records, Paul Matthyasse ‘P Funk’), bado mdogo hivyo kujikuta akidondosha chozi.

“Yaani mtu akikuambia una ugonjwa kama huo, lazima uumie kwa kweli na mara nyingi namfikiria mtoto wangu bado mdogo. Kwa sasa najitahidi kufanya matibabu ya haraka ili kuondoa tatizo hilo,” alisema Kajala.

Kajala Masanja ‘Kay akiwa na mwanaye.

KITAALAM
Kwa mujibu wa daktari mmoja wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ambaye aliomba jina kusitiriwa, mwanamke akiwa na uvimbe mkubwa kwenye mfuko wa uzazi na kwa muda mrefu, matibabu yake salama ni kukiondoa kizazi.
“Lakini kuna wanawake wanapatwa na vimbe mbalimbali kwenye mfuko wa kizazi lakini si kubwa, ni rahisi kuondoa kwa kuchubua kitaalam na kizazi kikabaki salama,” alisema daktari huyo.

WEMA BILA KUJALI
Wakati huohuo, Kajala amekumbwa na janga baada ya aliyekuwa shosti wake wa kufichiana siri kama siyo kutunziana mambo yao ya ndani, Wema Sepetu kumpaka runingani!

Baada ya Kajala kujishusha akisema yupo tayari kupatana na mwenzake, Wema, mwanadada huyo amemshukia Kajala akimwita ‘bogasi’ yaani mjinga na kwamba ni mtu mzima lakini hana akili.

Akizungumza kupitia Clouds TV Jumanne iliyopita, Wema alifunguka kwamba hivi karibuni alishangazwa na kitendo cha Kajala kuandika vitu vya ajabu kwenye ukurasa wake wa Mtandao wa Instagram akisema amejishusha kumuomba msamaha ili aonewe huruma kwa watu na yeye (Wema) aonekane kuwa hafai.
Mkali wa sinema za Bongo Wema Sepetu.

“Kabla ya kuandika vile nilikuwa nipo tayari hata akija kwangu nimkaribishe nimsikilize lakini kwa sasa sitaki kuambatana na Kajala.“Kajala ni mtu mzima lakini hana akili. Kuwa na Kajala ulikuwa ni upepo tu unapita. Alichokifanya mimi namuona bogus,” alisema Wema.

Kwa upande wake, Kajala alimjibu kwa kifupi bila kutaka kubebanisha maneno kwa kusema: “Siku zote duniani ukikimbizana na chizi na wewe utaonekana chizi, nimejishusha, nimechoka.”

PENNY: MITANDAO ILITAKA KUNITOA UHAI WANGU

Ndani ya safu hii leo tunakutana na Mtangazaji Penniel Mungilwa ‘Penny’ ambaye yuko kimya katika masuala ya utangazaji tangu alipoamua kuondoka Radio E FM.


Mtangazaji Penniel Mungilwa ‘Penny’.

Msikilize Penny alipobanwa kwa maswali kumi na Mwandishi Wetu Imelda Mtema.
Ijumaa: Upo kimya sana shosti, ni nini unachofanya kwa sasa?
Penny: Sasa hivi mimi ni mbunifu wa mpangilio wa nyumba na ofisi ambapo namshauri mtu aiwekeje nyumba yake katika muonekano mzuri wenye mvuto pamoja na ofisi kwa ujumla.

Ijumaa: Mambo ya utangazaji umeachana nayo au una mpango wa kusaka kazi sehemu nyingine?
Penny: Unajua hakuna kitu kizuri kama mtu kuwa na taaluma yako kichwani, yaani hata kama nitakaa miaka kumi bado fani yangu itakuwa ni utangazaji.

Ijumaa: Kuna tetesi kuwa ukikasirishwa tu na mpenzi unakimbilia kunywa sumu, ni kweli?
Penny: (kicheko) Hao wanaosema hivyo watakuwa wananijua sana kuliko mama yangu, siko hivyo wanavyodai jamani.
Ijumaa: Mwanaume ambaye uliamua kumuweka wazi alikuwa ni Diamond tu, kwa nini sasa hivi unaficha?
Penny: Unajua kuna mwanaume mwingine hapendi mambo ya kujulikana kwani wote siyo mastaa.

Ijumaa: Kwa sasa wewe na Wema ni marafiki, je mkikaa huwa hamuongelei mambo ya mpenzi wenu aliyepita?
Penny: Hakuna kitu kama hicho, sisi huongelea mambo yetu binafsi kwani urafiki wetu ni tangu kitambo.
Ijumaa: Kuna kipindi ulivalishwa pete ya uchumba na ulikuwa mbioni kuolewa, ilikuwaje?

Penny: Ni kweli na lengo bado liko palepale, ikifika muda nitaolewa kwani sijatangaza kama tumeachana.
Ijumaa: Kuna kipindi ulikutana na mtihani kupitia mitandao ya kijamii, ulijifunza nini?
Penny: Nilichojifunza ni kwamba watu wengi wanaotumia mitandao ya kijamii wanakurupuka na hawana utu kwani wanaweza kupoteza uhai wa mtu kama hayuko imara.

Ijumaa: Ulishafikiria kutoa uhai wako kwa ajili ya mitandao ya jamii?
Penny: Nilishawahi kuwaza nijiue lakini namshukuru sana mama yangu aliniambia kuwa hakuna kitu ambacho hakiwezi kuisha hata siku moja.

Ijumaa: Unazungumziaje bifu la Kajala na Wema?
Penny: Mimi ninachojua wale ni marafiki wanaopendana sana, ipo siku tofauti zao wataweka pembeni kwa sababu siku hizi hakuna haja ya kuwekeana mabifu.

Ijumaa: Ulishawahi kwenda kwa mganga kwa kusaka mafanikio au jambo lolote?
Penny: Siku zote katika maisha yangu mganga wangu ni Mungu maana ananijibu kwa haraka sana, sijawahi kumtegemea mganga wala hilo halitatokea.

WAGOMBEA URAIS WAMIMINIKA KWA MTABIRI

Gladness Mallya na Mayasa Mariwata

MAJANGA! Wakati vuguvugu la kutangaza nia ya kugombea nafasi ya urais likiendelea, imegundulika kuwa wagombea wengi wa urais wamekuwa wakimiminika kwa mtabiri maarufu Bongo, Maalim Hussein Yahaya, (pichani) maeneo ya Magomeni Mwembechai jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kutabiriwa safari yao hiyo, Ijumaa lina mkanda kamili.

Mtabiri maarufu Bongo, Maalim Hussein Yahaya.

Gazeti hili lilifanya uchunguzi wa kina baada ya kupata habari kutoka kwa watu wanaoishi jirani na mtabiri huyo kwamba wagombea kibao wanamiminika kwake ambapo lilifanikiwa kuwaona baadhi (majina tunayaifadhi) wakiingia katika ofisi ya mtabiri huyo kutabiriwa mambo yao kuelekea kwenye kugombea nafasi ya urais.

Mgombea mmoja alifika kwa mtabiri huyo akiwa katika gari la lenye vioo vyeusi (namba zake zinahifadhiwa) na aliongozana na mpambe mmoja.Mgombea urais mwingine aliyekuwa na nywele ndogo alifika katika ofisi za mtabiri huyo akiwa na mwanamke, haikuweza kufahamika kama ni mkewe au la.


Lowassa

“Hao mliowaona ni wachache mbona hapa wanapishana usiku na mchana na wengine wengi wanaogopa kuja mchana wanamuomba mtabiri abaki mpaka usiku mwingi ndiyo wanakuja, yaani hawa wagombea urais wanahangaika kweli,” alisema jirani mmoja kwa sharti la kutotajwa jina.

Baada ya uchunguzi huo, mapaparazi wetu walifika ofisini kwa mtabiri huyo na kumuuliza kuhusu wagombea wanaofika kwake kwa ajili ya kutabiriwa mambo yao kuhusu urais ambapo maalim Hassan alikuwa na haya ya kusema:

“Ni kweli wanakuja wengi sana lakini siwezi kukutajia majina yao maana ni kinyume cha maadili ya kazi yangu.
“Kwenye astrology (unajimu), kuna mengi na ndiyo maana wanakuja kwangu.


Membe.

Nikufahamisheni tu kwamba enzi hizo baba yangu Sheikh Yahya Hussein alikuwa anawatabiria marais kama vile Jomo Kenyatta (Kenya), Wiliam Tolbert (Liberia), Mfalme Sebhuza (Swaziland) na kadhalika, kwa hiyo siyo ajabu hawa kuja kwangu,” alisema Maalim Hassan.
Picha zilizotumika mbele za wagombea siyo waliokwenda kwa mtabiri.

JINSI YA KUKABILIANA NA TATIZO LA KUZIBA KWA MIRIJA YA UZAZI

Hili ni tatizo linalosababisha ugumba kwa wanawake kwa kiasi kikubwa. Wanawake wanaoshindwa kupata ujauzito hukabiliwa na matatizo matatu; Kwanza kabisa ni kuziba kwa mirija ya mayai kama tutakavyoona leo na pili ni matatizo katika mfumo wa homoni ambapo kuna sababu zake tutakuja kuziona katika matoleo yajayo.

Hata hivyo, dalili kuu ni kuvurugika kwa mzunguko wa hedhi, kutopata hedhi na kupata damu kwa muda mrefu au muda mfupi sana ambazo ni siku moja au mbili.

Dalili nyingine ambazo siyo nzuri katika mfumo wa homoni ambazo zinaweza kufanya mwanamke asipate mimba ni matiti kutoa maziwa wakati siyo mjamzito na wala hana mtoto anayenyonya.

Tatizo lingine la tatu ni kwa upande wa mwanaume kutokuwa na mbegu zenye ubora.
Yaani hana nguvu za kutosha au anawahi kumaliza tendo la ndoa ‘premature ejaculation’ kama tulivyoona hapo awali.
Kuziba mirija ya uzazi huzuia mbegu na mayai kukutana na kutungisha mimba. Mirija ya uzazi pia huitwa Oviducts, Uterine tubes au Salpinges.

AINA ZA UZIBAJI WA MIRIJA
Tumeona sababu kuu tatu zinazomfanya mwanamke asipate mimba. Kuziba kwa mirija ya uzazi huchukua asilimia ishirini ya tatizo la ugumba kwa mwanamke au mwanamke kupoteza uwezo wa kuzaa, pamoja na hizo sababu tatu, pia zipo sababu nyingine ndogo nyingi ambazo tutakuja kuziona kwa undani katika uchambuzi ujao.

Aina za uzibaji ni mirija kuziba upande wa mwishoni karibu na vifuko vya mayai ‘Distal tubal occlusions.’
Hali hii inahusiana kabisa na tatizo la mirija kuvimba au kujaa maji hali iitwayo kitaalamu Hydrosalpinx ambapo pamoja na mwanamke kushindwa kupata mimba, pia husumbuliwa na maumivu ya tumbo chini ya kitovu mara kwa mara yanayosambaa kulia na kushoto.

Hali ya kuvimba kwa mirija au mirija ya uzazi kujaa maji husababishwa na maambukizi ya vimelea vya ‘Chlamydia trachomatics’.

Katika hali hii pia huweza kutokea hali ya kizazi na viungo jirani kushikamana hivyo mirija pia hushikwa na kuziba.
Hali hii ya kuziba mirija mwishoni husababisha sehemu ya mirija iliyo kama vidole iitwayo ‘fimbriae’ kugandamana na kusababisha kushindwa kuchukua yai lililopevuka na kuliingiza katika mirija tayari kwa kutungisha mimba. Tatizo hili linapotokea, sehemu nyingine ya mirija inakuwa wazi au nzima. Mrija unaweza kuziba katikati ‘midsegment’ ambapo sababu kubwa inaweza kuwa mrija kufungwa au kukatwa kama njia ya kufunga uzazi. Mrija unaweza kuziba mwanzoni na sababu kubwa ni maambukizi kwenye kizazi kutokana na utoaji au kuharibika mimba na maambukizi mengine sugu ya kizazi.